Makame Mbarawa aiwakia ATCL

Makame Mbarawa aiwakia ATCL

Amuagiza Mkurugenzi kubadilisha safu yake mara moja.

Aonya watu waache upigaji wawe waadilifu.

Marketing Department yakosolewa. Awataka ambao hawawezi kuendana na kasi inayotakiwa wakae pembeni.

Asema wafanyakazi wa serikali watumie ATCL kusafiri Posta na TTCL zijiandae.

My take..

Kwakweli Marketing Department ya ATCL ni mbovu sana, namuunga mkono. Nenda twitter account yao au hata website yao. Dah! Inasikitisha.


----------------------------------------------------------
Zanzibar ASP Ameongezea maoni yake hapo chini...

Tatizo la ATCL ni kubwa sana kuliko vile watu wanavyodhania.Ni shirika lililoanzishwa kisiasa, Linafanya kazi kisiasa, Lilikufa kisiasa na sasa linafufuliwa kisiasa. Siasa na Biashara ni kama Maji na Mafuta, huwa haviendani kabisa.Yaani, Waziri Mzima anasema, uwekwe utaratibu ili wafanyakazi wa serikali wanaposafiri kwa Ndege basi Walazimishwe kupanda ndege za ATCL pekee!! Sijui kama waziri anajua athari za kauli yake kwa makampuni mengine ya ndege, Ubora wa Huduma za ATCL, Wajibu wa mfanyakazi wa serikali nk.Sijawahi kuona siasa ikifanikisha biashara.Ni suala la muda tu, ATCL itakufa tena, na tutaendelea kumsaka mchawi milele.... Anayeiloga ATCL ni serikali yenyewe.


Chanzo: TBC 1
Haha..Hawa watu wanaumia sana precisionair kuruka kwa mafanikio. Wameiga sana vita kwa kila namna, sasa wameamua kabisa kununua ndege kwa akili zao. Shida ni ktk ajira, niliwaambia watu, kubagua kanda yenye mafanikio ni kujiumiza. Tatizo jingine ni utawala uliopo ndio kabisa,una hofu na kanda ya kaskazini, kila angle wanaogopa kivuli cha hawa jamaa. Ktk siasa wanaogopa watahujumiwa, ktk Ndege wanaogopa watahujumiwa eti precisionair itapewa chapuo, ktk mawasiliano hivyo hivyo.Mwisho wa siku ni kuweka watu wanaofanya maigizo kila angle. Hii nchi ipo siku itakabidhiwa kwa wachapa kazi kiroho safi, wabaguzi watakuwa chalii wenyewe.
 
Wazalendo tupi tena wengi tu tutazioanda. Nakumbuka niliwahi kufanya kazi navwaswed. Ole wako umkatie tiket nyingine zaisi ya Aitr Tanzania. Lakini waTanzania wenyewe kawana mwanzo mwisho dah.
Aisee ulikua usingizini?
 
Mkuu hata TTCL itafuata mkumbo huo huo - makampuni ya simu nchini yatahakikisha Shirika hilo linabaki kulinda Mkonga wa mawasiliano na kuuza bundles za internet basi!!! Hakuna dalili zozote za kuonyesha Serikali yetu imekwisha lishtukia hilo - wasipo kuwa makini miaka itakatika bila shirika kuonyesha ushindani wa kweli na makampuni ya simu ya watu binafsi, wakati wao ndiyo wanapashwa kuwa kimbilio la raia walio wengi.
Mnakosea sana kudhani mchawi ni hao sekta binafsi. Yaani serikali ina usalama wa taifa unadhani wasingejua wanahujumiwa?

Mashirika ya uma yanakufa kwa sababu mbili kuu. Mosi, serikali haipaswi kufanya biashara maana cha wote hakina mwenyewe (lack of ownership). Pili hakuna ile kujituma kupata faida sana kwa maana ruzuku itatutoa tukikwama au hakuna mshindani.

TANESCO haina mshindani toka sekta binafsi mbona iko hoi miaka yote kukimbilia kupandisha bei bila ya kuboresha huduma? Kutwa kucha inaliwa kila kona. Why? Cha wote hakina mwenyewe na hata iliwe vp kuna ruzuku kufidia hasara.

Tusipende kulaumu sekta binafsi wakati upuuzi unaondelea serikalini kuna mazuzu kazi kusifia tu. Mashangingi. Ndege. N.k.

