Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,279
Wanawake huwa wanawajaribu wanaume kwa majaribu fulani ili waweze kujua kama wanaume hao wanafaa kuishi nao, bila ya kupima au kufanyia utafiti kama hayo majaribu wanayoyatumia kama yapo ndani ya uwezo wa wanaume husika wanaojaribiwa,
Hasara za kufanya hivi kwanza ni vigumu wewe mwanamke kugundua kama unadanganywa au lah! kwa sababu ni vigumu kujua uhalisia wa maisha ya mwanaume unayemjaribu.
Pia inaweza kupelekea ukawapoteza watu muhimu katika maisha maisha yako kwa sababu huwezi kutumia vigezo vinavyofanana kwa watu tofauti ambao wana maisha tofauti. Mfano swala la no sex before marriage si kila mwanaume anaweza kulikubali hivyo ni vibaya kutumia kigezo hicho kuwapima wanaume wawili au watatu tofauti na kuamini kwamba anayevumilia ndiye anayekufaa.
Pia kuna mwanamke anamjaribu mchumba wake labda amnunulie kitu fulani cha gharama lakini mwanaume kwa wakati huo anakuta ana majukumu mengine kama kujenga. Endapo mwanaume akishindwa kutimiza anaonekana hafai na kukimbilia kwa mwingine ambae anaweza kumpa hivyo vitu vya starehe ya muda na kumuacha mwanaume potential ambaye labda angevumilia wangefanya maisha pamoja....
Nawasilisha and nafungua milango ya kukosolewa na kuwa na mawazo tofauti na yangu ila milango ya matusi imefungwa..........
Hasara za kufanya hivi kwanza ni vigumu wewe mwanamke kugundua kama unadanganywa au lah! kwa sababu ni vigumu kujua uhalisia wa maisha ya mwanaume unayemjaribu.
Pia inaweza kupelekea ukawapoteza watu muhimu katika maisha maisha yako kwa sababu huwezi kutumia vigezo vinavyofanana kwa watu tofauti ambao wana maisha tofauti. Mfano swala la no sex before marriage si kila mwanaume anaweza kulikubali hivyo ni vibaya kutumia kigezo hicho kuwapima wanaume wawili au watatu tofauti na kuamini kwamba anayevumilia ndiye anayekufaa.
Pia kuna mwanamke anamjaribu mchumba wake labda amnunulie kitu fulani cha gharama lakini mwanaume kwa wakati huo anakuta ana majukumu mengine kama kujenga. Endapo mwanaume akishindwa kutimiza anaonekana hafai na kukimbilia kwa mwingine ambae anaweza kumpa hivyo vitu vya starehe ya muda na kumuacha mwanaume potential ambaye labda angevumilia wangefanya maisha pamoja....
Nawasilisha and nafungua milango ya kukosolewa na kuwa na mawazo tofauti na yangu ila milango ya matusi imefungwa..........