Majaribu mazito kwa mke wa mtu....msaada jamani!

Majaribu mazito kwa mke wa mtu....msaada jamani!

Nyleptha

Member
Joined
Jun 19, 2012
Posts
69
Reaction score
47
Amekuja kwangu akiwa na sura ya huzuni na majonzi tele, nikajua ana tatizo kubwa, nikaketi kumsikiliza habari aliyojia;

Ni mwanamke ameolewa miaka michache iliyopita yaani ndoa yao bado changa tu, ameajiriwa katika kampuni fulani binafsi wanamlipa mshahara wa kutosha kubadili mboga, mumewe alipata uhamisho kwenda mkoani kikazi kama mwaka tu umepita, wakapiga mahesabu wana miradi na wamejenga nyumba yao hapa, kipato chao ni cha kawaida tu hivyo wakaona mke aendelee na kazi hapa hapa ila mume ndio aende mkoani kusaka maisha halafu mume akipata nafasi atakuwa anakuja na mke anaweza kwenda pia.

Baada ya mume kuondoka mke ameendelea na maisha kama kawaida, ila TATIZO limeanzia pale ambapo rafiki yangu huyu amejikuta anavutiwa sana na mwanaume mmoja ambaye anakaa maneneo ya karibu na nyumbani kwake na mara kadhaa amekuwa akimkuta njiani na kumpa lifti na kuongea mawili matatu ya maisha. Kadiri siku zinavyokwenda anazidi kumpenda mwanaume huyu ambaye pia ni mume wa mtu! Hajui afanyeje kuepuka hali hii kwani ni mtu ambaye familia zao zimeshazoeana si rahisi kukatisha mahusiano ghafla kutaleta maswali sana, hawezi kuhama mtaa wala kubadili njia ni hiyohiyo moja, na wakati mwingine usafiri ni wa shida balaa inabidi tu akubali hiyo lifti. Huyo mwanaume hajaonyesha dalili yoyote ya kumzimikia rafiki yangu huyu wala kumtongoza, ni mdada tu ndio amempenda/tamani)!

Nimemshauri akae mbali na huyo jamaa na pia ajitahidi kwenda kumuona mumewe au amwambie mumewe aje haraka kuokoa jahazi, hayo yote ni majaribu tu kwa kuwa hajamuona mumewe siku nyingi! dada wa watu anasema hafikirii kumsaliti mumewe hata siku moja kwahiyo ndio anatafuta jinsi ya kukimbia jaribu hilo, anatamani apate wasaa amwambie ukweli, kitu ambacho naona si sahihi kwani anaweza akadraw attention ya huyo jamaa na kumfanya nae amuwazie kimapenzi na matokeo yake anaweza kumuweka katika majaribu zaidi wakafanya usaliti ktk ndoa zao.

Nimetoa ushauri kwa wengi lakini hili nimepungukiwa nondo, niongezeeni maoni yenu wadau! nimsaidieje huyu dada?

Ila ujumbe nilioupata hapa ni kwamba tusiache wake zetu mbali, sijui iwe ni kwa sababu gani lakini tufikirie marambili, pia kama mke yuko ktk hali hii je mumewe huko yuko ktk hali gani? anayashindaje majaribu? nimejiuliza sana.
 
Amekuja kwangu akiwa na sura ya huzuni na majonzi tele, nikajua ana tatizo kubwa, nikaketi kumsikiliza habari aliyojia;

Ni mwanamke ameolewa miaka michache iliyopita yaani ndoa yao bado changa tu, ameajiriwa katika kampuni fulani binafsi wanamlipa mshahara wa kutosha kubadili mboga, mumewe alipata uhamisho kwenda mkoani kikazi kama mwaka tu umepita, wakapiga mahesabu wana miradi na wamejenga nyumba yao hapa, kipato chao ni cha kawaida tu hivyo wakaona mke aendelee na kazi hapa hapa ila mume ndio aende mkoani kusaka maisha halafu mume akipata nafasi atakuwa anakuja na mke anaweza kwenda pia.

