Mgodo visa
JF-Expert Member
- Nov 1, 2016
- 3,589
- 3,639
Hakuna JINI Kafiri...!!
Huu uzi utalowana sasa hivi kwa mate! We subiri watoke talawei.
Huu uzi utalowana sasa hivi kwa mate! We subiri watoke talawei.
Hahahahaa kweli MAKATA jina maarufu la Majini,Kama alivyo maarufu Israeli.Na Mwenzake makata
Itakuwa duniani kote si unajua kuna pages mbili zilidondoka!!Huwa najiulizaga hivi huyo jini Maimuna anatambulika duniani kote kwa jina hilo Maimuna?maana ishu za majini zipo duniani kote.
Chief uliwahi kusikia jina linalojitambulisha kwa jina kama joseph, Aloyce au martha?Hakuna kitu kinatokea tokea hewani kila kitu kinasababu zake. Umeandika lakini sijajua kama hizo sentensi zako umezielewa
1. Hao mbwa wanapewa majina ya kikiristo sababu wanaishi na wakristo lakini mbwa siyo wakristo lakini wanauhusiano na wanakristo yaani wanaishi na watu wakristo.
2. Tukirudi kwenye mada, inaonesha majini wanaabudu kwenye dini ya kiarabu ndiyo maana lugha, majina na mavazi yanaendana na jamii ya kiarabu
3. Dini ya Kiarabu inasema "Mungu kaumba majini. Wapo majini wanaomubudu Allah, na wapo wasiomuabudu na pia kuna majini azuri na wabaya. Kwa wakristo ndiyo wanakubali kuwa Mungu kawaumba majini lakini hakuna jini linalomuabudu Mungu kwasababu ni malaika walioasi pamoja na shetani. Kiufupi hakuna jini mzuri au mbaya wote ni wabaya. Kwa sentensi yenu bado kuna uwalakini.
Mara nyingine shetani hujifanya malaika wa nuruMashetani aka Majini aka Mapepo yapo yameumbwa na Mungu kama tulivyoumbwa sisi Binaadamu.
Mungu kaumba MALAIKA, MAJINI na BINAADAMU ili wamuabudu tu, na sio chengine, na viumbe wasiomuabudu Mungu amewaekea adhabu kali
Marehemu Bibi yangu alikuwa hajui kusoma wala kuandika,lakini pale Shetani aka pepo anapokuwa amepanda kichwani kwake alikuwa anaweza kuongea kiarabu fasaha kabisa..
Marehemu Baba alikuwa ana uwezo wa kumwita jini wa Bibi, alipokuwa anamwita familia nzima inatakiwa wepo, Alikuwa ni jini wa famili, chakula chake kulikuwa, Asali, muwa, manda
Yule juni alikuwa anatusalimia kwa kutuzungusha shingo, kutunyoosha mkono huku Akisema "zein, zein", baba alikuwa anamwita jini wa Bibi pale anapokuwa anataka msaada wa kitu fulani..
Jini wa Bibi alikuwa na Uwezo mkubwa Sana, jina lake lilikuwa sio la kiarabu bali ni la kiswahili wa pwani, siku moja nilimsikia akisema wapi anatoka na yeye ni nani
Nilimsikia akisema yeye ni Mkuu wa Majini katoka sehemu fulani Pemba, vile vile alikuwa anawakilisha sehemu kubwa ya ufukwe wa Afrika Mashariki yaani, Mambasa, Unguja, Pemba, Kilwa..
Sitaki kutaja jina la huyu jini, kwakweli alikuwa na Uwezo wa ajabu Sana, uwezo wakuona na kutabiri, mambo mengi sana Alikuwa na Uwezo wa kuwaadhibu Majini wengine nk..
Haya mambo yapo, nimeyashuhudia mwenyewe, hivi viumbe vimeumbwa na Mungu,..
Yale tunayoyaona Makanisani ni "usanii", "utapeli",..huwezi kumtoa jini kwa kumpiga kelele, Majini wana vyakula vyao, wana njia zao za kuwaita na wana njia zao za kuwatoa,nimeyaona haya nikiwa na umri mdogo mpaka umri wa kumaliza Chuo
Tunatakiwa tujue kuwa hivi viumbe, ni kama sisi Binaadamu, wako wabaya na Wazuri, wako wanaomcha Mungu na wanaomuasi Mungu, lakini Wengi wao ni wa ha Mungu, wanaishi maisha marefu kuliko binaadamu
Kuitwa Mkiristo ni kawaida sana kazi ipo kuwa na imani ya kweli isiyo changanyika, huyo mbibi ni mlozi aka mchawiSiamini mambo ya Waganga, kwani ni wasanii, matapeli..
