Maisha yananichanganya msaada tafadhali

Maisha yananichanganya msaada tafadhali

Unaweza kusoma na kufanya biashara at the same time. Biashara ni ngumu may be Mara 20 zaidi ya ugumu wa shule. We chamsingi anza biashara ndogondogo tu ata kwa mtaji mdogo hv utaelewa jinsi biashara ilivo. Anza na mtaji mdogo ukitumia ada utashindwa tu lazima maana ada ukiitumia vinginevyo ni LAANA
 
Mimi nakushauri usiache shule ndugu. Komaa mpaka umalize.

Ukimaliza masomo sasa unaweza kuamua kujiajiri huku ukiwa na vyeti vyako. Elimu ni muhimu sana kuliko unavyofikiri wewe sasa hivi.

Kuwa mvumilivu, heri wewe unatumiwa hata hiyo buku 10 kwa wiki. Kuna wenzako hawaioni hiyo buku 10 lakini wanakomaa na elimu hivyo hivyo kigumu gumu. "Life is not a bed of roses".
 
Success is waiting for the man who says yes to success.
Success is waiting for the man who plans for it. Who says i will go to school and he does.
Mkuu hapo piga kitabu kwanza kuongeza maarifa.
Knowledge muhimu maana huwa haipotei bure.
 
Ushauri nzuri sana
Ushauri wangu ni kama ufuatao, kwanza tambua hakuna uwekezaji mzuri kama elimu, hivyo hutakufa njaa kama umewekeza hapo. Elfu kumi kwa week ukipunguza matumizi itakusaidia umalize chuo. Fanya jambo moja asikudanganye mtu, ajira zipo za kutosha kama una cheti kizuri, usimkatishe tamaa anayekusaidia umri wako katika karne ya sasa unahitaji elimu kwanza angalau ufike degree alafu ndiyo ufanye biashara. Nimekushauri hivi maana una mawazo sawa na mdogo wangu ninayemsomesha.
Asante kaka mawazo yako mazuri, kitu kinachokatisha tamaa ni mtu kasoma ana vyeti vizuri but nothing to do na hana plan
Inaonyesha unapenda business na unamikakati ya unapotaka kufika.
Nakushauri anza biashara mara moja.

Usiogope kushindwa kwasababu hapa mwanzoni mambo yatakuwa magumu tu. Usirudi nyuma

Nilianza business tangu college. Sikuacha chuo lakini muda mwingi nilikuwa natumia kwenye mambo yangu zaidi....nilifahamu nini nataka kwenye maisha yangu. Nikishindwa ni mimi na nikifanikiwa ni mimi. Maneno ya watu/wazazi si chochote sana kwangu.

My advice for you is...have courage to follow your heart. It somehow already know what you want to become.

Failure is part of success in the business, take it as a lesson.

All the best
 
Soma tu mdogo wangu ukisha hitimu ndiyo anza biashara , usiache shule
 
Ni mawazo yangu ndo maana nimeomba ushauri sikwenda Direct kwenye implementation kuniita "zero brain "unakuwa hujanisaidia ndugu yangu Hakuna aliyekamilika inawezekana experience yangu ni ndogo katika Maisha nikilinganisha na wewe, ndo maana nimeomba ushauri naamini humu kuna watu wana upeo mkubwa zaidi yangu kuna njia wametumia kufikia mafanikio tofauti na kusoma hicho ndo nataka sio matusi mkuu
Huyo alie kuita ziro brain yeye ndio ziro brain Ndg ukitaka mafanikio lazma uwe na maamuzi magumu kiasi kwamba wengine wanaweza fikiria umepotea kumbe ndio unaelekea pazuri mwenye kuumia ni wew hao wengine wanao kulazimisha upite hivi hawajui maumivu unayo pata kikubwa mshilikishe Mungu akutangulie kwenye mafanikio yako maana hiyo pesa unayo somea ndio mtaji wako usitegemee ukimaliza kusoma wazaz watahangaika na wew wataangalia wadogo zako wataanza kukuambia jitegemeee maana tumesha kusomesha elimu ulio nayo inatosha kukufanya upate kaz kumbe mambo yalisha badilika
 
Kwanza kabla hujaacha shule watafute watu walioacha shule alafu uwaombe ushauri juu ya kuacha shule na uone watakuambia nn.
Pili kabla hujaanza biashara ya kuuza juisi ya miwa pamoja na mgahawa tafuta watu ambao wanafanya biashara ya miwa pamoja na mgahawa na wakafanikiwa kisha uombe ushauri kutoka kwao na uone watakuambia nn.
Tatu tafuta kitabu cha "RICHEST MAN IN BABYLON" ambacho kimeandikwa na Bwana George S Clason.nakushauri udownload pdf na audio yake pia alafu kisome kwa makini sana then baada ya hapo fanya maamuzi.
Huo ni uoga sasa unamfundisha mwenzio cha mhimu fanya maamuzi magum mambo ya kuulizia hayo ni mbwe mbwe tu sawa na kwenda kuomba ushauri kwa mtu alie oa mwanamke eti unaenda kuuliza mke wako ulimtongozaje ukamuoa kila mtu na vocal zake na inategemeana na mazingira
 
We kijana nakufahamu ngoja niambie wazazi wako wasikutumie iyo ada
 
Fanya biashara hiyo utatoka.wasomi mbona tunao huku mtaani wanatafuta kazi
 
Umeshamaliza form six hesabu unajua kutoa, kuzidisha na kujumlisha basi inatosha anza kutafuta hela sasa hivi una 21 ikifika 31 uko mbali
 
...kamata gamba kwanza
..huku ukiusoma mchezo;
.....umri bado unaruhusu!
 
