Naandika post hii nikiwa sijui pa kuanza, il a kwa kifupi tu, nimeanza maisha mapya ya kuwa single mother.
Mimi na baba mtoto havijawork out kwa kweli na imenibidi nifanye maamuzi magumu.
Ni mwanaume nimekuwa nae kwa muda wa miaka saba ila hatujaoana, tumefanya mambo mengi ya maendeleao pamoja,ila gafla tabia yake ikabadilika akawa ni mtu wa kunigombeza bila sababu, chochote nikifanyacho kwakwe ni kibaya,lugha anayotumia kwangu akiwa na hasira ni mbovu, ila at the same time anasema ananipenda,nimekuwa ni mtu wa kuumia moyo kwa muda wote huo,najiuliza ni kupenda gani kwa namna hiyo.
Hivi karibuni nimeamua isiwe tabu kila mtu aendelee na ustaarabu wake,yeye amekuwa akitumia mtoto kunisema nina roho mbaya, sina huruma na maneno kedekede,ila kusema ukweli nimevumilia vya kutosha na sasa nimeona basi inatosha, ninampenda ndio na ingetokea miujiza abadilike ningemrudia ila ndo hivyo.kwa hasira amegoma hata kumuhudumia mtoto anasema akifika miaka saba nimpe sasa hivi akimuona atasikia uchungu kisa mimi simtaki.
Kwa wenye uzoefu jamani naanzaje kuishi maisha ya usingle mother wakati kila siku lazima mtoto aulizie daddy au hata akilia atalia daddy dady,nitakuja kumwambia nini akiwa mkubwa?na je nikija kuanza mahusiano mengine mtoto atanionaje?
Mimi na baba mtoto havijawork out kwa kweli na imenibidi nifanye maamuzi magumu.
Ni mwanaume nimekuwa nae kwa muda wa miaka saba ila hatujaoana, tumefanya mambo mengi ya maendeleao pamoja,ila gafla tabia yake ikabadilika akawa ni mtu wa kunigombeza bila sababu, chochote nikifanyacho kwakwe ni kibaya,lugha anayotumia kwangu akiwa na hasira ni mbovu, ila at the same time anasema ananipenda,nimekuwa ni mtu wa kuumia moyo kwa muda wote huo,najiuliza ni kupenda gani kwa namna hiyo.
Hivi karibuni nimeamua isiwe tabu kila mtu aendelee na ustaarabu wake,yeye amekuwa akitumia mtoto kunisema nina roho mbaya, sina huruma na maneno kedekede,ila kusema ukweli nimevumilia vya kutosha na sasa nimeona basi inatosha, ninampenda ndio na ingetokea miujiza abadilike ningemrudia ila ndo hivyo.kwa hasira amegoma hata kumuhudumia mtoto anasema akifika miaka saba nimpe sasa hivi akimuona atasikia uchungu kisa mimi simtaki.
Kwa wenye uzoefu jamani naanzaje kuishi maisha ya usingle mother wakati kila siku lazima mtoto aulizie daddy au hata akilia atalia daddy dady,nitakuja kumwambia nini akiwa mkubwa?na je nikija kuanza mahusiano mengine mtoto atanionaje?