Baada ya mume kuondoka mke ameendelea na maisha kama kawaida, ila TATIZO limeanzia pale ambapo rafiki yangu huyu amejikuta anavutiwa sana na mwanaume mmoja ambaye anakaa maneneo ya karibu na nyumbani kwake na mara kadhaa amekuwa akimkuta njiani na kumpa lifti na kuongea mawili matatu ya maisha. Kadiri siku zinavyokwenda anazidi kumpenda mwanaume huyu ambaye pia ni mume wa mtu! Hajui afanyeje kuepuka hali hii kwani ni mtu ambaye familia zao zimeshazoeana si rahisi kukatisha mahusiano ghafla kutaleta maswali sana, hawezi kuhama mtaa wala kubadili njia ni hiyohiyo moja, na wakati mwingine usafiri ni wa shida balaa inabidi tu akubali hiyo lifti. Huyo mwanaume hajaonyesha dalili yoyote ya kumzimikia rafiki yangu huyu wala kumtongoza, ni mdada tu ndio amempenda/tamani)!

Nimemshauri akae mbali na huyo jamaa na pia ajitahidi kwenda kumuona mumewe au amwambie mumewe aje haraka kuokoa jahazi, hayo yote ni majaribu tu kwa kuwa hajamuona mumewe siku nyingi! dada wa watu anasem haafikirii kumsaliti mumewe hata siku moja kwahiyo ndio anatafuta jinsi ya kukimbia jaribu hilo, anatamani apate wasaa amwambie ukweli, kitu ambacho naona si sahihi kwani anaweza akadraw attention ya huyo jamaa na kumfanya nae amuwazie kimapenzi na matokeo yake anaweza kumuweka katika majaribu zaidi wakafanya usaliti ktk ndoa zao.

Nimetoa ushauri kwa wengi lakini hili nimepungukiwa nondo, niongezeeni maoni yenu wadau! nimsaidieje huyu dada?

NB: hili janga halinihusu mimi, tafadhali.

Shida yangu ni kwenye hizo bold inanipa shida umeolewa halafu unaanza kumtamani mme wa mwenzio? acha tamaa dada kama unahitaji mkate wa uzima mpigie simu mmeo mwambie kuna EMERGENCY ARUDI HARAKA NYUMBANI,acha kudandia magari ya watu na kutamani vya wenzio.

kumbuka ukimsaliti mwenzio unaweza kumbana na haya ukapata mimba wakati mmeo hayupo!,ukapata magonjwa kama UKIMWI,itakutesa kwenye ndoa yako ukienda huko ukafanyiwa kitu mmeo hajawahi kukufanyia na upendo utaisha kwa mmeo,na huenda ukaendeleza huo mchezo.

"Ikimbieni zinaa"na mmeo akijua ulimsaliti ndipo atakutosa hapo kilio na kusaga meno utakuwa mgeni wa nani?
 
kuna mambo mengine hata kuyaombea ushauri yanakua kama upuuzi lrani

mara nyinigi type hii unakuta keshamegwa

akili ipo kichwani, lakini unamba ya mwenzako ati akushauri

:crazy::crazy:
 
Shida yangu ni kwenye hizo bold inanipa shida umeolewa halafu unaanza kumtamani mme wa mwenzio? acha tamaa dada kama unahitaji mkate wa uzima mpigie simu mmeo mwambie kuna EMERGENCY ARUDI HARAKA NYUMBANI,acha kudandia magari ya watu na kutamani vya wenzio.

kumbuka ukimsaliti mwenzio unaweza kumbana na haya ukapata mimba wakati mmeo hayupo!,ukapata magonjwa kama UKIMWI,itakutesa kwenye ndoa yako ukienda huko ukafanyiwa kitu mmeo hajawahi kukufanyia na upendo utaisha kwa mmeo,na huenda ukaendeleza huo mchezo.

"Ikimbieni zinaa"na mmeo akijua ulimsaliti ndipo atakutosa hapo kilio na kusaga meno utakuwa mgeni wa nani?

Asante mdau, ukisoma kwenye mada huo ndio ushauri ambao hata mimi nimempa, mumewe aje au yeye aende kwa mumewe haraka. naomba kama una mawazo zaidi jinsi ya kumsaidia kumuepuka huyu amtiaye majaribuni.
 
well if u want to short circuit ur marriage live in different cities!!! mfano hai huo hapo jamani. kwa wale mnataka kuoa mambo ya kuishi mikoa mbali mbali sio ndoa bali kujidanganya.
 
mmmmh jamani kama hafikirii kumsaliti mumewe mbona ni simple sana kumpotezea huyo mtu?!loh hivi mke wa mtu na akili zako mpaka ukaombe ushauri kwenye issue kama hii jamani?really?!hayuko serious asee

