Makadirio TRA foleni inatisha!

BOB LUSE

JF-Expert Member
Jan 25, 2014
3,585
2,893
Kuna Tatizo la Watanzania kufikiri na kufanya Maamuzi magumu yenye manufaa. Makadirio Kwa makampuni wanaruhusiwa kujikadiria kupitia kwenye mfumo bila Tatizo, japo nao mtandao wakati Mwingine ni tatizo.

Shida ipo Kwa Watu binafsi na walipa Kodi ambao hawajasajili makampuni tunazuiwa kufanya makadirio kwenye mfumo (online filing). Jambo hili lingeokoa muda wa mteja kukalia viti vya Serikali masaa matano mpaka SITA. Nchi zingine hata Majirani zetu, huhitaji kufuata huu urasimu.

Mazingira ya kuja kukadiriwa ana Kwa ana pia yanatoa nafasi ya kupokea rushwa Kwa Maafisa wa TRA kwakuwa wanapewa Mamlaka ya kuamua anachokiona kinafaa. Ushauri, Biashara zinafahamika, waweke viwango vya Kodi Kwa Biashara ndogo na pia kuwe na maswali kwenye mfumo ambayo mteja akijaza, mfumo ufanye makadirio ya Haki bila mtu kuja kupanga foleni maofisini.

Nipo Gongo la Mboto ofisi za TRA, kuna watu wamesimama, ofisi Zina feni kwaajili ya Wafanyakazi, Wateja wanajipepea kupata hewa nzuri na kupunguza joto, wateja wamesimama wengine mpaka nje. Mazingira sio rafiki, Maofisa wenyewe wa kukadiria Wana watu wengi, hata ukija, hujui utakaa muda gani. Teknolojia zifanye maisha yetu kuwa rahisi. Kuliko Hali ilivyo.

Sio jambo zuri kuacha kazi kuja kukaa bila kufanya kitu Kwa masaa.

Mungu Ibariki Tanzania, Tupe Akili na Hekima Kwa manufaa ya Taifa.
 
Pia Maofisa Wakienda kula ni saa nzima lazima iishe ndio anarudi kuja kuendelea na kazi, situation ya sio nzuri. Nafuu wangechukua Zoezi hili kama operation, dk 15 zinatosha kula na kuendelea na kazi ukifikiria wateja unaowahudumia, japo nao wanachoka, Naamini wanatumia muda huo ku break.
 
Kuna Tatizo la Watanzania kufikiri na kufanya Maamuzi magumu yenye manufaa. Makadirio Kwa makampuni wanaruhusiwa kujikadiria kupitia kwenye mfumo bila Tatizo, japo nao mtandao wakati Mwingine ni tatizo.

Shida ipo Kwa Watu binafsi na walipa Kodi ambao hawajasajili makampuni tunazuiwa kufanya makadirio kwenye mfumo ( online filing). Jambo hili lingeokoa muda wa mteja kukalia viti vya Serikali masaa matano mpaka SITA. Nchi zingine hata Majirani zetu, huhitaji kufuata huu urasimu.

Mazingira ya kuja kukadiriwa ana Kwa ana pia yanatoa nafasi ya kupokea rushwa Kwa Maafisa wa TRA kwakuwa wanapewa Mamlaka ya kuamua anachokiona kinafaa. Ushauri, Biashara zinafahamika, waweke viwango vya Kodi Kwa Biashara ndogo na pia kuwe na maswali kwenye mfumo ambayo mteja akijaza, mfumo ufanye makadirio ya Haki bila mtu kuja kupanga foleni maofisini.

Nipo Gongo la Mboto ofisi za TRA, Kuna watu wamesimama, ofisi Zina feni kwaajili ya Wafanyakazi, Wateja wanajipepea kupata hewa nzuri na kupunguza joto, wateja wamesimama wengine mpaka nje. Mazingira sio rafiki, Maofisa wenyewe wa kukadiria Wana watu wengi, hata ukija, hujui utakaa muda Gani. Teknolojia zifanye maisha yetu kuwa rahisi. Kuliko Hali ilivyo.

Sio jambo zuri kuacha kazi kuja kukaa bila kufanya kitu Kwa masaa.

Mungu Ibariki Tanzania, Tupe Akili na Hekima Kwa manufaa ya Taifa.
Nadhani shida ni sisi pia Watanzania huwa tunakasumba ya kupenda kusubiri dakika za majeruhi. Mimi huwa naenda kukadiriwa tokea mwezi wa kwanza sisubiri dakika za majeruhi ndiyo maana sikutani na foleni wala nini nafanyiwa taratibu makadirio. Nakumbuka hata zoezi la kusajili line za simu lilikuwa hivi hivi dakika za mwisho watu walilalamikia foleni sababu ya kwenda muda au dakika za mwisho. Shida hata mtandao nao ungezidiwa maana kasumba yetu Wabongo ni dakika za mwisho. Shida siyo mfumo uwepo wala ni kufika ofisini nachokiona ni watu kusubiri dakika za mwisho. Unadhani hata mfumo ukiwepo kama kila mtu kwa muda huo akiwa anatumia utakuwa na nguvu kweli? Pili siyo kila mtu anajua kusoma na kuandika mpaka useme mtu ajikadirie, sisi biashara tunapishana wengine hata hesabu kuziweka vizuri hajui ndiyo iwe kujikadiria? Hao wanaojikadiria utakuta wana watu wamewaajiri na wanawalipa pesa nyingi ndiyo maana hata biashara zao unaona ni kampuni. Mimi na wewe tutao uwezo wa kuajiri watu wa kutengeneza sijui wanaita kufaili.
 
