Elections 2010 Majukumu Makuu ya CHADEMA

Mzee Mtei siku zote kumbuka kuwa kumsema mwenzio ni raha saaana na kusemwa wewe ni chungu mno.

Wewe Mwl hakukupa fursa ya kukusikiliza na badala yake ukatimuliwa (though wewe unadai ulishaamua kuacha kazi pia). Au nikuulize, je wakati unatimuliwa kulikuwa na demokrasia? Ulisikilizwa kama ulivyostahili? Je wale wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kesi zao zipo mahakamani wanaposemwa kwenye majukwaa ya kisiasa unafikiri wanajisikiaje? (nchi yetu ni ya utawala wa kisheria kumbuka) Ungekuwa ni wewe unatuhumiwa tu (na moyoni unajijua hauko fisadi) unaposemwa hadharani utajisikiaje?

Tufikirie leo viongozi au wagombea wa vyama wanaanza kutuhumiana kwa tuhuma binafsi tutakuwa tanatathmini nini? Tuhuma ama hoja za kuleta maendeleo? Kama CCM walivyo na mapungufu hata Chadema pia mnayo, think about tribalism scandals, ufisadi wa Mbowe (two years ago), (au unataka kusema mliliona hilo ndiyo maana mkaamua Mbowe asigombee Uraisi?), uadilifu ktk maisha ya kindoa n.k. Kumbuka kwa kila mahali kuna aina ya watu tofauti tofauti, kuna wazuri na wabaya, wema na wasio wema, wezi na waibiwa, na kadhalika na kadhalika.

Unaweza ukawa mwanzilishi wa Chama ukifikiria kuwaletea watu wako mabadiliko ya kiuchumi kumbe wenzako ulio nao pamoja wanafikiria Chama hicho hicho kitawafanya wachumie matumboni mwao. Kama ilivyo CCM hata nanyi Chadema ni vivyo hivyo. Hata mabadaliko mnayoyasema yataonekana kwa siku 100 ni ndoto tu, its just a gear of bringing political change rather not solving core problems facing our country!

Usitudanganye sana Mzee Mtei! kuwa halisi, Sio wote tunakubaliana na wewe!

Tunajua mmejipanga wengi wa aina yako kama sisimizi. Hapa ni spray tu ya kuwafutilia mbali. Shwain.
 
salaama
  • profile.png
    View Profile
  • forum.png
    View Forum Posts
  • message.png
    Private Message
  • article.png
    View Articles
  • add.png
    Add as Contact
user-offline.png

Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png

Join Date Wed Aug 2010
Posts 8
Thanks : 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power






Avanti
user-offline.png

Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png

Join Date Tue Aug 2010
Posts 3
Thanks : 0
Thanked 0 Times in 0

PEOPLEZZZZZZZZZZZZZZZZZZZZZ POWEEEEER

2010 HATUDANGANYIKI




0
 
Watu kama mzee Mtei ni wa kuheshimiwa sana.

Mkuu mzee Mtei unafahamu mengi na tunakuombea Mungu azidi kukupa uhai ili utuoneshe njia ya kuwa na taifa la watu wenye kujua nini wanafanya kuleta maendeleo Tanzania.

Tanzania ya leo si Tanzania ya miaka ya 47, ina watu wenye upeo wa hali ya juu na sasa wanajua kuchambua kati ya pumba na mchele.
 
Unajua haya mapandikizi ya August 2010 wanataka kujenga hoja Chadema haijatapakaa nchi nzima, ili tuwasadiki wakati ule watakapokuwa wameiba kura za vijijini, eti tutaridhika! Hapana ! No no no! Operesheni Sangara imefungua njia na tunajua kabisa kura za vijijini kwingi tu tunazo, ole wenu mkiziiba!
 
Tunajua mmejipanga wengi wa aina yako kama sisimizi. Hapa ni spray tu ya kuwafutilia mbali. Shwain.

Unataka niwaze, nifikiri na nitende kama wewe? Hatujaumbwa hivyo, na ndiyo maana ya kuwa na demokrasia. Leta hoja, acha matusi.

Even if I am young member in the jamii forums I may be knowing it more than you.
 
Mzee Mtei;

Ni vema kuwa kuanzia Kipindi hiki CHADEMA ikaanza kujijengea "mtandao wa watu" kuanzia mitaani tunamoishi. CCM wana mfumo wa nyumba 10 na wote tunajua kuna mtu anaitwa balozi au mjumbe.

Mitaani kwetu kuna bendera luluki za wajumbe hawa.

CHADEMA ni vema ibuni mfumo sambamba na wa CCM au bora zaidi ili waweze kushinda.

Pili, tumia uzoefu wako na busara yako kuunganisha nguvu na vyama vyenye Nguvu. Chama kama CUF kama mtafanikiwa kitabalance vema.

Najua wasiwasi uliopo wa kutoa kuaminiana na kila chama kukituhumu kingine kuwa ni wakala wa CCM. Propaganda zilizopo kuwa CUF ni chama cha Waislam na wapemba na Chadema ni Chama cha Wakristo na Wachaga zinaweza tu kuepukika kwa nyie kupita vikwazo vyote, kuweka ubinafsi pembeni, maslahi ya taifa mbele na kuungana.

Ninayo imani kuwa kama uliyoyagusia na haya machache yakizingatiwa, come October and 2015 CHADEMA inaweza kuongoza Nchi.

