Majaji wa TMT 2015 hawana sifa za nafasi hizo

Majaji wa TMT 2015 hawana sifa za nafasi hizo

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,255
Reaction score
8,027
Mimi sijaelewa hizi nafasi hua zinapatikanaje! Ili mtu aqualify kua jaji TMT anatakiwa kuwa na vigezo gani? Au tu kwa sababu mtu ni migizaji ndiyo kigezo? Hapa ndo mtu unajua kua ni kupeana tu kwa sababu ya kujuana.

Haiwezekani unamfanyia mtu interview hujaongea nae chochote unamwambia eti "tuonane mwakani "Kwanini? Nini maana ya kuwa haji? Kwanini umkatishe mtu tamaa mapema hata bado hujafahamu anachoenda kukifanya?

Watu hubadilika siku hadi siku, Kwani jaji usiwe counselor, mentor, educator, emphasizer? Badala ya kumtia mtu matumaini Unapata wapi ujasiri wa kumwambia mtu tuonane mwakani? We ni Mungu? Kwani wewe hizo pesa umetoa mfukoni kwako?

Huyu bwana anayeitwa Roy Sarungi hafai kua jaji hata kidogo yupo kupiga pesa tu. Taifa linahitaji vijana wenye weledi wa kuigiza ili wapate ajira kukimu maisha ya familia zao lakini wakwamishaji ndio Hawa!

Hapa ndio tunaamini kuna Inawezekana kabisa Hawa watu wana watu wao mifukoni.

Tabia mbaya sana hii, Kwa season ijayo waangaliwe watu walio na vigezo vya kua majaji na sio wababaishaji.
 
Ynaa

Tafadhali me sio candidate! Ila wanavyowafanyia hawa madogo hakikubaliki.
 
Last edited by a moderator:
Karibia majaji wa mashindano mengi ya kutafuta vipaji lazima kati yao kuwe na mwehu mmoja,Kama salma jabir bss ya bongo,Kate wa nigerian got talent na yule Simon wa Britain's got talent
 
Ynaa

Tafadhali me sio candidate! Ila wanavyowafanyia hawa madogo hakikubaliki.
Naungana nawe asilimia 100. majaji wanajiona kama Miungu, hawana hata huruma au kujali hisia za vijana hawa! Vijana wanatafuta ajira tusiwakatisha tamaa. Inawezekana kuwaeleza wameshinda baada ya kuperform hata kwa muda mfupi na kutumia maneno yasiyokatisha tamaa.
 
Huyo uliyemtaja kwamba hajui kulea vipaji, si ajabu ameambukizwa tabia ya Ian Mbugua, jaji wa TPF season zote.Lakini wengi hawajui kwamba Ian ni muigizaji mzuri mwenye sifa nyingi Kenya.Anayoyafanya kwenye episodes za tpf ni uigizaji na watazamaji hufurahishwa nae sana.Ole anayeiga swaga za Ian!
 
niukweli kabisa wale majaji wooote ni vilaza hamunamo kitu yan bogasssi kabisa yambafuu
 
Wait... unakuta kwenye audtion husika nje kuna watu kama 500 hivi wanasubiri kuingia ndani! Wewe unapata nafasi ya kuingia, ile kutokea tu, upo very nervous; unaogopa camera inayoangaza ukumbi mzima!!! Itakuaje siku utakapokutana na camera inayoku-face wewe peke yako?!

Yaani unatarajia hapo watu waanze kukumbia, "hey, relax... don't worry, we're here for you!" Utapata wapi huo muda wakati nje kuna mamia ya watu wanasubiri kuingia? Watu wengi wanapenda kuigiza lakini kuigiza sio kazi ndogo kama wengi tunavyofikiri na ndio maana unashauriwa kabla hujaenda kwenye audition ya aina hiyo, fanya maandalizi...

fanya practice ya kujichetua chetua hata mbele ya wenzako baada ya kuwa tayari umeshahitimu kujichetua mbele ya kioo ukiwa peke yako coz' hujui utaambiwa ufanye nini! Unakuta mtu mwingine hata ile kujitamblisha tu kwake inakuwa taabu... atajing'atang'ata hapo hadi umbadilishie topic!
 
Sijaona hoja yeyote pale...mimi uzuri nafatilia kile kipindi...wako fair kabisa sema watu mnapendwa kubebwa bebwa na kubembelezwa.

Yani Million 50 mnataka mtu apewe kwa kubembelezwa? Watu tatizo hawako serious ..kila mtu ana angalia kabisa kuna watu hawako serious na hawajui na ndio maana wanatemwa....wanao jua wanasonga.

Watanzania ni mabingwa wa kulalamika.

Mara tunzo za watu haziko fair..
Mara KTMA hawako fair.....
Mara TMT hawako fair.....
Mara Bongo star search hawako fair...
Hakika watanzania ni mabingwa wa kulalamika kila kitu ...
 
Wait... unakuta kwenye audtion husika nje kuna watu kama 500 hivi wanasubiri kuingia ndani! Wewe unapata nafasi ya kuingia, ile kutokea tu, upo very nervous; unaogopa camera inayoangaza ukumbi mzima!!! Itakuaje siku utakapokutana na camera inayoku-face wewe peke yako?! Yaani unatarajia hapo watu waanze kukumbia, "hey, relax... don't worry, we're here for you!"

