Herbalist Dr MziziMkavu
Platinum Member
- Feb 3, 2009
- 43,077
- 34,848
WATU watano, wameuawa kwa kupigwa risasi baada ya gari walilokuwa wamepanda kutekwa na kundi la majambazi katika kijiji cha Sunya, Kata ya Sunya Wilaya ya Kiteto, mkoani Manyara.
Majambazi hao waliokuwa zaidi ya matano, walifanikiwa kupora mamilioni ya fedha kutoka kwa watu waliokuwa katika gari hilo ambao wengi wao ni wafanyabiashara wa mitumba na mifugo wilayani Kiteto.
Tukio hilo la aina yake lilitokea juzi majira ya saa 1:30 jioni, baada ya majambazi hao waliokuwa na silaha za moto na za jadi, kufunga barabara kwa majabali na kuteka gari hilo lililokuwa na wafanyabiashara waliokuwa wanaelekea katika mnada kijiji cha Mutura.
Kamanda wa polisi mkoani Manyara, ACP Parmena Sumari alithibitisha jana kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa kikosi cha askari tangu juzi usiku kilitumwa kufuatilia tukio hilo.
"Ni kweli majambazi yalivamia hilo gari na yameuawa watu watano, wanawake wawili, wanaume wawili na mtoto mmoja na bado tunafuatilia juu ya majina yao na namba za gari, "alisema Sumari.
Kamanda Sumari alisema katika tukio hilo watu wengine watano walijeruhiwa kwa risasi na hadi jana walikuwa wamelazwa katika kituo cha afya cha Sunya wilayani Kiteto.
Kamanda huyo, ambaye alieleza yupo safarini, alisema hadi jana mchana bado alikuwa hajapata taarifa kamili na aliwataka waandishi wa habari hizi kuwasiliana na msaidizi wake ambaye hata hivyo naye alisema bado hana taarifa kamili.
Mkuu wa wilaya ya Kiteto, Frank Uhaula alithibitisha jana kutokea mauaji hayo katika wilaya yake na kueleza kuwa uchunguzi na msako wa watuhumiwa wa tukio unaendelea.
Afisa Mtendaji wa kata ya Sunya, Charles Adola alisema kuwa hadi jana mchana walikuwa bado wakiendelea na msako na bado utambuzi wa waliouawa ulikuwa unaendelea.
Adola alisema kabla ya majambazi hayo hayajaua, yalipiga risasi kadhaa hewani kulazimisha gari kusimama na liliposimama, waliwauawa watu hao na kuwajeruhi wengine huku na kupora fedha na mali nyingine.
Tukio hili ni mfululizo wa matukio ya ujambazi ambayo yameanza kuibuka tena katika maeneo mbali mbali hapa nchini.Majambazi yaua watano Manyara