Ieleweke kuwa wengine tunaamini maendeleo yatakuwepo kama kutakuwa na upinzani wa kutosha Bungeni hata kwa level ya 50-50%.
mimi najitolea kuwa wakala siku ya uchaguzi katika kituo au vituo katika jimbo la kawe dar es salaam, inshaallah
 
Unajua haya mapandikizi ya August 2010 wanataka kujenga hoja Chadema haijatapakaa nchi nzima, ili tuwasadiki wakati ule watakapokuwa wameiba kura za vijijini, eti tutaridhika! Hapana ! No no no! Operesheni Sangara imefungua njia na tunajua kabisa kura za vijijini kwingi tu tunazo, ole wenu mkiziiba!

Dhana ya 'mapindikizi' ni dhana ya mtu asiyekuwa na hoja...yaani mtu akitoa altenative views basi tayari ni pandikizi....mimi ningekuwa mpenzi wa kweli wa CHADEMA ningefuatilia kwa makini criticism zinazotolewa na kuzifanyia kazi..hata kama hazifurahishi masikio yangu.....sasa wewe subiria matokeo ya OPERESHENI SANGARA.....utashangazwa OCTOBER 31. Hakuna wa kuwaibia chochote....mnaji defeat wenyewe kwa kushindia ndoto ya ushindi pasipo kuwa na mikakati ya kisayansi....... angalieni wapinzani makini wanavyofanya kuchukua nchi.....cheki reference ya Barak Obama alivyofanya.....cheki reference ya NPP ya Ghana na Prof John Atta Mills walivyofanya. Ukweli inabaki pale pale CHADEMA is no where near what NPP was. Nendeni mkajifunze vizuri kwa wenzenu ndio mtaelewa ninachosema...

HAIBIWI KURA MTU YOYOTE......suala ni CHADEMA haijajenga ushawishi wa kutosha na kuaminika kwenye GRASSROOT.... laiti kura zingekuwa zinapigiwa kwenye JAMII FORUM..I can guarantee kwamba mgepata asilimia 110% including na za wizi.... lakini as long as kura zinapigiwa kule vijijini....BADO BADO hamjajipanga vya kutosha.....ANZENI SASA KUJIPANGA KWA AJILI YA 2015...
 
Dhana ya 'mapindikizi' ni dhana ya mtu asiyekuwa na hoja...yaani mtu akitoa altenative views basi tayari ni pandikizi....mimi ningekuwa mpenzi wa kweli wa CHADEMA ningefuatilia kwa makini criticism zinazotolewa na kuzifanyia kazi..hata kama hazifurahishi masikio yangu.....sasa wewe subiria matokeo ya OPERESHENI SANGARA.....utashangazwa OCTOBER 31. Hakuna wa kuwaibia chochote....mnaji defeat wenyewe kwa kushindia ndoto ya ushindi pasipo kuwa na mikakati ya kisayansi....... angalieni wapinzani makini wanavyofanya kuchukua nchi.....cheki reference ya Barak Obama alivyofanya.....cheki reference ya NPP ya Ghana na Prof John Atta Mills walivyofanya. Ukweli inabaki pale pale CHADEMA is no where near what NPP was. Nendeni mkajifunze vizuri kwa wenzenu ndio mtaelewa ninachosema...

HAIBIWI KURA MTU YOYOTE......suala ni CHADEMA haijajenga ushawishi wa kutosha na kuaminika kwenye GRASSROOT.... laiti kura zingekuwa zinapigiwa kwenye JAMII FORUM..I can guarantee kwamba mgepata asilimia 110% including na za wizi.... lakini as long as kura zinapigiwa kule vijijini....BADO BADO hamjajipanga vya kutosha.....ANZENI SASA KUJIPANGA KWA AJILI YA 2015...

Huo ndiyo ukweli ila unaumiza!!!
 
Dhana ya 'mapindikizi' ni dhana ya mtu asiyekuwa na hoja...yaani mtu akitoa altenative views basi tayari ni pandikizi....mimi ningekuwa mpenzi wa kweli wa CHADEMA ningefuatilia kwa makini criticism zinazotolewa na kuzifanyia kazi..hata kama hazifurahishi masikio yangu.....sasa wewe subiria matokeo ya OPERESHENI SANGARA.....utashangazwa OCTOBER 31. Hakuna wa kuwaibia chochote....mnaji defeat wenyewe kwa kushindia ndoto ya ushindi pasipo kuwa na mikakati ya kisayansi....... angalieni wapinzani makini wanavyofanya kuchukua nchi.....cheki reference ya Barak Obama alivyofanya.....cheki reference ya NPP ya Ghana na Prof John Atta Mills walivyofanya. Ukweli inabaki pale pale CHADEMA is no where near what NPP was. Nendeni mkajifunze vizuri kwa wenzenu ndio mtaelewa ninachosema...

HAIBIWI KURA MTU YOYOTE......suala ni CHADEMA haijajenga ushawishi wa kutosha na kuaminika kwenye GRASSROOT.... laiti kura zingekuwa zinapigiwa kwenye JAMII FORUM..I can guarantee kwamba mgepata asilimia 110% including na za wizi.... lakini as long as kura zinapigiwa kule vijijini....BADO BADO hamjajipanga vya kutosha.....ANZENI SASA KUJIPANGA KWA AJILI YA 2015...