Mitaani majaribu ni mengi sana na huwezi kujua utakutana nayo wapi na kwa jinsi gani. labda kosa liwe langu kuleta hii mada hapa, ila nimemshauri accordingly. lengo ni kuwafikishia ujumbe pia wengine wenye mtanziko kama huo, pia kuomba ushauri si vibaya inategemea tu unamuomba nani, amekuja kwangu kama msimamizi wake wa ndoa hivyo ni msiri wake pia, akitarajia nimpe mwongozo mzuri sio kumpoteza.
 
mmmmh jamani kama hafikirii kumsaliti mumewe mbona ni simple sana kumpotezea huyo mtu?!loh hivi mke wa mtu na akili zako mpaka ukaombe ushauri kwenye issue kama hii jamani?really?!hayuko serious asee

it is loniless that makes the booze and infedility all the more alluring
 
Bila kupepesa macho wala usimung'unye maneno mwambie rafiki yako Umalaya sio mzuri.
 
well if u want to short circuit ur marriage live in different cities!!! mfano hai huo hapo jamani. kwa wale mnataka kuoa mambo ya kuishi mikoa mbali mbali sio ndoa bali kujidanganya.

Nakuunga mkono, ndoa ni wawili pamoja. Tujitahidi kuzilinda ndoa zetu kwa kila hali, kama ni kazi tutafakari uzito wake kama unazidi umuhimu wa ndoa.
 
Asante mdau, ukisoma kwenye mada huo ndio ushauri ambao hata mimi nimempa, mumewe aje au yeye aende kwa mumewe haraka. naomba kama una mawazo zaidi jinsi ya kumsaidia kumuepuka huyu amtiaye majaribuni.

Hili swala lingekuwa rahisi sana kusolve kama mkaka ndio angekua amemtamani huyu mdada. Lakini kwa jinsi ninavyowajua wadada wakishataka kitu, huu ushauri wetu ni kazi bure tuu. Huyu mdada lazma atamegwa tu. Sanasana labda ataanza kuufanyia kazi huu ushauri baada ya kumegwa mara kadhaa (kama bado).
 
Huyo anawashwa na mumewe asiporudi haraka anaweza kumegwa dakika yoyote ile,hakuna cha kumshauri zaidi ya kwenda kwa mumewe apate tiba ya tamaa za kimahaba.
 
Nakuunga mkono, ndoa ni wawili pamoja. Tujitahidi kuzilinda ndoa zetu kwa kila hali, kama ni kazi tutafakari uzito wake kama unazidi umuhimu wa ndoa.

ndio maana mie nasema kuna wanawake wa aina mbili; those who want to be wives and those who get married becoz thats wat is expected of them from society. marry the former. maana huyo ndio anajua umuhimu wa ndoa.
pia lazima katika uchumba mambo kama hayo mzungumze...nani ataacha kazi ikiwa mume au mke kapata kazi sehemu nyingine usiseme oh tutajuaga mbele ya safari
 
ndio maana mie nasema kuna wanawake wa aina mbili; those who want to be wives and those who get married becoz thats wat is expected of them from society. marry the former. maana huyo ndio anajua umuhimu wa ndoa.
pia lazima katika uchumba mambo kama hayo mzungumze...nani ataacha kazi ikiwa mume au mke kapata kazi sehemu nyingine usiseme oh tutajuaga mbele ya safari

Umeongea point nzuri sana.:high5:
 
huyo ni pepo anaanza,kama yalivyo maumivu ya kichwa!huanza polepole,bora ahame akiishi kwa shida na kipato cha kawaida cha mmewe,kuliko haka kamchezo anakotaka kuanzisha!!mwambie safari moja huanzisha safari nyingine,hataishia hapo!
 
Keshamegwa huyo,anataka umuunge mkono tu. Wewe jaribu kumwambia agegedwe na huyo jamaa uone atakavyokujibu baada ya siku kadhaa
 
Keshamegwa huyo,anataka umuunge mkono tu. Wewe jaribu kumwambia agegedwe na huyo jamaa uone atakavyokujibu baada ya siku kadhaa

Hapana mdau, hapo mimi sikubaliani nawe, ndoa niliyoisimamia ikifungwa siko tayari kuiona ikivunjika wakati nimepewa nafasi ya kuiokoa! Nimempa ushauri mzuri halafu uamuzi ni wake, kusuka au kunyoa, akiamua mwenyewe kuvunja ndoa yake basi mikono yetu sote ni misafi kwa kutoshiriki kumuangusha dhambini.
 
Back
Top Bottom