Sasa kama hujasajiliwa na VAT (sio lazima kampuni) utajikadiria vipi wakati presumptive tax payers hawawajibiki kuandaa mahesabu?

Maana yale mahesabu ndio yanatoa ukweli wa kodi inayotakiwa kulipwa. Otherwise lazima uende uhojiwe location ya biashara, wacheki EFD, waangalie na aina ya biashara, kisha Officer ataona akupige vipi...

Yaani ujikadirie laki moja kwa biashara ya kulipa milioni 3?
 
Nipo Gongo la Mboto ofisi za TRA, kuna watu wamesimama, ofisi Zina feni kwaajili ya Wafanyakazi, Wateja wanajipepea kupata hewa nzuri na kupunguza joto, wateja wamesimama wengine mpaka nje. Mazingira sio rafiki, Maofisa wenyewe wa kukadiria Wana watu wengi, hata ukija, hujui utakaa muda gani. Teknolojia zifanye maisha yetu kuwa rahisi. Kuliko Hali ilivyo.
Pia ingepunguza sana urasmi, uMungu mtu etc, ni simple application ambayo unaverify mauzo yako kwa kipindi fulani na iwe unaweza kureview kila baada ya robo ya mwaka ili kuweka uhalisia kuliko hivi sasa ambapo rushwa ndo ina determine kiasi cha kodi mfanya biashara anatakiwa kulipa!!
 
Pia ingepunguza sana urasmi, uMungu mtu etc, ni simple application ambayo unaverify mauzo yako kwa kipindi fulani na iwe unaweza kureview kila baada ya robo ya mwaka ili kuweka uhalisia kuliko hivi sasa ambapo rushwa ndo ina determine kiasi cha kodi mfanya biashara anatakiwa kulipa!!
Wabongo hata ufanye nini hatuwezi , mfano mdogo tu ATM imewekwa mtu atoe pesa kwa haraka na urahisi lakini unakuta mtu anapambana na kadi nne atoe milioni 4.Badala ya kwenda ndani kutoa pesa na kupisha wengine. sasa turudi humu ni kwamba mfumo upo kwa mujibu wa wale wanaotengeneza hesabu sababu wanahitaji kuandaa sasa wewe unakuta unabiashara kwa siku unaingiza 30,000 au chini ya hapo na hesabu pengin ni ngumu kutengeneza unataka usipate msaada wa kufanyiwa kazi bure
 
Kuna Tatizo la Watanzania kufikiri na kufanya Maamuzi magumu yenye manufaa. Makadirio Kwa makampuni wanaruhusiwa kujikadiria kupitia kwenye mfumo bila Tatizo, japo nao mtandao wakati Mwingine ni tatizo.

Shida ipo Kwa Watu binafsi na walipa Kodi ambao hawajasajili makampuni tunazuiwa kufanya makadirio kwenye mfumo (online filing). Jambo hili lingeokoa muda wa mteja kukalia viti vya Serikali masaa matano mpaka SITA. Nchi zingine hata Majirani zetu, huhitaji kufuata huu urasimu.

Mazingira ya kuja kukadiriwa ana Kwa ana pia yanatoa nafasi ya kupokea rushwa Kwa Maafisa wa TRA kwakuwa wanapewa Mamlaka ya kuamua anachokiona kinafaa. Ushauri, Biashara zinafahamika, waweke viwango vya Kodi Kwa Biashara ndogo na pia kuwe na maswali kwenye mfumo ambayo mteja akijaza, mfumo ufanye makadirio ya Haki bila mtu kuja kupanga foleni maofisini.

Nipo Gongo la Mboto ofisi za TRA, kuna watu wamesimama, ofisi Zina feni kwaajili ya Wafanyakazi, Wateja wanajipepea kupata hewa nzuri na kupunguza joto, wateja wamesimama wengine mpaka nje. Mazingira sio rafiki, Maofisa wenyewe wa kukadiria Wana watu wengi, hata ukija, hujui utakaa muda gani. Teknolojia zifanye maisha yetu kuwa rahisi. Kuliko Hali ilivyo.

Sio jambo zuri kuacha kazi kuja kukaa bila kufanya kitu Kwa masaa.

