APPROXIMATELY
JF-Expert Member
- Aug 10, 2021
- 2,035
- 2,737
Ndugu wana jamii habari zenu,ni jambo la kumshukuru MUNGU kuwa tunapumua bila kulipa ushuru, japo maisha magumu ila tunakomaa nayo maana tutamlalamikia nani?mwenyewe kasema '' usinichoshe tusichoshane''.
Mnajuwa nini ndugu zangu, kuna mda mwingine ukikaa chini ukiyatafakari maisha ya sasa na ya zamani unaona bora maisha ya zamani, ila ukifikiria hali ilivyo sasa unajikuta unapenda maisha ya sasa.
Katika harakati za ukuaji, haswa kwa mwanaume, ana pitia kipindi kigumu sana cha ukuuaji, ninaposema kipindi kigumu na maanisha hivi, mtoto wa kiume mpaka kukua anapitia maisha ambayo mwenyezi MUNGU anamnusuru na mambo mabaya mengi.
Napenda ni toe ushuhuda wa maisha niliyopitia nikiwa mdogo enzi zile, japo wengi huficha waliopitia ila mimi leo naweka bayana maisha yangu ya utotoni, naomba mfuatane nami katika mtiririko huu wa maisha ya mwanaume.
Kwa majina yangu ya kupewa na wazazi wangu naitwa David Alexandre ila kibongo bongo naitwa daudi, jamii forums MNanijua kama
APPROXIMATELY, nilizaliwa katika hospital ya mount meru iliyopo arusha, miaka ile ya 90 Na something.
Kipindi hicho wazazi wangu walikuwa wanaishi sekei, mama ni mchagga wa machame, baba ni maasai.
Tuna ndugu wengi sana, yani kwa sisi wa maasai tunamaboma mengi sana, kwa hapo sekei tunanyumba kibao, bado za ngaramtoni, arusha chini, sanawari na kisongo, wazee wetu walishika maeneo mengi Big up kwao.
Kwetu sisi mimi ni mtoto wa mwisho kwa mama yangu, ila baba ana wake 3 ambao wa kwanza ni mama yangu mwenye watoto 8, wa pili ni mama mdogo mwenye watoto 7, na watatu ni mama mdogo pia mwenye watoto 11, baba ni hatari anatimiza ile aya 'nendeni mkazaliane' babu yangu kwao walizaliwa watoto 36, baba ake na babu yangu alikuwa na wake 4, ndugu wa babu wamezinguka maeneo yote ya arusha ikiwemo iliboru, mianzini, kijenge, ngarenaro, matejoo, kijenge.
Mpaka hapo ushaona tulivyowengi arusha, nina ndugu zangu mwenye uwezo sana Alex yule mwenye mabucha kibao iliboru ni kaka mkubwa, nina kaka wengine wauza madini, wauza mazao jumla na reja reja, nimeandika haya ili uwe na uhalisia kidogo wa maisha ya arusha.
Katika kipindi cha ukuuaji nilipitia maisha ambayo yalikuwa ya hatari sana, sema ni neema za MUNGU tu leo hii nisingekuwa hapa duniani, ila namshukuru MUNGU kuniweka hai mpaka leo..
Chekechea nilianza nikiwa na miaka 3, nakumbuka nilikuwa najielewa kidogo ila sio sana, maana hata nyimbo za zamani nazikukumbuka kama mabata mabata wadogo, mwalimu wetu hapendi kelelee n.k,
Shule ya msingi nilisoma sanawari kwa darasa la 1 mpaka 3,ila darasa la 4 mpaka la 7 nilimalizia kaloleni.
Itaendelea......
Mnajuwa nini ndugu zangu, kuna mda mwingine ukikaa chini ukiyatafakari maisha ya sasa na ya zamani unaona bora maisha ya zamani, ila ukifikiria hali ilivyo sasa unajikuta unapenda maisha ya sasa.
Katika harakati za ukuaji, haswa kwa mwanaume, ana pitia kipindi kigumu sana cha ukuuaji, ninaposema kipindi kigumu na maanisha hivi, mtoto wa kiume mpaka kukua anapitia maisha ambayo mwenyezi MUNGU anamnusuru na mambo mabaya mengi.
Napenda ni toe ushuhuda wa maisha niliyopitia nikiwa mdogo enzi zile, japo wengi huficha waliopitia ila mimi leo naweka bayana maisha yangu ya utotoni, naomba mfuatane nami katika mtiririko huu wa maisha ya mwanaume.
Kwa majina yangu ya kupewa na wazazi wangu naitwa David Alexandre ila kibongo bongo naitwa daudi, jamii forums MNanijua kama
APPROXIMATELY, nilizaliwa katika hospital ya mount meru iliyopo arusha, miaka ile ya 90 Na something.
Kipindi hicho wazazi wangu walikuwa wanaishi sekei, mama ni mchagga wa machame, baba ni maasai.
Tuna ndugu wengi sana, yani kwa sisi wa maasai tunamaboma mengi sana, kwa hapo sekei tunanyumba kibao, bado za ngaramtoni, arusha chini, sanawari na kisongo, wazee wetu walishika maeneo mengi Big up kwao.
Kwetu sisi mimi ni mtoto wa mwisho kwa mama yangu, ila baba ana wake 3 ambao wa kwanza ni mama yangu mwenye watoto 8, wa pili ni mama mdogo mwenye watoto 7, na watatu ni mama mdogo pia mwenye watoto 11, baba ni hatari anatimiza ile aya 'nendeni mkazaliane' babu yangu kwao walizaliwa watoto 36, baba ake na babu yangu alikuwa na wake 4, ndugu wa babu wamezinguka maeneo yote ya arusha ikiwemo iliboru, mianzini, kijenge, ngarenaro, matejoo, kijenge.
Mpaka hapo ushaona tulivyowengi arusha, nina ndugu zangu mwenye uwezo sana Alex yule mwenye mabucha kibao iliboru ni kaka mkubwa, nina kaka wengine wauza madini, wauza mazao jumla na reja reja, nimeandika haya ili uwe na uhalisia kidogo wa maisha ya arusha.
Katika kipindi cha ukuuaji nilipitia maisha ambayo yalikuwa ya hatari sana, sema ni neema za MUNGU tu leo hii nisingekuwa hapa duniani, ila namshukuru MUNGU kuniweka hai mpaka leo..
Chekechea nilianza nikiwa na miaka 3, nakumbuka nilikuwa najielewa kidogo ila sio sana, maana hata nyimbo za zamani nazikukumbuka kama mabata mabata wadogo, mwalimu wetu hapendi kelelee n.k,
Shule ya msingi nilisoma sanawari kwa darasa la 1 mpaka 3,ila darasa la 4 mpaka la 7 nilimalizia kaloleni.
Itaendelea......