Hivi wewe unajua historia ya vyama vingi Tanzania? KUDADADEKIIII!!!
Sema vilianza lini na CCM ilianza lini kupora mali zilizojengwa na watanzania wote
 
Unajua haya mapandikizi ya August 2010 wanataka kujenga hoja Chadema haijatapakaa nchi nzima, ili tuwasadiki wakati ule watakapokuwa wameiba kura za vijijini, eti tutaridhika! Hapana ! No no no! Operesheni Sangara imefungua njia na tunajua kabisa kura za vijijini kwingi tu tunazo, ole wenu mkiziiba!

Kwa uelewa wangu pandikizi...ni stranger asiye belong kwenye kundi Fulani....It is only natural kwa watu wa kundi husika ku resent against stranger huyo kwasababu mtu wa aina hiyo siku zote hakuwa sehemu ya kundi lao, ameibuka ghafla na kujiingiza katika kundi na kuanza kutoa mawazo yake ambayo ni tofauti na mtazamo wa kundi zima....hivi ndivyo baadhi yetu tunavyoonekana ndani ya JAMII FORUM

The same analogy could be drawn kule kwenye mchakato wa uchaguzi majimboni...... CCM imejikita majimboni, ina mfumo ulio active kuanzia wajumbe wa mashina, viongozi wa matawi, viongozi wa kata, viongozi wa wilaya na viongozi wa mkoa.....system yote hii ipo karibu na wananchi..siku zote..ni sehemu ya mfumo wa maisha kule vijijini...... hivyo inapofikia kipindi kama hiki cha uchaguzi....wapiga kura wengi (hasa vijijini) wanaji identify na mfumo waliouzoea, mfumo wanaoishi nao..... mifumo ya ya chadema iliyokuwa inactive miaka yote na kuibuka kipindi cha uchaguzi...kwa formula ile ile ya ndani ya jamii forum niliyoitaja juu......wanakumbana na resentment ya wananchi....hawajui jamaa hawa wanatokea wapi, walikuwa wapi, mbona lugha yao ni ya tofauti na lugha tuliyozoea kuisikia.....and eventually wanawakataaa....hawawapigii kura.

Soooo there you go...CHADEMA needs to build systems kwenye grassroots....kwa sasa hawana system....ndio maana leo inawalazimu heavy weights wale wale akina MARANDO, MPENDAZOE kuhusika na uzinduzi wa kampeni katika kila jimbo...juzi walikuwa Ubungo, Jana walikuwa Kawe, Kesho wataenda Ukonga..hiyo yote ni kwasababu kule majimboni CHADEMA haina watu.....na hili litakuja kuwagharimu sana....haiwezekani Lwakatare amudu vizuri majukumu ya kampeni zake za Ubunge katika jimbo la Bukoba Mjini,wakati huo huo a play a role ya msaidizi wa Mhe. Slaa kwenye kampeni nchi nzima.....kwa hali hiyo, LWAKATARE akishindwa Ubunge Oktoba, utalalamika kweli kwamba ameibiwa KURA? Kwa taarifa nilizonazo...kule Bukoba Mjini, ukiachilia CCM, CUF bado ina grassroot base ambayo ni lazima LWakatare apambane nazo ili kushinda.

Tofauti na hali ilivyo kwa CHADEMA, tukiangalia upande wa CCM....majimbo mengi yameshazindua kampeni zake.....hawakusubiri...Kinana, Msekwa waende kule majimboni kwenye uzinduzi...ni kwasababu systems zipo mpaka kwenye grassroot.....anapopita Mhe. Kikwete kwenye maeneo yale, anachofanya ni kuwawekea uzito zaidi wagombea hao.

Tatizo la CHADEMA kutokuwa na grassroot base linawafanya wazidiwe hata na CUF.....CUF pamoja na kutokuwa na majimbo ya ubunge huku Bara, wanazo grassroot base zao zilizo active..ndio maana in terms of IDADI ya kura...Prof Lipumba hujikuta akipata kura nyingi kuliko mgombea wa CHADEMA..
Until something is done........msitegemeee maajabu yoyote ya ushindi... Na wale wanaodhani OPERESHENI SANGARA italeta impact, ninasikitika kuwaambia....sio rahisi... LAITI MFUMO ULIO ACTIVE TOKA CHINI ungekuwepo...OPERESHENI SANGARA ingekuwa na maana kwani ingekuwa ina invigorate kazi inayofanywa na makada wetu walipo ACTIVE kwenye grassroot on full-time basis....
 
CHADEMA is getting their priorities wrong....

Mzee Mtei, anadai JUKUMU KUBWA WALILONALO NI KUFICHUA UOZO WA CCM NA KUCHUNGA KURA......in my view that is a very misguided priority....ni kwa jinsi hii..lazima CHADEMA ishindwe uchaguzi mkuu ujao..kwani chama chochote chenye nia ya kupata ushindi...priority yake ya KWANZA ni KUTAFUTA KURA... Kwanza uzipate kura hizo, then ndio uzilinde..

Kura zinapatikanaje? Kura hazitafutwi kwa njia ya kuelezea mapungufu ya wapinzani wako pekee, na kupandisha jazba....kura zinatafutwa kwa kuwafikia wapiga kura na kuwaelezea mpaka waelewe utawafanyia nini, msimamo wako kuhusu mambo yanayowagusa ni upi......