Ushauri wangu ni kama ufuatao, kwanza tambua hakuna uwekezaji mzuri kama elimu, hivyo hutakufa njaa kama umewekeza hapo. Elfu kumi kwa week ukipunguza matumizi itakusaidia umalize chuo. Fanya jambo moja asikudanganye mtu, ajira zipo za kutosha kama una cheti kizuri, usimkatishe tamaa anayekusaidia umri wako katika karne ya sasa unahitaji elimu kwanza angalau ufike degree alafu ndiyo ufanye biashara. Nimekushauri hivi maana una mawazo sawa na mdogo wangu ninayemsomesha.
kuna wasomi wengi wana degree wako mtaani wanakufa njaa ajira hakuna.......niambie leo hii ni kampuni gani imetoa nafasi za kazi? AJIRA HAKUNA.......hebu washauri graduate walioko mtaani sasa hivi wa apply kampuni gani yenye nafasi za ajira...ajira hakuna
 
kuna wasomi wengi wana degree wako mtaani wanakufa njaa ajira hakuna.......niambie leo hii ni kampuni gani imetoa nafasi za kazi? AJIRA HAKUNA.......hebu washauri graduate walioko mtaani sasa hivi wa apply kampuni gani yenye nafasi za ajira...ajira hakuna
Narudia tena hakuna cheti kizuri kinachokosa kazi, kazi zipo, ajira zipo. Elimu haitakitupa milele, utachelewa lakini one day mambo yatajipa. Mimi baada ya kumaliza masterz nilikaa miaka mitatu sina ajira, ila sikukata tamaa. Nikipatacho kwa sasa ni matunda ya elimu. Kwa hiyo fanya moja kwanza la msingi mengine ndiyo yafuate.
 
Elimu inathamani kubwa sana. Usiache Elimu aende zake. Ukiwa na Elimu utahangaika kwa muda mfupi IPO Simu utapata ajira. Aliyesoma na wewe ambae hukusoma mwenzako IPO siku atakuacha kitaa. BIASHARA WENZAKO. SASA WANAFILISIKA WEWE UNATAKA UKAFANYE BIASHARA!!! Huoni wenzako wakifunga fremu? ELIMU UTAKUWA NAYO HADI KABURINI. Hata hivyo ulitakiwa urudie mtihani upate credit usome Digrii. Hata hivyo sio mbaya KWAMOYO WANGU WA DHATI KABISA SOMA SHULE.AJIRA ZIPO.SASA HIVI ZIMESIMAMA KWA SABABU RAIS ANAREKEBISHA MFUMO MZIMA WA SERIKALI. Yaani ukose Jeshi,ukose Upolisi, Ukose privati sekta!? Haiwezekani. SOMA SOMA SOMA.ACHANA NA KELELE. ZA WALIOSHINDWA SHULE.Hao wazazi wako nawapongeza sana, Mimi Mzee Wangu hakutaka nisome na aliditisha kunilipia ada tangu nikiwa kidato cha kwanza. Mama wa kambo akishirikiana na Mzee Wangu, Niliipigania Elimu nikawa naomba misaada kwa watu hadi nikahitimu kidato cha NNE, Sita, Diploma na Chuo kikuu.sasa Nina Diploma na Nina Digrii. Nimesoma bila msaada wa mzazi. BORA YAKO WEWE UNAO WANAOKUSAPOTI MIMI SIKUWA NAO.NA MZAZI WANGU PESA ALIKUWA NAYO NA ALIKUWA ANAFANYIA TAZARA. NASEMA SOMA KIJANA, SOMA
 
Huyo alie kuita ziro brain yeye ndio ziro brain Ndg ukitaka mafanikio lazma uwe na maamuzi magumu kiasi kwamba wengine wanaweza fikiria umepotea kumbe ndio unaelekea pazuri mwenye kuumia ni wew hao wengine wanao kulazimisha upite hivi hawajui maumivu unayo pata kikubwa mshilikishe Mungu akutangulie kwenye mafanikio yako maana hiyo pesa unayo somea ndio mtaji wako usitegemee ukimaliza kusoma wazaz watahangaika na wew wataangalia wadogo zako wataanza kukuambia jitegemeee maana tumesha kusomesha elimu ulio nayo inatosha kukufanya upate kaz kumbe mambo yalisha badilika
Umeongea kitu kikubwa sana,,,,wazazi wengi wakishakusomesha tu ukamaliza, wananyoosha mikono juu na kukuachia uwanja wewe na mama kairuki bila kujua kwasasa mambo ya ajira ni magumu sana. Mungu atusaidie kwakweli
 
Back
Top Bottom