Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Hivi majuzi nilihudhuria msiba wa jamaa yetu mmoja ambaye alikuwa amejitoa roho kwa kile alichodai kuwa maisha ni magumu. Kwamba pamoja na kuwa na Elimu nzuri lakini ameshindwa kupata ajira.
Siku hiyo nilikuwa na mgeni kutoka Uganda na niliambatana naye kule msibani. Wakati tunapiga soga, pale msibani, yuko bwana mmoja akasema kuwa marehemu hatazikwa kwa mujibu wa taratibu za kidini (Marehemu alikuwa ni Mkristo) kwa sababu amejiuwa na kwa mujibu wa dini hiyo ni dhambi hivyo hakuna kiongozi wa dini atakayeshiriki msiba ule.
Yule rafiki yangu kutoka Nchini Uganda akadakia, akasema kule kwao mtu akijiuwa maiti yake inacharazwa bakora hadharani kabla ya kuzikwa. Aliendelea kubaisha kwamba kule kwao kujitoa roho ni jambo lenye kufedhehesha sana na ndio maana ukawekwa huo utaratibu wa kucharaza maiti bakora ili kuwatisha watu wasijitoe roho.
Mimi huu utaratibu nimeupenda, maana utapunguza matukio ya watu kujitoa roho kwa kuhofia maiti zao kucharazwa bakora…………………
Siku hiyo nilikuwa na mgeni kutoka Uganda na niliambatana naye kule msibani. Wakati tunapiga soga, pale msibani, yuko bwana mmoja akasema kuwa marehemu hatazikwa kwa mujibu wa taratibu za kidini (Marehemu alikuwa ni Mkristo) kwa sababu amejiuwa na kwa mujibu wa dini hiyo ni dhambi hivyo hakuna kiongozi wa dini atakayeshiriki msiba ule.
Yule rafiki yangu kutoka Nchini Uganda akadakia, akasema kule kwao mtu akijiuwa maiti yake inacharazwa bakora hadharani kabla ya kuzikwa. Aliendelea kubaisha kwamba kule kwao kujitoa roho ni jambo lenye kufedhehesha sana na ndio maana ukawekwa huo utaratibu wa kucharaza maiti bakora ili kuwatisha watu wasijitoe roho.
Mimi huu utaratibu nimeupenda, maana utapunguza matukio ya watu kujitoa roho kwa kuhofia maiti zao kucharazwa bakora…………………