Mungu Ibariki Tanzania, Tupe Akili na Hekima Kwa manufaa ya Taifa.
Kwa nini msiajiriwe?
 
Kuna Tatizo la Watanzania kufikiri na kufanya Maamuzi magumu yenye manufaa. Makadirio Kwa makampuni wanaruhusiwa kujikadiria kupitia kwenye mfumo bila Tatizo, japo nao mtandao wakati Mwingine ni tatizo.

Shida ipo Kwa Watu binafsi na walipa Kodi ambao hawajasajili makampuni tunazuiwa kufanya makadirio kwenye mfumo (online filing). Jambo hili lingeokoa muda wa mteja kukalia viti vya Serikali masaa matano mpaka SITA. Nchi zingine hata Majirani zetu, huhitaji kufuata huu urasimu.

Mazingira ya kuja kukadiriwa ana Kwa ana pia yanatoa nafasi ya kupokea rushwa Kwa Maafisa wa TRA kwakuwa wanapewa Mamlaka ya kuamua anachokiona kinafaa. Ushauri, Biashara zinafahamika, waweke viwango vya Kodi Kwa Biashara ndogo na pia kuwe na maswali kwenye mfumo ambayo mteja akijaza, mfumo ufanye makadirio ya Haki bila mtu kuja kupanga foleni maofisini.

Nipo Gongo la Mboto ofisi za TRA, kuna watu wamesimama, ofisi Zina feni kwaajili ya Wafanyakazi, Wateja wanajipepea kupata hewa nzuri na kupunguza joto, wateja wamesimama wengine mpaka nje. Mazingira sio rafiki, Maofisa wenyewe wa kukadiria Wana watu wengi, hata ukija, hujui utakaa muda gani. Teknolojia zifanye maisha yetu kuwa rahisi. Kuliko Hali ilivyo.

Sio jambo zuri kuacha kazi kuja kukaa bila kufanya kitu Kwa masaa.

Mungu Ibariki Tanzania, Tupe Akili na Hekima Kwa manufaa ya Taifa.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inapenda kuwataarifu wafanyabiashara wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa katika kipindi hiki cha makadirio ya kodi ya mapato imesogeza Huduma ya makadirio na kupewa namba ya Malipo (control Number) katika vituo vyake vya Huduma kama ifuatavyo

Ilala : Kitunda karibu na kituo cha Polisi, Majohe Kichangani na Viwege

Tegeta : Mbezi Bichi kwa Zena mkabala na KFC, Bunju B na Goba mkabala na Simba oil

Kariakoo : Tandamti/Nyamwezi na Kipata/Congo

Wafanyabiashara wanaombwa kutembelea maeneo hayo.
 
Kuna Tatizo la Watanzania kufikiri na kufanya Maamuzi magumu yenye manufaa. Makadirio Kwa makampuni wanaruhusiwa kujikadiria kupitia kwenye mfumo bila Tatizo, japo nao mtandao wakati Mwingine ni tatizo.

Shida ipo Kwa Watu binafsi na walipa Kodi ambao hawajasajili makampuni tunazuiwa kufanya makadirio kwenye mfumo (online filing). Jambo hili lingeokoa muda wa mteja kukalia viti vya Serikali masaa matano mpaka SITA. Nchi zingine hata Majirani zetu, huhitaji kufuata huu urasimu.

Mazingira ya kuja kukadiriwa ana Kwa ana pia yanatoa nafasi ya kupokea rushwa Kwa Maafisa wa TRA kwakuwa wanapewa Mamlaka ya kuamua anachokiona kinafaa. Ushauri, Biashara zinafahamika, waweke viwango vya Kodi Kwa Biashara ndogo na pia kuwe na maswali kwenye mfumo ambayo mteja akijaza, mfumo ufanye makadirio ya Haki bila mtu kuja kupanga foleni maofisini.

Nipo Gongo la Mboto ofisi za TRA, kuna watu wamesimama, ofisi Zina feni kwaajili ya Wafanyakazi, Wateja wanajipepea kupata hewa nzuri na kupunguza joto, wateja wamesimama wengine mpaka nje. Mazingira sio rafiki, Maofisa wenyewe wa kukadiria Wana watu wengi, hata ukija, hujui utakaa muda gani. Teknolojia zifanye maisha yetu kuwa rahisi. Kuliko Hali ilivyo.

Sio jambo zuri kuacha kazi kuja kukaa bila kufanya kitu Kwa masaa.

Mungu Ibariki Tanzania, Tupe Akili na Hekima Kwa manufaa ya Taifa.
Duu
 
Mkuu ni nini kilikuzuia kwenda Kufanyiwa Makadirio toka mwezi wa Kwanza?
 
ni utaratibu ule ule wa kiafrika mteja kwao ni mbwa wala hawana thamani naye, hakuna kitu kinachokwenda nchi hiyo zaidi ya uchawa tu na kujipendekeza na kutajataja jina la hangaya kila sehemu hata kama halihusiki. SHAME
 
Back
Top Bottom