Maisha ya ndoa yamenishinda

Maisha ya ndoa yamenishinda

Naishi na mzazi mwenzangu nahisi hana nyota ya mafanikio nifanyeje kila ninachofanya sifanikiwi kabla ya kuwa nae mambo yalikuwa hayakwami naombeni ushauri.
Hapo tatizo sio huyo uliyenaye, angalia mfumo uliokua unapatia pesa umebadilika, hivyo lazima ubadilike kutokana na mifumo inavyobadilika, tatizo hili ni kubwa sana ktk nchi za wenzetu na sasa limefika hapa kwetu, maisha yanaenda kasi sana, panga unapotaka kufikia kwenye maisha yako, panga matumizi yako vizuri, chukua hatua ya kufanya jambo ambalo unaamini litakufikisha kwenye mafanikio uliyopanga.
 
KUOA NI JAMBO PANA LINALOHITAJI UPEMBUZI YAKINIFU KABLA YA KUFANYA MAAMUZI HAYO...........

KWA ANDIKO HILI NI DHAHIRI KUWA HUKUFIKIRIA VYEMA KABLA YA KUFANYA UAMUZI........

MIKASA NA MISUKO SUKO NI SEHEMU YA MAISHA AMBAYO KILA MWANADAMU ANAPITIA BILA KUJALI AMEOA AU YUPO SINGLE.......

UNACHOTAKIWA KUJUA NI KUWA HAKUNA HALI INAYODUMU.....NYAKATI ZINAPITA NA WATU SHUPAVU HUDUMU......
 
Naishi na mzazi mwenzangu nahisi hana nyota ya mafanikio nifanyeje kila ninachofanya sifanikiwi kabla ya kuwa nae mambo yalikuwa hayakwami naombeni ushauri.
Ww ulimuoa ili ufanikiwe? Amekuwa kazi yeye?
Mafanikio yanaanza na ww.
Anyway kwenye suala la nyota. Ulikuwa wapi siku zote usigundue hito hali?

Matatizo yako usije ukamdondoshea mwenzio. Tatizo linaanza na ww.
 
Naishi na mzazi mwenzangu nahisi hana nyota ya mafanikio nifanyeje kila ninachofanya sifanikiwi kabla ya kuwa nae mambo yalikuwa hayakwami naombeni ushauri.
Kipato kabla ya ndoa, kilikurosha wewe binafsi, sasa umeoa, majukumu na gharama zimezidi na hujaongeza kipato. Kaa chonjo, ataongezeka na mtoto kama sio watoto, sijui utafanya nini?
 
Siku utakayo acha kutafuta sababu ya kwanini haufanikiwi ndo siku hiyo hiyo utaanza kufanikiwa.


Wenzako wanatafuta hela wewe unatafuta sababu kwanini hufanikiwi???

By the way mama mkwe wako au mama ako sio wachawi???maana mtoto wa mchawi hafanikiwagi???nimemaliza...
 
Back
Top Bottom