Wapiga kura wapo wapi?.....80% ya wapiga kura wa Tanzania wapo vijijini...sioni kama CHADEMA wana any mechanism ya kufikia wapiga kura walio wengi...zaidi ya kwenda na helikopta siku moja kupiga debe kisha wanaondoka...... CCM kwa upande mwingine wana mechanism inayowafikia wapiga kura...wana mtandao wa wajumbe wa nyumba kumi kumi, wana mfumo wa uongozi ulio hai FULL-TIME kuanzia kwenye matawi , kata, wilaya, mkoa... Mfumo huo upo active wakati wote kabla ya uchaguzi, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.....

CHADEMA hawa mfumo imara kama wa CCM, mifumo yao inakuwa active wakati wa vipindi vya uchaguzi na baada ya uchaguzi zinarudi kuwa inactive....ndio maana wameshindwa kuwa na wagombea wenye kukidhi vigezo vinavyotakiwa na tume ya uchaguzi katika MAJIMBO kwa ajili ya nafsi za UBUNGE na UDIWANI..... na ni kwasababu hiyo, wapiga kura hasa walio vijijini hawana attachment na CHAMA husika kwasababu....hawawajui....hawako active kwenye maeneo yao, wakati wa heri na taabu.

Kwa hili...tu lazima tukubali ukweli kwamba, haitokuwa rahisi kwa CHADEMA kupata ushindi ambao wapenzi wake wanatamani upatikane.....ushindi haupatikani by mere wishes...unafanyiwa kazi....wengi wenu mlio USA mnakumbuka...organization ya Barak Obama..iliyoanzia kweye grassroots ndio iliyompa mtaji mkubwa wa kushindana ndani ya CHAMA CHAKE na baadaye kwenye uchaguzi mkuu.....MHESHIMIWA WILBROAD SLAA hana base hiyo.....hata hii FRIENDS OF SLAA imechelewa sana.....ilitakiwa mobilization ya FOS ianze miaka 5 iliyopita...na sio leo hii dakika za lalasalama na kuanza kuchangisha pesa kwenye mkutano wa hadhara....it is too late.....Msidhani uelewa na ushabiki mlionao ndani ya mitandao ya aina hiii.....ndio hali ilivyo kwa wananchi kule Nanyumbu, Msalasala, Iyungo, Kojani, Katavi, Ileje etc etc

Ni kweli wapiga kura siku hizi hawadanganyiki....kama KAULI MBIU YA CHADEMA inavyosema....ni uelewa huo huo wa wapiga kura wasiodanganyika..watatambua kwamba ahadi nyingi zinazotolewa na mgombea wa CHADEMA za kufanya mambo within 100 days ni uongo mtupu....KWELI HAWATADANGANYIKA....

Ushauri wa Bure kwa Chadema:
Wekeni nguvu zenu ku retain majimbo ya Ubunge mliyokuwa nayo last time...na kuweka nguvu kwenye yale majimbo ambayo prospects za kupata ni kubwa...(hasa yale maeneo ambayo wagombea wa CCM wapo weak au yale maeneo ambayo wagombea wenu wapo strong)......KWa kufanya hivyo, mtapata reasonable number of seats itakayowawezesha kuwa Chama Kikuu cha Upinzani Bungeni.....na kwa jinsi hiyo, mtakuwa na suati zaidi ya kutoa constructive criticism kwa serikali.....


Msipofanya hivyo,,,,mkaishia kutawanya nguvu zenu kila mahala.....I can assure you....mtaishia kupata majimbo idadi ile ile ya last time na pengine pungufu zaidi na CUF wataishia kuwa CHAMA KIKUU CHA UPINZANI BUNGENI

Sinshangai mkuu kwa statistics zako hapa chini, wale wale... tena uko so organized; UMETUMWA!!!!!


salaama
user-offline.png
Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
Join Date Wed Aug 2010
Posts 12
Thanks : 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power:becky:
 
..binafsi sipigi kura kwa kuangalia kama chama kina mtandao nchi nzima ama la.

..napigia kura candidate, and this time nadhani Slaa atatufaa.

..rekodi ya utendaji ya Kikwete inadhihirisha wazi kwamba ameshindwa uongozi.

..kama CCM iko karibu na wananchi, basi ni katika kuyakwaza, na kuyahujumu, maendeleo ya wananchi hao.

..I HOPE THIS TIME WANANCHI WATASIKILIZA KWA MAKINI HOJA ZA WAGOMBEA NA KU-JUDGE NANI ATAWAFAA.
 
ukitaka kujua ccm ina mapandikizi ona jinsi yasivyo na adabu hapa. mnashindwa kumheshimu mzee kama Mtei utamheshimu nani? hata kikwete anabidi awe macho nanyi. huenda ni yale ya Nyerere kuwa kikwete akiondoka mtakufa njaa
 
Mzee Mtei siku zote kumbuka kuwa kumsema mwenzio ni raha saaana na kusemwa wewe ni chungu mno.

Wewe Mwl hakukupa fursa ya kukusikiliza na badala yake ukatimuliwa (though wewe unadai ulishaamua kuacha kazi pia). Au nikuulize, je wakati unatimuliwa kulikuwa na demokrasia? Ulisikilizwa kama ulivyostahili? Je wale wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kesi zao zipo mahakamani wanaposemwa kwenye majukwaa ya kisiasa unafikiri wanajisikiaje? (nchi yetu ni ya utawala wa kisheria kumbuka) Ungekuwa ni wewe unatuhumiwa tu (na moyoni unajijua hauko fisadi) unaposemwa hadharani utajisikiaje?