Utapata wapi huo muda wakati nje kuna mamia ya watu wanasubiri kuingia? Watu wengi wanapenda kuigiza lakini kuigiza sio kazi ndogo kama wengi tunavyofikiri na ndio maana unashauriwa kabla hujaenda kwenye audition ya aina hiyo, fanya maandalizi...

fanya practice ya kujichetua chetua hata mbele ya wenzako baada ya kuwa tayari umeshahitimu kujichetua mbele ya kioo ukiwa peke yako coz' hujui utaambiwa ufanye nini! Unakuta mtu mwingine hata ile kujitamblisha tu kwake inakuwa taabu... atajing'atang'ata hapo hadi umbadilishie topic!

Watu wanapendwa kubebwa bebwa na kubembelezana
 
Watu wanapendwa kubebwa bebwa na kubembelezana
Umeona enh! Tunapenda kubebwa bebwa wakati hata inapotokea mtu akaamua kutubeba, aghalabu huwa tunaingia kwenye mbeleko tukiwa na nyembe zetu mkononi!!! TZS 50 million sio pesa ndogo hata kidogo... pesa ambayo wengine hadi tutaingia kaburini hatutakuja kuishika mkononi halafu mtu anaenda kujaribu!!!

The only thing am disappointed ni kwamba nilikuwa na matarajio makubwa sana na Proin coz' kwa ninavyomjua Lukaza nilikuwa na imani kubwa kwamba angeleta mabadiliko makubwa sana kwenye movie industry! Unfortunately, inaelekea hakupata washauri wazuri wa kumwambia ni nini hasa tunakosa kwenye tasnia yetu! Kosa alilofanya Lukaza chini ya Proin ni sawa na kosa lililofanywa na Bakhresa na Azam FC yake! Mbaya zaidi, sijui hata kama Lukaza mwenyewe anafahamu, ile timu yake imeshaanza kuingiza unprofessional kwenye kazi... sometime you need to know somebody inside!
 
Ma-judge inabidi wawe firm ili wapate watu wanaojua kuigiza kweli na sio wauza sura. Ila pia ni muhimu wawe na namna ya kuwatolea watu nje, sio lazima um-crush mtu kama kokoto kumjuza kwamba bado anahitaji mazoezi zaidi.

Mie binafsi niliboreka zaidi na yule mtangazaji wa kiume, anajitahidi kulazimisha kuchekesha ila hachekeshi chochote. Awe kawaida tu, asilazimishe fani. Au kama vipi amrudishie Joti mic yake.
 
Sijaona hoja yeyote pale...mimi uzuri nafatilia kile kipindi...wako fair kabisa sema watu mnapendwa kubebwa bebwa na kubembelezwa.

Yani Million 50 mnataka mtu apewe kwa kubembelezwa? Watu tatizo hawako serious ..kila mtu ana angalia kabisa kuna watu hawako serious na hawajui na ndio maana wanatemwa....wanao jua wanasonga.

Watanzania ni mabingwa wa kulalamika.

Mara tunzo za watu haziko fair..
Mara KTMA hawako fair.....
Mara TMT hawako fair.....
Mara Bongo star search hawako fair...
Hakika watanzania ni mabingwa wa kulalamika kila kitu ...

Mkuu, naomba nikusahihishe kidogo.. Sio Tunzo, ni Tuzo! Naona ni kosa unalolirudia mara kwa mara, hivyo si mbaya tukiwekana sawa.. We're brothers!

Kuhusu hili suala, nadhani Watanzania bado tunakosa kitu kimoja tu cha msingi; Seriousness.. Yaani kwenye masuala mengi tunapwaya kwa sababu hatuko serious, hakuna jingine.

Ukitazama washiriki, hawako serious; Waandaaji nao, hawako serious, Majaji pia hawako serious, Mambo yanaenda enda tu. Ndio maana kila linaloanzishwa huwa halidumu na halileti matokeo chanya..

Sina haja ya kuwa specific coz this applies to everything we touch!
 
Huyo uliyemtaja kwamba hajui kulea vipaji, si ajabu ameambukizwa tabia ya Ian Mbugua, jaji wa TPF season zote.Lakini wengi hawajui kwamba Ian ni muigizaji mzuri mwenye sifa nyingi Kenya.Anayoyafanya kwenye episodes za tpf ni uigizaji na watazamaji hufurahishwa nae sana.Ole anayeiga swaga za Ian!

Ian kiboko yake Hemed. Nikikumbuka alivyomchana siku ile huwa nacheka sana alimpa ukweli wake
 
Tatizo la Tanzania ni kupenda "njia mkato" na kutothamini "profession" mbalimbali.
Mwanamuziki ataandika nyimbo yake na kuingia studio bila ya kumtafuta mjuzi wa lugha kwa mfano ili ahariri mashairi yake,mwandishi wa filamu anaandika kisa kinachohusu haki na sheria lakini hatafuti wanasheria ili kupata maoni yao,na hawa jamaa wa TMT wameshindwa kupata mtu toka CASS ama TASUBI ambao wangewawekea miongozo ya kitaalamu!
 
Back
Top Bottom