Siku moja nilikutana Bibi mmoja alikuwa na miaka kama 89,alikuwa mkristo, katika mazungumzo yetu aliniambia Kuwa mtoto wake wa kiume anaemtegea kapata wazimu amekuwa kuchaa
Nilimuuliza sasa amechukua hatua gani, kumsuru na huo ugonjwa, alilonijibu nilishangaa, sikuweza kuamini..
Aliniambia kampeleka kwa Sheikh kusomewa, nikamuliza Je mtoto wake alipata nafuu Akanijibu ndio, tena sana..
Nikamuuliza kwanini asimpeleke kwa Mchungaji wakati yeye ni Mkristo?! Akanijibu baba angu wewe acha tu!
Nilichanganyikiwa, nilishindwa kumfahamu yule Bibi.. Labda wadau mnaweza kunieleza kwanini imekuwa vile kwa huyu Bibi
Suleiman wa quran ni tofauti sana na wa bibliaKwa Mujibu wa kitabu cha Kurani Mungu hakuumba binaadamu peke yake, kaumba Malaika, Majini, Binaadamu, Wanyama na viumbe vyengine..
Nabii Suleiman(Solomon) Mungu alimpa uwezo wa kuongea na Majini pamoja na Wanyama..
Hivi viumbe vipo lakini havipo KISIASA, vina uwezo lakini tumeamriwa tusiviabudu..
Inawezekana, Biblia ni mkusanyiko wa vitabu haijulikani nani kaandika..Suleiman wa quran ni tofauti sana na wa biblia
Hapana yule Bibi alikuwa sio mchawi, Ukristo ni dini ya Kubuni, hakuna Hata sehemu moja katika Biblia Yesu kasema aabudiwe, au dini (gospel) anayoihubiri iitwe KristoKuitwa Mkiristo ni kawaida sana kazi ipo kuwa na imani ya kweli isiyo changanyika, huyo mbibi ni mlozi aka mchawi
Majini na Malaika ni viumbe viwili tafauti..Mara nyingine shetani hujifanya malaika wa nuru
TUNATUMIA JINA LA YESUHakika Quran haikuwacha kitu hata dawa na kinga hupatikana kwenye Quran. Masheikh wengi hutumia surat za Quran mfano suratul kursi ina kinga kubwa sana. Sasa sijui upande wa wakristo wao inakuwaje
Nangatukaa![]()
Sawa, lakini ukweli ni huo, huwezi kumtoa au kumfukuza kiumbe chenye uwezo kuliko Binaadamu, kiumbe kilichomsaliti Mungu, kwa kumpiga kelele, "kwa jina la Yesu, toka, toka...." inabidi ujiongeze kidogo
Sawa lakini je unaijua tofauti baina ya majini na masheitani?Majini na Malaika ni viumbe viwili tafauti..
Majini ni viumbe vilivyoumbwa na Mungu, viumbe hivi havionekani, vinaishi duniani, vinaishi katika jamii tafauti,pamoja na Binaadamu, vina makabila tafauti, vina Miji yao nkSawa lakini je unaijua tofauti baina ya majini na masheitani?
Labda kwa kukuweka sawa nahitaji tofauti hapo kwanza
Kwani Lucifer na Yesebeli ni nani!? Hayo ni majina tu ya Majini kama vile Asha na FatumaAahah Laiti Ungejua!
Watu wanapambana na Lucifer na Yezebeli.
Sembuse Jini???
Kuna siku kwenye tv nilikuwa namuangalia nabii mmoja anatowa watu mapepo basi akaja kijana ndio ana jini na anasema ni Lucifer,ila kilichonifurahisha zaidi ni kiingereza chake huyo Lucifer maana alikuwa anaongea kiingereza ila kilikuwa cha kutafuta maneno. Nikaona huyu Lucifer anatakiwa akapigwe msasa na Ras simba.Aahah Laiti Ungejua!
Watu wanapambana na Lucifer na Yezebeli.
Sembuse Jini???
Jini buji bujiJini Petro, jini Yohane, jini Yakobo hah haaa, hahaaa
Hii ni lugha gan mkuu,Hapana "ZEIN ZEIN", Alikuwa anakusudia salama salama au hamjambo...