Tufikirie leo viongozi au wagombea wa vyama wanaanza kutuhumiana kwa tuhuma binafsi tutakuwa tanatathmini nini? Tuhuma ama hoja za kuleta maendeleo? Kama CCM walivyo na mapungufu hata Chadema pia mnayo, think about tribalism scandals, ufisadi wa Mbowe (two years ago), (au unataka kusema mliliona hilo ndiyo maana mkaamua Mbowe asigombee Uraisi?), uadilifu ktk maisha ya kindoa n.k. Kumbuka kwa kila mahali kuna aina ya watu tofauti tofauti, kuna wazuri na wabaya, wema na wasio wema, wezi na waibiwa, na kadhalika na kadhalika.

Unaweza ukawa mwanzilishi wa Chama ukifikiria kuwaletea watu wako mabadiliko ya kiuchumi kumbe wenzako ulio nao pamoja wanafikiria Chama hicho hicho kitawafanya wachumie matumboni mwao. Kama ilivyo CCM hata nanyi Chadema ni vivyo hivyo. Hata mabadaliko mnayoyasema yataonekana kwa siku 100 ni ndoto tu, its just a gear of bringing political change rather not solving core problems facing our country!

Usitudanganye sana Mzee Mtei! kuwa halisi, Sio wote tunakubaliana na wewe!

CHADEMA is getting their priorities wrong....

Mzee Mtei, anadai JUKUMU KUBWA WALILONALO NI KUFICHUA UOZO WA CCM NA KUCHUNGA KURA......in my view that is a very misguided priority....ni kwa jinsi hii..lazima CHADEMA ishindwe uchaguzi mkuu ujao..kwani chama chochote chenye nia ya kupata ushindi...priority yake ya KWANZA ni KUTAFUTA KURA... Kwanza uzipate kura hizo, then ndio uzilinde..

Kura zinapatikanaje? Kura hazitafutwi kwa njia ya kuelezea mapungufu ya wapinzani wako pekee, na kupandisha jazba....kura zinatafutwa kwa kuwafikia wapiga kura na kuwaelezea mpaka waelewe utawafanyia nini, msimamo wako kuhusu mambo yanayowagusa ni upi......

Wapiga kura wapo wapi?.....80% ya wapiga kura wa Tanzania wapo vijijini...sioni kama CHADEMA wana any mechanism ya kufikia wapiga kura walio wengi...zaidi ya kwenda na helikopta siku moja kupiga debe kisha wanaondoka...... CCM kwa upande mwingine wana mechanism inayowafikia wapiga kura...wana mtandao wa wajumbe wa nyumba kumi kumi, wana mfumo wa uongozi ulio hai FULL-TIME kuanzia kwenye matawi , kata, wilaya, mkoa... Mfumo huo upo active wakati wote kabla ya uchaguzi, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.....

CHADEMA hawa mfumo imara kama wa CCM, mifumo yao inakuwa active wakati wa vipindi vya uchaguzi na baada ya uchaguzi zinarudi kuwa inactive....ndio maana wameshindwa kuwa na wagombea wenye kukidhi vigezo vinavyotakiwa na tume ya uchaguzi katika MAJIMBO kwa ajili ya nafsi za UBUNGE na UDIWANI..... na ni kwasababu hiyo, wapiga kura hasa walio vijijini hawana attachment na CHAMA husika kwasababu....hawawajui....hawako active kwenye maeneo yao, wakati wa heri na taabu.

Kwa hili...tu lazima tukubali ukweli kwamba, haitokuwa rahisi kwa CHADEMA kupata ushindi ambao wapenzi wake wanatamani upatikane.....ushindi haupatikani by mere wishes...unafanyiwa kazi....wengi wenu mlio USA mnakumbuka...organization ya Barak Obama..iliyoanzia kweye grassroots ndio iliyompa mtaji mkubwa wa kushindana ndani ya CHAMA CHAKE na baadaye kwenye uchaguzi mkuu.....MHESHIMIWA WILBROAD SLAA hana base hiyo.....hata hii FRIENDS OF SLAA imechelewa sana.....ilitakiwa mobilization ya FOS ianze miaka 5 iliyopita...na sio leo hii dakika za lalasalama na kuanza kuchangisha pesa kwenye mkutano wa hadhara....it is too late.....Msidhani uelewa na ushabiki mlionao ndani ya mitandao ya aina hiii.....ndio hali ilivyo kwa wananchi kule Nanyumbu, Msalasala, Iyungo, Kojani, Katavi, Ileje etc etc

Ni kweli wapiga kura siku hizi hawadanganyiki....kama KAULI MBIU YA CHADEMA inavyosema....ni uelewa huo huo wa wapiga kura wasiodanganyika..watatambua kwamba ahadi nyingi zinazotolewa na mgombea wa CHADEMA za kufanya mambo within 100 days ni uongo mtupu....KWELI HAWATADANGANYIKA....

Ushauri wa Bure kwa Chadema:
Wekeni nguvu zenu ku retain majimbo ya Ubunge mliyokuwa nayo last time...na kuweka nguvu kwenye yale majimbo ambayo prospects za kupata ni kubwa...(hasa yale maeneo ambayo wagombea wa CCM wapo weak au yale maeneo ambayo wagombea wenu wapo strong)......KWa kufanya hivyo, mtapata reasonable number of seats itakayowawezesha kuwa Chama Kikuu cha Upinzani Bungeni.....na kwa jinsi hiyo, mtakuwa na suati zaidi ya kutoa constructive criticism kwa serikali.....


