Makamba usikubali kuchezewa wala kudanganywa na hao wahandisi wa JNHPP. Tani 26 si nzito kama wanavyokudanganya

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Hawa wahandisi wa mradi wa JNHPP wanamdanganya sana huyu waziri January Makamba kwa sababu yeye mambo ya sayansi ni mashikolo mageni. Eti tani 26 ni uzito mkubwa sana unaohitaji a special immobile crane kuunyanyua!

Mhuuuuu! Kweli? Kwa nini hawa wahandisi wanamfanyia hivyo Makamba? Mbona tani 26 au zaidi ndizo tunazoziona zimebebwa na malori ya semi trailer manarabarani mwetu. Mbona hayo mamia ya makontena yanayoshushwa na kupandishwa kila siku kwenye meli katika bandari zetu yanazidi hizo tani 26?

Nini hasa tatizo? Kwa nini wasikodi moja ya cranes zilizoko kwenye bandari zetu ili bwawa la JNHPP lianze kujazwa maji katika msimu huu wa mvua kama ilivyokuwa imepangwa? Makamba usikubali kuchezewa na hao wahandisi. Wananchi hawatakuelewa. Hizo kazi ili ziendelee zinahitaji ukali na si diplomasia.

Tusipojaza maji bwawa hilo msimu huu wa mvua ina maana itabidi tusubiri hadi msimu wa mwaka 2023/24 kujaza bwawa hilo. Maana yake hadi 2025 hatutakuwa na umeme wa JNHPP ambao ungalishusha bei ya unit moja ya umeme kutoka sh 350/ hadi sh 30/ kama ilivyo kwenye nchi zilizoendelea kama China na Ulaya.

Viwanda vyetu vingaliweza kuzalisha bidhaa zenye bei inayoweza kushindana kwenye masoko ya kimataifa. Hili kama halitafanikiwa tutegemee umeme kupanda bei maradufu, kukatika mara kwa mara na mgawo wa umeme na maji kama ilivyokuwa enzi zile za Richmond. Hili litaufanya ushindi kwenye uchaguzi mkuu kuwa ngumu sana kwa chama chenu.
 
Kipindi cha ukali kimeshapita mkuu

Hiki ni kipindi cha round-table and dialogue consensus

Ukali ulituchelewesha sana
 
Alipiga yeye peke yake, sasa ni zamu ya wengine kupiga. Wahandisi wameamua wasiondoke hivi hivi
 
Kipindi cha ukali kimeshapita mkuu

Hiki ni kipindi cha round-table and dialogue consensus

Ukali ulituchelewesha sana
Round-table na dialogue consensus ufanye na wahandisi wawongo, wabadhirifu na wapiga dili?

Kinachotakiwa ni system madhubuti ya kuwabaini wabadhirifu hawa wa mali na miradi ya umma pamoja na wazembe. Baada ya hapo ni kuwachukulia hatua kali ili liwe fundisho kwa wengine. Kalumekenge staili ndiyo suluhisho kwa wabongo. Ukicheka na nyani utaambulia mabua.

Hayo mambo ya round- table na dialogue consensus awaachie akina Mulamula. Yeye Makamba avae over roll la kihandisi na awe mkali anapokagua na kusimamia miradi hiyo. Anatakiwa kuwa na back information kutoka TISS na wahandisi wake walioko pale wizarani.
 
Yawezekana walimuona analeta ujuaji wakamwingiza Chaka.Au aliwaambia watafute namuna ya kuhalalisha kukodisha ili wapige.

Waziri hatakiwi kuwa na chanzo kimoja tu Cha information,na siyo kuongea kila Mara utafikiri msemaji wa Serikali.

Ona kwa muda mfupi karopoka kweli.

Alitangaza miezi 2 umeme ukikatika atatumbua.....

Mara tena umeme ulikuwa haukatiki sababu watu waliogopa kutumbuliwa.

Mara miundo mbinu imechakaa,amesahau enzi za Msoga gang ndo zilikuwa nyimbo zao hizi Mara maji,Mara miundo mbinu mibovu.
Mara Lile Beans mkataba sijui uko nyuma sijui siku 400.

Mara kuchelewa kukamilika mradi si tatizo,huyu ni waziri kweli?

Anachotakiwa January ajue kwamba yeye Hana uwezo kabisa wa kiongozi ila kabebwa na jina la baba yake tu.
 
Akina Shibuda sasa wanachekelea kwa anachokifanya Makamba. Udenda umeanza kuwatoka kuelekea 2025 kwani Makamba anawatengenezea njia bila yeye kujua! Mama inabidi iwastukie watu hawa kabla mambo hayajavurugika kabisa. Umeme ndiyo uchumi na mambo yote kwenye nchi yanategemea umeme.

Sasa hivi maeneo mengi nchini hayapati umeme hadi usiku kwa kisingizio cha ukarabati wa grid ya taifa. Kwa nini ukarabati huo usifanyike usiku muda ambao hakuna uzalishaji wa kiuchumi? Ujenzi wa miundo mbinu hususani SGR, JNHPP na shughuli nyingi za kiuchumi hufanyika mchana na siyo usiku. Hawa jamaa mchana tangia saa mbili asubuhi hadi saa 12 jioni wanakata umeme na kuurudisha usiku. Kama si sabotage tuiiteje?
 
Kwanza hilo crane lenyewe liko wapi? Linafika lini?
Mkuu habari ya crane wala usiiamini, mradi huu huu zinaletwa transformer za tani karibia 80 au mia kwa kutoka dar zinakuja na lory mpaka mzenga zikipakiwa kwenye treni kuelekea huko kwenye bwawa. sasa jiulize hiyo crane wanayosema haipo je hiyo inayobeba hizo transfomer ni crane kutoka mbinguni??
Mimi nimeiona hiyo crane kwa zaidi ya miezi mitatu ikiwa imepaki pale mzenga jirani na reli na kituo cha polisi, tena hiyo crane ni ya tani mia moja wala si kama crane hazipo.
 
Back
Top Bottom