Majanga ya kiasili kwa kiasi kikubwa husaidia kudhibiti ongezeko letu sisi wanadamu

Majanga ya kiasili kwa kiasi kikubwa husaidia kudhibiti ongezeko letu sisi wanadamu

mcTobby

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2018
Posts
6,498
Reaction score
18,159
Haya majanga ya kiasili kama maporomoko ya ardhi, matetemeko ya ardhi ,tsunami pamoja na vimbunga vya msimu kwa kiasi kikubwa huangamiza idadi kubwa ya watu..

Sisi tutaendelea kujifariji na kuzaana KAMA BAKTERIA kwamba kila mtoto anakuja na sahani yake, lakini tukumbuke Asili nayo hutukumbusha kwamba sisi ni wanadamu tu. Kila uchwao tafiti nyingi hufanyika ili kujikinga na majanga ya asili lakini wapi.

Japan huko wanataka kujenga ukuta mkubwa kuzunguka baadhi ya visiwa vyake ili kujikinga na janga la Tsunami, lakini hili sio suluhisho la ku battle na Nature. Yote haya tunayafanya tukiamini tutazaana tu na mambo yataenda kama tunavyotaka..

Tukumbuke Rasilimali ni chache hivyo lazima tupunguzwe na Asili ili kuwe na usawaziko wa kiasili(Balance of nature) . Ni kweli inauma na kuhuzunisha tukiona wanadamu wenzetu maelfu kwa maelfu wanakufa kwa majanga lakini tutafanyaje sasa Pale asili inapoamua kufanya kazi yake ya asili?
 
vipi kuhusu majanga ambayo sio ya kiasili?
mfn,magonjwa COVID-19,vita...nk
 
Ingekuwa ni hvy bc kila nchi duniani zingekumbwa na hayo majanga
 
Kuzuia nature isifanye kazi haiwezekani.. Ila Japan itapunguza athari zaidi
 
Leo nilikuwa natazama Worldometer.

Population/idadi ya Watu Duniani 8.2billion.

TANZANIA million 70.
Nafasi ya 21 Duniani.

Walau "binadamu" wa sasa tumejitahidi na kuendelea Kuyatambua na kuyaelewa maumbile/nature, Kwa manufaa ya uhai wetu. Ingawa Bado safari inaendelea.
 
Back
Top Bottom