Majaribuni mikononi mwa watu wa kitengo

Majaribuni mikononi mwa watu wa kitengo

Mkuu watu wa kitengo wasingekupa hata chance ya kuandika haya kama kweli walitaka uwe mmoja wao!
 
imagina
Nikiwa kidato cha tatu mwaka 2008 nilipata rafiki kijana mpole,mstaarabu kweli kweli ambaye alikua anafanya kazi serikalini lakini sikujua hasa ni ofisi ipi alikua anaifanyia kazi mpaka baadaye baada ya miaka miwili akili ilipopevuka kidogo. Kwasababu nilikua nasoma day school jioni nilikua naenda kwake tunakula,kunywa na kubishana story za mpira kidogo. Siku moja nilimpeleka home majira ya usiku saa mbili usiku.

Tulipomaliza kula nilimsindikiza mie nikarud home, ile naingia ndani tu bibi yangu ambaye kwa wakati huo alikua mtumishi kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya kwa takribani miaka 20 aliniuliza kwa mshangao "unaongea nini na watu wa security??" Sikumuelewa nilijua ni complications za bibi yangu maana alikua mtata kweli kweli na kwasababu alinilea tokea mdogo na alinichagulia hadi rafiki wa kuongea nao.

Miaka miwili baadaye nikiwa kidato cha tano siku moja nilirudi toka shule ilikua likizo fupi, nikaenda kwa jamaa yangu kumpa hi bahati mbaya alikua ametoka ila nilipompigia simu alinambia niingie ndani kwan mlango aliegesha na angenikuta hapo baadaye kidogo. Kwenye meza ya chakula kulikua na laptop na baadhi ya documents nilienda kuchukua ile computer ili nichek kama movies zitakuwepo maana nilitoka bweni kuhenyeka na misuli ya masomo nilikua na ukame wa movies.

Nilipoigusa ile PC Nilishtuka nilipoona ujumbe uliokiua kwenye mfano wa emails uliokua unampa jamaa yangu maekekezo ya kumfuatilia kwa kina aliyekua waziri wa miundombinu na uchukuzi kwa wakati huo tena ukimkomandi "haraka sana". Sikujua huyo jamaa ni nani mpaka amfuatilie professor yule, chini ya zile documents kulikua na ID iliyoeyesha jamaa alikua ni nani. Nilikuja kufikiria maneno ya bibi yangu nikachanganya na akili yangu kuwa nilikua karibu mno na "jasusi" la serikali na tokea hapo nikaanza kuwa makini na watu nnaongea nao. Sikuwahi kumuuliza jamaa kitu chochote maana nilianza kumuogopa na nilikua na mtizamo hasi kuhusiana na majasusi

Mwaka 2015 nikiwa namalizia kadigrii kangu siku moja jumamosi saa kumi na mbili hiv asubuhi nilipigiwa simu na watu walijitambulisha kuwa ni ma ofisa kutoka "UTUMISHI" hivyo napaswa kuamka na kwenda chuo ntawakuta wakiwa hapo kwenye bwalo kubwa la mitihani na mikutano ya chuo sikujua wapi wametoa namba zangu maana nilipigiwa kwenye line ya voda ambayo huwa siitumii mara kwa mara na line yangu iliyozoeleka ya tigo niliizima. Mnyamwezi nikajisemea ukisikia "zali la mentali ndo hili" mwezi mmoja kabla ya final exams naitwa interview na serikali?

Nilipofika chuoni nilikuta wajomba wapo na wanafunzi wa kozi zingine kibao, mara nikaona na washikaji zangu sana wawili ambao nilikua nasoma na kuishi nao mtaani wapo. Nikiri kuwa ile interview ilikua ya ajabu ina maswali karibu kitabu cha kurasa 100... nilijiuliza hii ni interview ya namna gani?

Baada ya kumaliza chuo niliamua kubaki town kutafuta life nilijua mkoani kisingekua na fursa za ajira kama hapa town.... huu ndo wakati uliokuwa mgumu kwanuki boom lilikua limekata na mtaani palikua pamoto sana... ilikua kila ikifika jion nakaa kibalazani napiga story na masela niliosoma nao na tukaamua kubaki town kukomaa, miezi 9 ilikua imepita baada ya chuo kuisha, ikumbukwe kuwa katika masela sita tuliokua tunashinda kijiweni jioni wanne tulishiriki kwenye ile interview ya mwez wa sita kabla hatujamaliza chuo.

Kwa wakati ule kijiwe kilikua kinachangamka vibaya mno, tukaanza kupokea wageni tusiowajua ambao baadaye walikuja kuwa washkaji zetu sana kariba ya watu hawa haikutofautiana kabisa na jamaa yule wa miaka ya 2008 niliyowaambia mwanzoni kabisa mwa story hii, walikua washikaji wawili wapole sana, watanashati na wanaonekana kuwa na akili nyingi sana. Maswali yao na hoja zao zililenga kupata ufahamu wetu juu ya masula mbali mbali hasa ya kisiasa na kiuchumi ila hasa mitizamo yetu ya kisiasa.