Serikali kazi yake iweke mazingira wezeshi na sawa kwa sekta binafisi kushindana. Hapo sisi walaji ni full bata kuanzia ubora viwango bei upatikanaji uhakika thamani n.k.
 
Umeambiwa ndege ilisubiri board members. Na bado unaongea habari ya majet wind? Au ndo kutetea kila kitu? Hapa ni wazalendo wanalilia shirika linavyo endeshwa kizembe wakati serikali ina nia nzuri ya kulifufua. Bila kubadirisha aina ya watendaji walio na mawazo ya kizamani, hili shirika litarudi kulekule. Kumbukeni hata JK aliapoingia madarakani alikuwa na nia ya kulifufua kwa kiasi fulani. Nakumbuka aliweka mkurgenzi mpya akaingia kwa mbwembwe nyingi. Na mtaji wakapewa over 4b. Waliishia takukuru. Yasije yakajirudia sasa. Serikali iwapime ATCL kila baada ya miezi mitatu ili kama kuna harufu ya uozo urekebishwe haraka na asiangaliwe mtu usoni. Hapa kazi tu.
Wazalendo tunasema hakuna sababu kununua midege kwa taslimu wakati kuna ya msingi kufanya. Shirika lifutwe tu au mtaji utaobaki baada ya madeni wawekeze precision.

Serikali hina haja kufanya biashara ya usafiri. Ni upuuzi tu huo. Wajifunze toka mataifa menginewe. Walioendelea (na pengine ndo maana wameendelea) hawana hayo mashirika. Swissair waliuza lao kitambo.

Wanaojikongoja wanang'ang'ania ufahari kuwa na ndege na kushindia hasara. Kenya SA Rwanda Misri n.k. wote hasara.

Na Magu badala hata ya kwenda kujifunza Ethiopia, anaenda kwa walioshindwa. Tangu waanze Rwandair hawajawahi kupata faida. It's time before hawajafunga virago na wataanza ATCL then Rwandair.

Kinachowashinda kuwekeza kwa Precision ni nini? Au hata Fastjet.
 
Bila IT na Marketing kushirikiana na kuweka mfumo friendly and Transparent,wapigaji wataendelea kupiga milele.
Zote hizo ni sawa na kufunga Ac chumbani ili utumie blanketi kama kwenye bongomuvi. Kisha unaanza kutafuta dobi mzuri kufua mablanketi na fundi mzuri kuhudumia Ac.

Hasara inaanziaga kwenye wazo halafu inatengeneza mfumo wa domino kwenye utendaji.
 
Tatizo la atcl kama huna ujuzi kwenye airline industry uwezi and kujuwa Walsh and kuliongelea watu wengi wanaongea kisiasa , kiutendaji serikali inatakiwa kuhakikisha shirika hilo hilo linasaidiwa kwa mambo mengi sana,
1,serikali lazma lianzishe handling company kunusuru matumizi ya kulipia handling Au kuhudumia abiria Na mizigo kwa mfano ndege ikituwa mwanza kwa trip wanalipia zaidi ya laki nne je ikituwa viwanja vitatu watalipa kiasi gabi,
2, nasema siasa maana airline ni Industry kama unavoona madaktari sasa kuchukuwa watu ambao sio wajuzib bila ya elimu ya airline au uzoefu ni kuliuwa shirika shule muhimu sana
Hapa kwetu baada ya kuliuza shirika hilo mpaka eliminates the ya mambo ya airline yalikufa leo hata kufanya loadsheet unahitaji and kwenda kusomea nje ya nchi
Hivo msione ndege zinaruka zina mambo mengi sana
Hakuna kudharau kuna watu wanaona Ni biashara rahisi sana
Wasitumie nguvu. Wawekeze kwenye anaeweza au waachane na kuendesha biashara ya ndege.

Kama ni kukuza utalii, nchi zenye utalii mkubwa sana wala serikali zao haziendeshi mashirika ya biashara ya ndege. Marekani, Ufaransa, ujerumani, n.k. Tuige walio mbele. Sio makapuku wenzetu.

Kuna shida kubwa sana kwenye mfumo wa mawazo wa wanaowashauri watawala. Wanawazia zama za ujima bado. Mara kulazmisha watu kupanda ndege na upuuzi mwingine mwingi tu.
 