Msipofanya hivyo,,,,mkaishia kutawanya nguvu zenu kila mahala.....I can assure you....mtaishia kupata majimbo idadi ile ile ya last time na pengine pungufu zaidi na CUF wataishia kuwa CHAMA KIKUU CHA UPINZANI BUNGENI

Mwalimu wenu ana matatizo
 
..binafsi sipigi kura kwa kuangalia kama chama kina mtandao nchi nzima ama la.

..napigia kura candidate, and this time nadhani Slaa atatufaa.

..rekodi ya utendaji ya Kikwete inadhihirisha wazi kwamba ameshindwa uongozi.

..kama CCM iko karibu na wananchi, basi ni katika kuyakwaza, na kuyahujumu, maendeleo ya wananchi hao.

..I HOPE THIS TIME WANANCHI WATASIKILIZA KWA MAKINI HOJA ZA WAGOMBEA NA KU-JUDGE NANI ATAWAFAA.

Joka kuu upo sahihi mtu anatakiwa kupiga kura kwa kuangalia sera za chama husika na sifa za mgombea wa chama hicho...lakini kwa mfumo wa siasa tuliopo, wapiga kura walio wengi..hasa wa vijijini bado wanapigia CHAMA...kwa mtaji huu....kura yako na watu wengine wenye mtazamo kama wako hazitoshi kumuingiza Mheshimiwa Dk Slaa IKULU. Hili somo la KUWEKEZA KWENYE GRASROOTS lazima lieleweke ili CHama chochote chenye kutafuta ushindi kifanikiwe barani Afrika.

Hapajawahi kutokea chama cha upinzani kilichopata ushindi simply kwa kufanya siasa za mijini na kwenye mitandao...ukiangalia cases chache za vyama vya upinzani vilivyoshinda uchaguzi na kuchukua dola,source yao kubwa ya ushindi ni GRASSROOT base...angalia kule Zambia Movement for Multiparty Democracy (MMD) cha Chiluba, kilitokea kwenye grassroots....kilipata support ya watu wa migodini na wakulima wa vijijini....ndipo wakaiangusha UNIP. Ukiangalia kule GHANA, the National Democratic Party (NDP) kiliweza kukiondoa chama tawala New Patriotic Party (NPP) kwasababu walikuwa na grassroot base (wao kwakuwa walishawahi kuwa madarakani chini ya General Rawlings) walishakuwa na mizizi kwenye grassroots. Actually ukifuatilia siasa za Ghana utaona kilichokuwa chama tawala (NPP) kilikuwa na wafuasi wengi mijini na kwenye diaspora kama ilivyo Chadema...lakini ndio hivyo...wakang'oka. (cheki allAfrica.com: Ghana: Ruling Party Set for Sweep in National Poll)

Hata ukiangalia kwa jirani zetu Kenya.....KANU ilitawala muda wote kwasababu ilikuwa na base kwenye grassroot...na kuondoka kwake maradarakani kulitokana na SPLIT ya KANU yenyewe.....na siasa za ukabila zilizotawala kwao huko.

To cut the long story short ushindi hauji kwa wishes na ndoto...LAZIMA CHADEMA irudi kwenye grassroots
 
Salaaama,
Mkuu umeandika vitu ambavyo mimi vimenishinda kabisa kufananisha wala kulinganisha.

Kwanza umetumia mifano ya Obama na Prof. John Evans Atta Mills kama mifano bora ya jinsi walivyoweza kufanikiwa. Hivi unachukulia maisha ya Obama na huyo Atta ukilinganisha na maisha ya Dr. Slaa au kitu gani?

Hawa watu, vyama vyao havikuanza jana kushika maradaka ya kuongoza. Yaani wamekuta tayari vyama vimekwisha jineemesha kisiasa na vimestawi iwejke ufananishe na Chadema mabcho hakijawahi kushika madaraka ya kuongoza nchi?..Hicho chama cha Domokratic cha Marekani huwezi kukifananisha na Chadema, na wala kusimama na hicho chama cha NPP ambacho pia umewapongeza.

Halafu navyojua mimi Atta sii kiongozi wa NPP isipokuwa anatoka chama cha NDC, chama alichokuwa akiongoza na Jerry Rawlings..hivyo ujenzi wa chama umeanza toka wakati ule na walisha ongoza nchi kwa muda mrefu kuliko unavyotaka wewe kutuhabarisha. Ingekuwa ushauri bora zaidi kwetu kama ungetumia mfano wa vyama hivi ni jinsi gani walianza hata kuweza kuchukua ushindi kwa mara ya kwanza kabisa ikiwa tunashabihiana kimazingira na malengo.

Mwisho, hao NPP ambao unasisitiza tuwasome hivi wamefanikiwa kipi haswa cha kufikia wewe kuwazungumzia kama mfano bora...na sidhani kama mazingira yetu yapo sawa kwani kila chama kimeundwa ktk mazingira yake, watu wake nam malengo tofauti hivyo muundo wa itikadi hauwezi kufanana..
 
Salaaama,
Mkuu umeandika vitu ambavyo mimi vimenishinda kabisa kufananisha wala kulinganisha.

