Maisha yananichanganya msaada tafadhali

Mkuuu, pole kwanza katika kipindi hiki cha mpito.

Ila la msingi sana, usi disapoint wanaona mengi kwako kivipi??

Yeah, una potential lakini endapo biashara haita work out utapewa lawama na suport itaisha hapo , hapa endapo tu utaajiiba na kutumia ada huko.

Lakini cha msingi, hebu tumia mbinu zako ,huelewa wako kuongea na member wa familia. Waeleze juuu ya mawazo yako, anza na yule unaehisi atakuelewa kwa urahisi hapo utapata njia ya kuanza.

Wazeee , wakikubali na kuto kuwa na hofu juu ya future wako ,utapata baraka zao na full suport za kiuchumi na moyo.

Wape mifano ya watu waliosoma na kusugua game, waambie mwisho wa siku hakuna ajira so lazima ujiajiri hata ukisoma IT. Wape mifano ya watu walio barikiwa na kutoka kupitia biashara , wajuze kuwa ndoto zako ni kuwa miongoni mwao.

Ngumu, it will take time but hakuna lisilo wezekana.

GOD BLESS YOU BROTHER
 
Nashukuru sana ndugu yangu, nimekaa nao mara nyingi ila hakuna aliye tayari imefika hatua nafanya kitu kuwapa furaha na amani ya moyo lakini siko well committed na ninachokifanaya.
 
Do what you like! Ila achana na hiyo biashara ya miwa.
Anzisha kamugahawa kadogo simammia wewe mwenyewe huku ukizingatia usafi kwa hali ya juu,baada ya mtaji kikuwa anza kijishulisha na biashara uzipendazo.
Biashara ya chakula haofanywi na wanaume wengi lakini ni biashara nzuri pia wewe utaifanya kiosomi zaidi pia risk yake ni ndogo
 
Lengo kuu ndo hilo mgahawa na huduma ya juisi Kama extra.
 
Ushauri wangu ni kama ufuatao, kwanza tambua hakuna uwekezaji mzuri kama elimu, hivyo hutakufa njaa kama umewekeza hapo. Elfu kumi kwa week ukipunguza matumizi itakusaidia umalize chuo. Fanya jambo moja asikudanganye mtu, ajira zipo za kutosha kama una cheti kizuri, usimkatishe tamaa anayekusaidia umri wako katika karne ya sasa unahitaji elimu kwanza angalau ufike degree alafu ndiyo ufanye biashara. Nimekushauri hivi maana una mawazo sawa na mdogo wangu ninayemsomesha.
 
Mkuu suala la kuuliza biashara kwa wenye uzoefu kwa uzoefu wangu wabongo huwa tunatabia ya kukatishana tamaa! Kwa ushauri wangu ukiwa likizo its right Time ti do! Lastly biashara usiwekeze kubwa anza na juisi utafanikiwa!
 
Asante kaka mawazo yako mazuri, kitu kinachokatisha tamaa ni mtu kasoma ana vyeti vizuri but nothing to do na hana plan
 
Inaonyesha unapenda business na unamikakati ya unapotaka kufika.
Nakushauri anza biashara mara moja.

Usiogope kushindwa kwasababu hapa mwanzoni mambo yatakuwa magumu tu. Usirudi nyuma

Nilianza business tangu college. Sikuacha chuo lakini muda mwingi nilikuwa natumia kwenye mambo yangu zaidi....nilifahamu nini nataka kwenye maisha yangu. Nikishindwa ni mimi na nikifanikiwa ni mimi. Maneno ya watu/wazazi si chochote sana kwangu.

My advice for you is...have courage to follow your heart. It somehow already know what you want to become.

Failure is part of success in the business, take it as a lesson.

All the best
 
Mkuu suala la kuuliza biashara kwa wenye uzoefu kwa uzoefu wangu wabongo huwa tunatabia ya kukatishana tamaa! Kwa ushauri wangu ukiwa likizo its right Time ti do! Lastly biashara usiwekeze kubwa anza na juisi utafanikiwa!
Kupewa ushauri ni jambo moja na kuuchukua ushauri huo ni jambo jingine.
 
Pole sana ndugu cha msing wazo la biashara sio vbaya unapo badil mawazo inabidi uwe na bidia mara 2 hata zaidi
 
Wazo zuri ila fanya haya kabra ya kuanza hiyo biashara yako:soko la bidhaa yako,ukashalipata angalia compititors wa bidhaa yako na utawapikuje?,ukijilidhisha na hayo anza kuzalisha na halarisha biashara yako
 
kunywa sumu ukiona .umri dogo unaona kama umepita milima na mabonde
 
Huku unamshauri hata akusoma ajira hamna halafu unasema wanaoshinda mitandaoni kuitukana serikali ni wavivu. Ueleweke vipi au na wewe ni stress zinakusumbua?
 
Kujiajiri ndo the best solution, usitake kuishi kwa kipato utakachopangiwa na mwajiri hivyo fanya kile moyo unataka, kataa kutumwa jitume
 
Kwanza hongera sana kwa kuwa na mtazamo chanya,
Kimsingi yote yanawezekana kama utakuwa na mikakati mizuri na si vyema ukawa na maamuzi ya haraka sana ukiwa unajua bado ni Tegemezi.
 
Ushauri wangu. Sikushauri uache Chuo. Maliza,upate cheti. Kumbuka,una miaKa 7
+4+2+1...=13, uko shule. Ulichobakiza ni kidogo. Pia,ongea na wenzako,jenga urafiki nao,wenye kutoka familia nzuri kipesa watakupa tafu umalize. Nilitamani,upate cheti cha IT,baadae ufungue duka la electronics inayoendana na fani yako! Tukukute Kariakoo au Nyerere Road Mwanza uko vyema. Badala ya kuanza na kuuza vichai vya rangi,nunua bisibisi na tester,weka kibao barazani,"FUNDI COMPUTER,SIMU,NK.". Utakua haraka,ndo uingiea hatua nyingine. Mambo ya kuzunguka na mahindi siyo fani,japo inaweza kulipa!
 
nakubali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…