Nilishindwa kuhisi chochote maana walijitambulisha kuwa wao ni wanafunzi waliohitimu chuo kama sisi ila wao walimaliza Mzumbe university morogoro. Kumbe walikua kazini bwana na kazi yao ilikua ni kuangalia mienendo yetu kabla ya kuitwa rasmi kitengoni wao wanaita "vetting " na hapa palikua pamoto maaana tulinza kuhisi kuchunguzwa kupita kiasi kila nikiamka mara aunt yangu wa mbeya anauliza "kuna watu wananipigia simu kuniuliza kuhusu wewe uliwapa namba yangu?" Kesho yake jamaa yangu niliyesoma nae shule ya msingi darasa la kwanza 1999 hadi darasa la saba 2005 nae anaulizwa ulizwa kuhusu mimi...nikiwauliza washikaji zangu nao ni hivyo hivyo.... hapo tukajua fika kua tulikua chini ya uangalizi wa kitengo....
TUTAENDELEA
imaginative
 
Nimeishi na kufanya kazi na watu wa kitengo, but hakuna mwanakitengo mpumbavu wa kuacha laptop ikiwa log in kwenye e mail afu mlango wazi.

Kuna kitengo mmoja nilikutana nae Mbeya, alikua na simu NNE. Mbili za kazi ambazo hazitoki chumbani kwake, mbili za matumizi binafsi.

Alikua very social na anagonga mtungi hatari but huwezi kuingia chumbani kwake hata alewe mpaka kuzima.

Mkuu kawadanganye wapiga debe
 
Hawezi kuwa hata karibu nna mwana usalama huyu! Wakati 'ule'mlipokuwa kijiweni akiwauliza maswali kadhaa kuhusu nyie aliwezaje kuji cover kuto expose back ground yake ikiwa hapa tu hakuna aliyemuuliza hata swali moja lakini yeye katiririka tu bila hata nukta wala koma? Jasusi anafundishwa namna ya kuji cover dhidi ya jasusi mwingine,na jasusi mwingine kwa mujibu wa ethics za kijasusi ni mtu YEYOTE hadi Kitu CHOCHOTE! Hiyo loophole ya wewe tu kumtambua jasusi ina mdisqualify huyo kuwa hafai kuwa jasusi! Jasusi gani huyo anayempigia Shangazi yako simu na kumuuliza habari zako wakati ana uwezo wa kuku track 24/7 kwa almost nyendo zako zote?maana hata kwenye kuulizia tu njia ya kuelekea sehemu fulani kuna namna ya kuuliza ambayo haitamwacha muulizwaji na shaka,hakuna jasusi who is so unethical to the point of binding himself to the blue chain like that! Yaani unampigia simu Shangazi yake,shangazi anampigia mjomba,mjomba anampigia dada yake ambaye ndiye mama yako kuwa kuna watu wanaulizia ABC zako,naye anampigia baba yako kumweleza,baba yako anatafuta hiyo namba ya huyo mpigaji aongee naye!hapo unakuta baba naye ni jasusi wa upande mwingine,unadhani atafanyaje? Anakutengenezea trojan horse! Balaa!
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
Avatar tu inaonyesha

Ntakuweka kitengo cha ...

Hawa watu wapo mkuu

Mimi niliwakwepa kinoma ...
Haikua dream yangu kufanya kazi huko ingawa nna uchungu sana na nchi yangu

Watu wote walio karibu yangu ..
Ni watu wa huko
.walitaka waniifluence hadi shule ya kusom a

Looh .. Nikaona upumbav niende kutetea maccm yabak madarakan

... Mbinu nlizotumia siri yangu ...
.ila aaahahaha aisee

Mmoja nkamwambia labda .. TFDA ..
 
Avatar tu inaonyesha

Ntakuweka kitengo cha ...

Hawa watu wapo mkuu

Mimi niliwakwepa kinoma ...
Haikua dream yangu kufanya kazi huko ingawa nna uchungu sana na nchi yangu

Watu wote walio karibu yangu ..
Ni watu wa huko
.walitaka waniifluence hadi shule ya kusom a

Looh .. Nikaona upumbav niende kutetea maccm yabak madarakan

... Mbinu nlizotumia siri yangu ...
.ila aaahahaha aisee

Mmoja nkamwambia labda .. TFDA ..
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Kama ni TFDA mkuu na mimi napamind sana, usinisahau aisee ukipata dili
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Kama ni TFDA mkuu na mimi napamind sana, usinisahau aisee ukipata dili
Ilikua zaman nikiwa form five

Nshapotezea ...

Tanzania dah ...

Pambanen wakuu ...

Mimi ngoja ntafute maarifa zaidi

Nivunje rekodi ya yule jamaa aliyechukua phd ana miaka 30
 
Usiendelee unifichua siri za nchi unaifanya kazi ya hao jamaa kuwa ngumu iwapo unatoa siri jinsi wanavyofanya kazi.
Hakuna siri yoyote hapo mbona kawaida tu na mimi siku moja nitakuja kuelezea safari yangu kutoka skauti,jkt mpaka RTS
 
Ilikua zaman nikiwa form five

Nshapotezea ...

Tanzania dah ...

Pambanen wakuu ...

Mimi ngoja ntafute maarifa zaidi

Nivunje rekodi ya yule jamaa aliyechukua phd ana miaka 30
Poa poa mkuu.

Kulingana na masomo aliyosoma kupata PhD kwa umri huo inawezekana.

Huwezi kulinganisha na mtu aliyesoma MD au Pharmacy.

Mtu akianza MD akiwa na miaka(mathalani) 21, 5yrs(Bachelor), 1yr(Intern), 3yrs(Masters), 4yrs(PhD).

Jumla 21 +5 +1 +3+ 4=34yrs

Ni nadra sana kwa mtu anayesoma kozi za afya(science) kupata PhD akia na miaka 30.
 
Back
Top Bottom