kama ni pesa watahonga hadi basi, ila kura zetu zitaenda kwenye chama kingine ila siyo ccm
Kwani hapo suala ni kumjua kiongozi kwa sura? Kwani hapo alitakiwa kumjua hakimu kwa sura? Mimi sijaona mahali ambapo wamesema kwamba amewekewa pingamizi kwa vile alishindwa kumjua hakimu kwa sura!! Suala hapo ni kutoandikwa jina la hakimu ingawa maelezo yanasema imetiwa saini mbele yangu: Jina la Hakimu........................Sasa hapo kumjua kwa sura imetoka wapi? Huyu mgombea naye katia aibu kwa kweli unashindwa kuona vitu kama hivyo? Wewe unabebelea li-fomu ambalo halina jina!! Shame on him! Na huyo Mkurugenzi naye kasaidia sana hilo jimbo lichukuliwe bila kupingwa, kwa nini alipoona hizo kasoro hakumweleza huyo mgombea arudishe hiyo fomu ili ikaandikwe jina? Mbona tume wenyewe walimruhusu Rungwe kurudia picha alizokuwa amezisahau nyumbani? Nafikri kwa wakurugenzi wetu wao wangepokea tu hizo fomu ili iwe rahisi kwa maccm kuweka pingamizi. Hapa NEC inatakiwa itumie tu akili ya kibinadamu kumrudisha huyo jamaa kwenye kinyang'anyiro!!eti jibu ni hapana!! watu smart hua wanawajua viongozi wao kwa sura mkuu,,, sasa mgombea ubunge mzima kutomjua hakimu we haikuumizi kichwa hata kidogo au ndo zile tabia zetu za kila siku za kuwapa lawama wengine kwa kila ujinga tunaoufanya? ni kweli huelewi mkuu ama unajitia tu hamnazo?
Kama ni mtu makini,kwann afanye makosa ya kijinga ktk masuala muhimu,hii inaonesha hata angepata uongozi,asingeweza kuwa serious,msitee uzembe...
CCM Wapi wamepingwa?
Huu mjadala ni wa watu wenye ubongo mpana. Sidhani kama unaweza kuona mantiki kwenye hoja yakembona hausemi bungeni napo kuwepo na kitengo cha kusaidia wabunge kusoma miswada?hv mbunge mzima anashndwa kuhoj kama huyu ninayeruhusu anisainie ni hakimu ama sio hakimu mpaka kitengo cha usaidiz kiwepo kwel??hv viongoz wake walikua wap kuliona hili kabla hajarudisha,inaonesha viongoz waukawa hawakukagua na kujiridhsha ujazwaj wa fomu hzo!
Hizi sheria za NEC za kuweka mapingamizi ni kubaka demokrasia ni kiasi cha kuelekezana jinsi ya kijaza fomu, NEC walitakiwa kuwa na kitengo cha kusaidia kujaza fomu kama vile uhamiaji