Watanzaina na pia afrika nzima tumeendekeza sana uchawi. Mbona wenzetu huku ulaya wanjenga magorofa kila siku lakini husikii mambo kama hayo. Na ikitokea ajali kwenye ujenzi wataandika kwenye kila gazeti. Inabidi tuelimike sasa. Uchawi umeletwa kwa kuharibu na wala si kujenga au kufanikiwa
Watanzaina na pia afrika nzima tumeendekeza sana uchawi. Mbona wenzetu huku ulaya wanjenga magorofa kila siku lakini husikii mambo kama hayo. Na ikitokea ajali kwenye ujenzi wataandika kwenye kila gazeti. Inabidi tuelimike sasa. Uchawi umeletwa kwa kuharibu na wala si kujenga au kufanikiwa
ni jambo la kificho mno, lisilojulikana na wengine wengi lakini ukweli ni kwamba magorofa mengi uyaonayo yana roho za watu au imevunja mifupa ya watu kwa njia za ajali au yamekunywa damu ya kikafara
si mara zote wafanyao mambo haya ni wamiliki la hasha bali mambo haya hufanywa pia na wakandarasi na hata waliopewa tenda mbali mbali kwenye site husika... Nia na lengo ni moja tuu kupata zaidi au kujikinga kishirikina
kama tungekuwa na takwimu za kitaifa si ajabu kati ya kila magorofa kumi saba yamesababisha maafa vilema na makovu... Hili jambo lina level zake kuanzia kutoa kafara dogo la mtu mmoja mpaka ibada za makafara zifanywazo na makandarasi wakubwa kufikia viwango vya freemason
ndio maana kwenye ujenzi wa mahekalu makubwa ya ibada hufanyika ibada maalum za kumwomba mungu aepushe mbali mabaya yote kwenye ujenzi husika mpaka mwisho wa ujenzi wake.
Hata wewe kwa kutambua hili fanya hivyo kwenye ujenzi wako hata kama si ghorofa ili nyumba yako isije kuwa ni chanzo cha mabalaa na mitihani ya dunia
nimekupata mkuu Mshana wajinga wamefukia kuku shambani kwangu eti wanataka nisiwe na. mawazo na shamba langu kabisa,aliyefukia ni yule ambaye nimenunua shamba kutoka kwake
Mimi yalinikuta hayo nilinunua site nilijenga fasta baada ya miezi 3 nikahamia, yaliyonikuta Mungu ndo anaejua. Kiukweli Nyumbani imenishinda nimeiacha ni majanga mpk Leo sijakaa Sawa.
mkuu mshana Jr kafara ya kufukia kuku ina uzito kiasi gani, naomba nipe maarifa hapa, yaan mtu kafukia kuku mahali kama zindiko vile
hakuna kitu kama hicho , ni imani yenu tu, hutegemea malezi yako, jamiii uliokulia na kulelewa, elimu, mazingira unamoishi , imani potofu sana hizo
Mkuu moghaka mambo haya yapo aisee kuna watu wanabukua yaan unalima wewe halafu yeye anavuna kimiujiza kabisa, mkuu tembea uone, jirani yangu aliwahi kumkuta mwanamke anaoga shambani kwake mchana kweupe katikati ya shamba
mwacheni huyo anasema ni imani tu.siku akijikuta kalazwa chooni na yupo uchi atarudi kuomba msaada.
Kuna watu hii brainwashing ya mzungu imewaathiri sana
sasa mshana ni jinsi gani ya kuzuia watu wanao bukua maana ni jambo lililokubuhu kabisa yaan wewe unalima halafu mtu anavuna kimazingara sometimes hata kama ni mahindi umeanika anaiba tu kiuchawi
Dawa yake ni nini hapo mkuu mshana kama una elimu nayo