Kwanza umetumia mifano ya Obama na Prof. John Evans Atta Mills kama mifano bora ya jinsi walivyoweza kufanikiwa. Hivi unachukulia maisha ya Obama na huyo Atta ukilinganisha na maisha ya Dr. Slaa au kitu gani?

Hawa watu, vyama vyao havikuanza jana kushika maradaka ya kuongoza. Yaani wamekuta tayari vyama vimekwisha jineemesha kisiasa na vimestawi iwejke ufananishe na Chadema mabcho hakijawahi kushika madaraka ya kuongoza nchi?..Hicho chama cha Domokratic cha Marekani huwezi kukifananisha na Chadema, na wala kusimama na hicho chama cha NPP ambacho pia umewapongeza.

Halafu navyojua mimi Atta sii kiongozi wa NPP isipokuwa anatoka chama cha NDC, chama alichokuwa akiongoza na Jerry Rawlings..hivyo ujenzi wa chama umeanza toka wakati ule na walisha ongoza nchi kwa muda mrefu kuliko unavyotaka wewe kutuhabarisha. Ingekuwa ushauri bora zaidi kwetu kama ungetumia mfano wa vyama hivi ni jinsi gani walianza hata kuweza kuchukua ushindi kwa mara ya kwanza kabisa ikiwa tunashabihiana kimazingira na malengo.

Mwisho, hao NPP ambao unasisitiza tuwasome hivi wamefanikiwa kipi haswa cha kufikia wewe kuwazungumzia kama mfano bora...na sidhani kama mazingira yetu yapo sawa kwani kila chama kimeundwa ktk mazingira yake, watu wake nam malengo tofauti hivyo muundo wa itikadi hauwezi kufanana..

Kaka Mkandara, kwanza niombe radhi kwa mixup ya NDC na NPP...nashukuru kwa kusaihisha..
Pili naomba nitofautiane na wewe, suala la chama kuwa kikongwe sio automatic ticket ya kuweza kuji organize na kupata ushindi...laiti ukongwe ungekuwa ndio kigezo cha organization, basi KANU isingeanguka mara mbili toka itoke madarakani na UNIP isingeanguka zaidi ya mara nne toka kitoke madarakani...na hivi ni vyama vikongwe vyenye historia tangu enzi za kumtoa mkoloni..

Kwa mtazamo wangu kinacho matter...sio uzee, wala uchanga wa chama...kinacho matter ni kuwa na ORGANIZATION na mikakati inayokiwezesha chama kuwafikia walengwa (wapiga kura)....hicho ndicho MMD ya ZAMBIA walifanya...na hicho ndicho CHADEMA wanaweza kufanya 2015 na huko mbeleni....ila kwa sasa CHADEMA HAIJAWAFIKIA WAPIGA KURA VIJIJIN na HIVYO USHINDI 2010 NI NDOTO....

Anzeni kazi ya kujijenga sasa, na baada ya uchaguzi....MWISHO wa uchaguzi ndio usiwe mwisho wa ujenzi wa chama kwenye grassroots....
 
Kaka Mkandara, kwanza niombe radhi kwa mixup ya NDC na NPP...nashukuru kwa kusaihisha..
Pili naomba nitofautiane na wewe, suala la chama kuwa kikongwe sio automatic ticket ya kuweza kuji organize na kupata ushindi...laiti ukongwe ungekuwa ndio kigezo cha organization, basi KANU isingeanguka mara mbili toka itoke madarakani na UNIP isingeanguka zaidi ya mara nne toka kitoke madarakani...na hivi ni vyama vikongwe vyenye historia tangu enzi za kumtoa mkoloni..

Kwa mtazamo wangu kinacho matter...sio uzee, wala uchanga wa chama...kinacho matter ni kuwa na ORGANIZATION na mikakati inayokiwezesha chama kuwafikia walengwa (wapiga kura)....hicho ndicho MMD ya ZAMBIA walifanya...na hicho ndicho CHADEMA wanaweza kufanya 2015 na huko mbeleni....ila kwa sasa CHADEMA HAIJAWAFIKIA WAPIGA KURA VIJIJIN na HIVYO USHINDI 2010 NI NDOTO....

Anzeni kazi ya kujijenga sasa, na baada ya uchaguzi....MWISHO wa uchaguzi ndio usiwe mwisho wa ujenzi wa chama kwenye grassroots....
Bila samahani.. ndio tupo hapa kujadili na sii kubishana.. karibu sana mkuu wangu. Kwa hiyo maelezo yako yote ya kwanza hayana nguvu kama utaamini ukongwe sio kigezo isipokuwa ni kuwafikia wananchi (wapiga kura) vijijini?.

Pili, nafikiri Chadema wamefanya mengi kuwafikia wananchi vijijini kuliko hata hivyo vyama ulivyovisema. Sasa kama swala ni mikakati ya kuwafikia wananchi wa vijijini sidhani kama vyama vyote ulivyovitaja vimeweza kufanya zaidi ya Chadema pasipo ukongwe wao ktk siasa..Hao MMD unaozungumzia wao walikuwa na agenda moja tu. Nayo ni kuwaondoa UNIP madarakani jambo ambalo Chadema wamejipanga pia wakiwa na lengo hilo hilo.

