Makaidi ajitolea kunusuru 'ndoa' ya Zitto, CHADEMA

Makaidi ajitolea kunusuru 'ndoa' ya Zitto, CHADEMA

ZZK matatizo boy,kafulila alipokosana na chama chake na kutaka kuvuliwa uanachama aliomba na kukiri makosa yake na wala alikuwa afichi kama aliomba sana na kulia asifukuzwe ila sasa huyu machinooo duh!ndiyo maana nasema zitto ni mzuri lakini si lazima kuungana nae kwenye haya mapambano
 
huyu ndugu anyetaka kupatanishwa na chadema iloi ajiunge na ukawa ni huyohuyo aliyewatukana ukawa na kuwaia wasalka tonge
 
Katika ukurasa wa kwanza wa gazeti la Mwananchi la leo,kuna habari isemayo "Makaidi ajitolea kunusuru ndoa ya Zitto,CHADEMA". Kwenye habari hiyo inayoandikwa katika kurasa za 1 na 4, Mwenyekiti huyo mwenza wa UKAWA na NLD Emmanuel Makaidi amekaririwa akidai kuwa Zitto alimuomba kumpatanisha na Mwenyekiti wa CHADEMA,Freeman Mbowe. Makaidi amedai kuwa sasa yu tayari kuanza kazi aliyoombwa na Zitto kwakuwa Mbowe anaingilika na ni mtu makini,safi na muungwana.

Lakini,Zitto alipoulizwa kuhuu hilo alikana na kusema kuwa kama kuna haja ya kufanya hivyo atakaa na Mbowe na kuyamaliza. Pia Zitto amesema kuwa asilazimiswe kuingia UKAWA kwa njia ya CHADEMA tu kwakuwa aweza kuingia UKAWA kupitia CUF,NCCR-Mageuzi au ACT-Tanzania. Alisema "Huyu mzee ni mtu ninayemheshimu sana na juhudi zake ni nzuri,lakini sijawahi kuzungumza naye kuhusu kupatanishwa na chama changu,sisi wenyewe tuna uwezo kukaa wawili na kuyamaliza,jitihada zake kwasasa hazijahitajika"

Baada ya kukana kumuomba Makaidi, Makaidi amesema " amekana huyu Bwana,haa! Tulikutana pale kantini Bungeni,aweza kukutajia namashhidiwaliokuwapo,laini mimi nilikuwa nafuatilia jinsi ykumuingia huyoBwana mkubwa wa CHADEMA na sasa naona inawezekana."

Lengo ni zuri. Lakini mkweli ni nani?
=======================

Kakodiwa na mengi kuwapatanisha upeo wa makaidi ni sifuri
 
zito yuko sahihi kukataa hata kama kweli alimwomba mzee makaidi kwa nini aende kwenye community media kuyasema hayo? maana siasa mnazijua wandugu ukijifanya mnyonge na ukapiga magoti ni lazima wabaya wako wakuzomee sana ko hata ningekuwa mimi nisingekuwa tayari kukubaliana na hilo
 
...Nimekerwa na neno NDOA.,kumbe mtu akijiunga na chama inakuwa ndoa.
Nasubiri Southampton vs Manchester United leo saa tano usiku.
 
Kama Zitto na Mbowe wana mambo binafsi wanayotaka kusuluhisha, hayatuhusu. Lakini kama ni mambo ya chama yatamalizwa kichama. CDM si mali ya Mbowe.
Gazeti la Mwananchi wamefanya spinning hiyo makusudi...ili kuuaminisha umma kuwa Chadema ni mali ya Mbowe, jambo ambalo si kweli. Na kama Zitto katamka kuwa 'atakutana na Mbowe wayamalize' (kwamba Mwananchi hawakumlisha maneno Zitto), basi Zitto anahusika moja kwa moja kwenye hujuma hii dhidi ya Chadema.
 
Gazeti la Mwananchi wamefanya spinning hiyo makusudi...ili kuuaminisha umma kuwa Chadema ni mali ya Mbowe, jambo ambalo si kweli. Na kama Zitto katamka kuwa 'atakutana na Mbowe wayamalize' (kwamba Mwananchi hawakumlisha maneno Zitto), basi Zitto anahusika moja kwa moja kwenye hujuma hii dhidi ya Chadema.
Swahiba wa Zitto Msaki bado yuko Mwananchi?
 
...Nimekerwa na neno NDOA.,kumbe mtu akijiunga na chama inakuwa ndoa.
Nasubiri Southampton vs Manchester United leo saa tano usiku.
Wamebadili muda. Ni saa 2:45 usiku, usije subiri saa tano ukakuta ngoma imekwisha.
 
zito yuko sahihi kukataa hata kama kweli alimwomba mzee makaidi kwa nini aende kwenye community media kuyasema hayo? maana siasa mnazijua wandugu ukijifanya mnyonge na ukapiga magoti ni lazima wabaya wako wakuzomee sana ko hata ningekuwa mimi nisingekuwa tayari kukubaliana na hilo
Haiepukiki. Hili la Zitto Mbowe hana mamlaka nalo peke yake. Litaamuliwa kichama, hivyo haliwezi kufanywa siri.
 
CHADEMA SIO MBOWE, amekihujumu chama sio MBOWE hata iweje ZZK hatumtaki CDM. Kama wanapatanishwa ni kwenye dili zao zingine kama zipo sio kuhusu CDM

Umemaliza kila kitu kiongozi! Cdm hatuhitaji vigeugeu na wanafiki kama huyo bwana mdogo.akafie mbele huko!
 
Akili chache lakini inahekima na busara..
Akili nyingi lakini haina hekima na busara..zito utapotea usifikir upepo wa escrow utakuvumisha kama zamani..
 
Na bado najiuliza ivi mwananchi mnagenda ipi na zito kabwe
 
mwanzoni nilikuwa namkubali sana lakini kumbe ni mnafiki mkubwa kibaraka wa ccm
 
Back
Top Bottom