Akihojiwa na bbc swahili, January makamba amesema na wao(ccm) wa nashangaa ZEC kufuta uchaguzi japo walikuwa wanaongoza ingawa kwa ushindi mwembamba.
Makamba anapaswa kuona aibu kwa matamshi haya, Ina maana ccm haifaham kinachoendelea ZEC?
Makamba, mungu apendi dhuruma. Acheni janjajanja isiyo na msingi.
Habari wakuu,
Leo mapema kidogo, January Makamba ambae ameongea kwa niaba ya chama cha mapinduzi. Ameongea na waandishi wa habari na kuongelea mambo kadhaa ikiwemo vurugu au fujo.
Makamba: Kujaribu kuwahamasisha vijana waingie mtaani, wafanye vurugu, wafanye fujo haikubaliki hata kidogo, taifa letu sisi ni zaidi ya hitaji la madaraka la mtu mmoja mmoja, amani ya nchi yetu ina thamani kubwa sana.
Wenzetu wa UKAWA wana haki ya kulalamika wanavyotaka usiku na mchana lakini hawana haki ya kuliingiza taifa hili katika machafuko kwa kuwahimiza vijana, kuwapanga vijana, kuweka mipango watu waingie barabarani, waandamane, wafanye vurugu, waharibu mali za watu, wasimamishe shughuli za watu wengine kama nchi hatuwezi kukubali hili jambo.
Tunawaomba watanzania waendelee na shughuli zao kama kawaida na huku kila mmoja akitambua wajibu wake wa kulinda amani wa nchi yetu.
Mwisho kuna hili suala la kuahirisha uchaguzi wa Zanzibar tumelipata hivi karibuni, sisi sio wasemaji wa tume, tume ya uchaguzi wa Zanzibar itatoa kauli yenyewe kuhusu sababu zilizopelekea uchaguzi huu ukasimamishwa ambacho tunafahamu sisi ni mambo mawili.
Kwanza mamlaka ya kisheria ya kuahirisha, kusimamisha au kufuta matokeo ya uchaguzi wanayo tume ya uchaguzi ya Zanzibar wanayo mamlaka hayo kisheria na sababu za kufanya hivyo wanaweza kuzitoa wenyewe.
Pili kuahirisha uchaguzi Zanzibar hakuna mahusiano yoyote na uchaguzi wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, chaguzi hizi zinaendeshwa na tume mbili tofauti, matokeo ya Urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa upande wa Zanzibar ni matokeo halali kwa sababu yameendeshwa katika utaratibu na tume tofauti.
youtube video