Na sii kweli kwamba MMD waliweza kuwafikia wananchi wapiga kura vijijini isipokuwa wananchi wenyewe wa Zambia walitaka CHANGE ya uongozi baada ya Kaunda na UNIP kushindwa kuwaletea maendeleo kwa zaidi ya miaka 40 ya utawala wao. Wakaelewa malengo ya chama kipya na viongozi waliokimbia UNIP tofauti na sisi. Kwa hiyo utaona kwamba tofauti iliyopo baina ya Zambia, Kenya, Ghana au hata Marekani na sisi ipo kwa wananchi wenyewe.

Watanzania kwa uzoba wetu bado tunafikiria kwamba hakuna jema linaloweza patikana wakitoka CCM. Bado tuna mawazo mgando ya yaliyogandishwa toka tupate Uhuru na Changes zozote zile za kiutawala zitaondoa Unyenyekevu na amani (utumwa wa fikra) hivyo kuhofia kutokitegemea chama CCM kwa maendeleo ya nchi yetu..Kwa maana kwamba akili ya mtumwa siku zote humtazama na kulinda maslahi ya bwana (master) wake ili apate riziki yake..Na ndicho kinachoendelea hadi leo kiasi kwamba hata Chadema wafanye nini bado wapo watu wenye mtazamo unaotisha yaani pasipo CCM (masters) hakuna maisha..

Chadema wameweza kuanzisha operation Sangara hadi vijijini lakini nambie ni Watanzania wangapi wanataka hata kujua yaliyomo ktk operation hiyo. Na sii ajabu nazungumza na wewe hapa lakini hujawahi kupitia Operation Sangara na kufahamu mafundisho yake yaani siasa kwetu imekuwa kama dini. Wapo waislaam au Wakristu hawajawahi maishani mwao kushika kitabu cha dini nyingine hata kusoma tu kufahamu kina maagizo gani...

Hata baada ya Chadema kuwapeni wananchi Ilani yao ya uchaguzi bado wengi wana amini Chadema haijawafikia wananchi vijijini hali huwezi kunambia hata sehemu moja iwe kata au nyumba kumi Kitaifa wasiojua kuna chama Chadema na kina malengo ya kuwaondoa CCM madarakani. Ila sema tu kwamba katika sehemu zote hizo vijijini, wananchi wengi wamebatizwa ktk jina la CCM na hawaoni imani nyingine zaidi ya CCM kiasi kwamba sii jukumu la Chadema tena kuwalazimisha wananchi wapate kuifuata.

Chadema wamezungumzia umuhimu wa kuwaondoa CCM madarakani, lakini nambie ni Watanzania wangapi (wapiga kura) wako tayari kuona hilo linatokea! nadhani utasema sii wengi lakini nakuhakikishia kwamba mwaka huu, CCM wana wakati mgumu sana kisiasa kwa sababu wananchi wengi wamechoka na ndio maana hata wewe umezungumzia zaidi hofu yako kwa Chadema kuliko wakati mwingine wowote sawa na mzazi ambaye kaambiwa na mwanaye kwa mara ya kwanza kuwa amepata mchumba!...Mkuu wangu Chadema imefikia muda wa kuchukua majukumu mazito na hakuna muda wa kufikiria kujipanga hadi vijijini ambako sii swala la kuweka majengo isipokuwa IMANI ya kubadilisha uongozi wa nchi yetu kwa mara ya kwanza baada ya CCM kushindwa kuyafikisha maendeleo kwa wananchi vijijini..

Tazama mikutano yooote ya CCM, kwa waliohudhuria utagundua kwamba asilimia kubwa wamevaa magwanda ya kijani na njano..yaani wanachama. Umati mkubwa umelembwa na rangi za chama tofauti na Chadema ambao utawaona walalahoi wapiga kura wakihudhuria mikutano yao kupokea ilani ya chama wakati ile ya CCM wengi wanakuja kumwona rais wao kwa mara ya kwanza baada ya kuishi Ulaya (ooops) kwa muda mrefu.

Kikubwa sio swala la Chadema kushindana na CCM kuwafikia wananchi vijijini ila ni Chadema kuwapelekea maendeleo wananchi wa vijijini..
 
Uchaguzi kila mara ni deal kwa watu wanaogombea uongozi hakuna hata mmoja anayejali maslahi ya wananchi, ukipiga kura unawaongezea nguvu walaji wajisifu kuwa tumepata kura nyingi lakini hakuna lolote. Kuna tofauti kidogo au afadhali tu lakini sio kwamba wanatujali kwa sana. Kuanzia wabunge mpaka hao wanaokimbilia Ikulu hakuna demokrasia ya kweli. Kiongozi akishachaguliwa anahama mji wake anahamia jiji lenye maraha mpaka siku za uchaguzi zifike tena. Mbunge wa Arusha haishi safari za Dar es salaam na hii ni kwa majimbo mengi tu Tanzania.Mpaka hii leo hakuna mbunge yeyote aliyewahi kuthubutu kukaa kwenye mji wake na kujaribu kuwasiliana na kukusanya mawazo na kero za waliomchagua kwamba sasa hivi kipindi cha bunge kimewadia je tukazungumze nini? In Fact mtu anaamka asubuhi anafika kwenye kikao anasema yake tu yaliyomjia siku hiyo bora kasema tu na kibaya zaidi unawaona wengine kwenye kikao wanadiriki kusinzia. Nchi sijui inakwenda wapi na sijui tufanyeje wajirekebishe hawa. tunataka maendeleo ubinafsi umepitwa na wakati.
 
Back
Top Bottom