edwayne
JF-Expert Member
- Apr 5, 2013
- 8,880
- 9,683
Sasa hii inatofauti gani na kafara za wachawiZamani ilikuwa ni kawaida kuwatoa watoto dhabihu kwa Mungu eti kwamba sadaka ya kuteketezwa ile unayoipenda zaidi ndio nzuri zaidi. Mnajua Jephta alimtoa mwanaye wa kike na nani sijui aliwajengea wanae katika kuta za hekalu/ukuta sijui.
Muendelezo wake ndo kama sasa hivi mtu akikushawishi kumtolea Mungu mali kubwa 'itakayokuuma' eti ndio utakuwa umeonesha kumpenda zaidi.
Ifahamike wazi Mungu hajawahi kuhitaji sadaka all along, na hata kama ukikaza shingo kwamba ni lazima kumtolea toaga tu kwa mapenzi yako sio eti kama ni kitu anakihitaaaaaaaaaaji.
Kwa mtazamo mama yake, na mwanae hawangemchukulia baba yao kama katili binafsi, no hard feelings. Wangeshukuru tu kwa pamoja na waliendelea kupendana zaidi. Maana mtoaji na mtolewaji wote walikuwa na hisia kwamba hilo ni jambo zuri sana. Mtoto labda hata aliona kapendelewa, kapendwa zaidi, kutolewa ikawa ni ishara ya upendo zaidi kuliko ukatili.
Mnakumbuka yule binti wa jephta/sijui joshua pia. Hata yeye atakuwa aliona yeye kutolewa ni jambo sahihi kabisa. Msiwaone wa ajabu, au msione kifo ni kitu kibaaaaaaya. Kufa kwa ajili ya kusudi/worthy goal huendelea kuchukuliwa kitu cha heshima. Wanaokufa RUSSIA NA UKRAINE ni uthibitisho tosha. Kilichobadilika ni goals tunazozichukulia ni worthy kulingana na utamaduni wa wakati husika