Marketing department ifanyiwe kazi ikiwezekana ifumuliwe,kusiwepo na ufanyaji wa kazi kwa mazoea.
Guys... spare your efforts. Hakuna sababu ya msingi serikali kuwa na hilo shirika. Iwe usalama, utalii, n.k isipokua tu labda ufahari. Na hatujitaji ufahari kwa sasa
 
Mwanzo mgumu, ATCL irekebishe hizo kasoro na itoe huduma za kisasa zaidi na kwa haraka ,wajitahidi kwenda muda wasiwaweke abiria sehemu kwa muda mrefu, Tanzanis tunahitaji shirika la ndege kwa gharama yeyote, hatutaweza kufika kama tutakuwa tunaanzisha kitu maramoja, tunakumbana na challenges tunakimbia ,au tunalalamika, we need to face the challenges not to run from the challenges. Tunahitaji ndege nyingi zaidi ziingie ,kwa nini tuogope bhana kuendesha shirika la ndege just running kuna ugumu gani,nchi zingine zimeweza kwa nini Tanzania mshindwe?
Taja sababu walau tatu tu za kwanini ni lazima kuwa na shirika la kibiashara la ndege linaloendeshwa na serikali
 
Haha..Hawa watu wanaumia sana precisionair kuruka kwa mafanikio. Wameiga sana vita kwa kila namna, sasa wameamua kabisa kununua ndege kwa akili zao. Shida ni ktk ajira, niliwaambia watu, kubagua kanda yenye mafanikio ni kujiumiza. Tatizo jingine ni utawala uliopo ndio kabisa,una hofu na kanda ya kaskazini, kila angle wanaogopa kivuli cha hawa jamaa. Ktk siasa wanaogopa watahujumiwa, ktk Ndege wanaogopa watahujumiwa eti precisionair itapewa chapuo, ktk mawasiliano hivyo hivyo.Mwisho wa siku ni kuweka watu wanaofanya maigizo kila angle. Hii nchi ipo siku itakabidhiwa kwa wachapa kazi kiroho safi, wabaguzi watakuwa chalii wenyewe.
Japo umeiweka kiukabila ila nakuunga mkono kuna kihoro kikubwa kwa serikali kuipa flag Precision. Na kiko so unfounded. Sana sana na hearsays.

Kama ndivyo, watuokolee hasara (kupoteza kodi zetu kwa mishahara iso tija na ruzuku zisoisha) wafunge hiyo biashara na kupea private sector uwanja huru watoane jasho. Kwetu itakua faida tu.
 
yani watu wanavyolalamika mpaka naogopa kupanda, nimebook hii ndege lakini nilipoomba kucancel route nikaambiwa nitakatwa elf 50 kwa kichwa kwa route, nilibaki kama nimepigwa shot ya umeme
 
Ndugu zanguni ndege hazitaki mchezo...
Ni afadhali tusiwepo na shirika la aina hiyo kuliko yatokee kama ya ADAM AIR.
Ni busara watu wa NTSB waanze kufanya pre investigation ...kabla ya jambo litarajiwalo...Mungu aepushie mbali.
 
yani watu wanavyolalamika mpaka naogopa kupanda, nimebook hii ndege lakini nilipoomba kucancel route nikaambiwa nitakatwa elf 50 kwa kichwa kwa route, nilibaki kama nimepigwa shot ya umeme
Mkuu we si ulitaka Kwenda FastJet au Precision Air? Ndio wanaiandaa kuwa Monopoly polepole...
 
Mamilioni ya dola yamepotea kisiasa.
Magu ana vita na raia wake anataka maisha yao yawe magumu hapohapo anataka tumuungishe kwenye ndege zake, never.
Huweza kuwa na ugomvi na wateja halafu unategemea faida.
 
dah mi hiyo pesa ya ndege wangeipeleka kwa reli naona tungepata faida mara dufu tofaut na hy ndege maana hatuna hata kipato cha kupanda hzo ndege bali tungewachia sekta binafsi kujihusisha huko tu..sisi mwend wa kodi tuu
Reli nayo sio mchezo Mkuu; inatakiwa kujipanga hasa. Hiyo hela iliyonunulia ndege sijui hata kama ingetosha standard gauge ya reli kutoka Kituo cha Station - Dar hadi Pugu.
 
Back
Top Bottom