Maisha ya Dodoma ni Magumu sana

Maisha ya Dodoma ni Magumu sana

Tunaoishi dodoma na familia zetu zinaenda chooni bila shida ni wanaume kweli kweli mtupe Heshima zetu,

Huku chumba kibaya kibaya tu ili mradi kiwe na umeme na maji ni elfu 50,

Chumba angalau, angalau Single tu elfu 60k au 70k kwa mwezi,
Self kuanzia 80k mpaka 100k huku bili ya maji ikikuelemea,
Ukitaka master, Yenye chumba kimoja, sebure na choo ndani jiandae na kuanzia 150k mpaka 180k kwa mwezi huku bili ya umeme,maji na ya kodi ya jengo ikikuelemea,

Ukitaka Apartment, au Nyumba nzima ya kuanzia vyumba viwili au vitatu yenye sebure, choo ndani, master room moja na jiko jiandae na kuanzia 350K mpaka 500k kwa mwezi.

Usisahau na malipo ya dalali ya mwezi mmoja.


Ukifanikiwa kuishi dodoma mwaka bila shida yeyote basi hakuna mkoa utashindwa kuishi hapa Tanzania.


Cc Zero IQ

Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee upo sahihi.dodoma ni pagumu si mchezo.
 
Mkulungwa, unalinganisha bei ya bidhaa Dodoma na kipande kipi cha nchi. Bei ulizozitaja nikilingasha na DAR mbona ni za kawaida, mfano kilo ya mdudu kwa TZS 10,000
Hujamuelewa anachoimanisha ni kuwa how Bei ilingane na town
 
Wakuu hbr za jioni??,Wiki hii Nilikuwa DODOMA kwa shughuli za Kiofisi,nimependa jinsi jiji la Dodoma linavyokua kwa kasi,Lakini hali ya maisha inaonekana ni ngumu Sana kuliko Dar es salaam.

Nilitafuta guest house,bodabo whyda akaniambia kuwa vyumba vya bei ya chini ni 20,000/=,nikashangaa Sana kwasababu niliwahi kwenda DSM na nikafanikiwa kupata gesti ya 10,000/=, nzuri tu.Chakula kwa Dodoma ndo usiseme,kipimo changu cha kwanza ni kwa Mama ntilie, maana watu wengi wa hali ya chini huenda huko kununua chakula;

Aise kina bei hatari [emoji134][emoji134][emoji134], Kuna sehemu niliambiwa wali nyama 3,000/=,Ugali nyama 3000/=,Wali samaki 3500/=, Ugari Maharage 2000/= na wali Maharage 2500/=, Sehemu nyingi za Mama Ntilie bei ni hizo.Nilipolala ni karibu na Holly Cross Center inayomilikiwa b

Na Kanisa Katoliki Jimbo kuu la DODOMA,Aise hapo kitimoto ya kukaanga kilo ni 10,000/=,Ya kubanikwa ni 12,000/=,Ndizi moja 500/=. Ugari kuku robo 6000/=.Na vyakula vingine bei zipo juu pia.Haya nikasema Niulize Vipi kuhusu nyumba za kupanga?;Kheee!!!,Bei nilizotajiwa nilishangaa Sana.Twende Bodaboda aisee Hivi kweli kutoka Holly Cross Center hadi Mkonze mtu anaanza na 6000/=baada ya kuvutana Sana ndo anaishia kwenye 4000/=.

Sijauliza viwanja.Nastaajabu kwasababu miaka ya Nyuma DODOMA haikuwa ghali kiasi hicho.Nilijiuliza swali moja kuwa DODOMA ni wafugaji wazuri wa mifugo sasa Kwanini bei ya Nyama ya ng'ombe ipo juu hivi?? Mnazidiwa na Morogoro ambao hawafugi km ninyi kweli??!!!.

Serikali ichunguze Hali hii, kwasababu inachangia kwa kiasi kikubwa sana Watumishi wa wizara waliokuwa wamehamishiwa DODOMA kutoka Dar kutamani kurudi Dar kuliko kuishi DODOMA.Tafadhari Serikali inusuru Hali hii.
dah, guest ya 10,000 mwanangu unatafuta matatizo kama si kuibiwa basi kungunj
 
Nitakwenda soon nikaone uhalisia.

Nenda ukajionee mkuu. Na kwa sasa wanaelekea msimu wao wa utajiri, msimu wa korosho kila mwananchi ana hela, inasemekana msimu huu unaweza kuwa na mauzo mazuri pamoja mazao mengi, kwa hakika nenda ukirudi utatoa ushuhuda humu. Au kama kuna mtu ameshawahi kuishi atatoa ushuhuda humu
 
Aiseee tutafute pesa



Kuna rafiki yangu yupo TRA makao makuu

Toka nimekutana maybe hajawahi burgain wala kulalamika pesa hata msosi anauliza haangaiki na Menu
Sasa Kumbe umesema yupo tra?!!!.
 
Hujatembea vzuri mkuu.alafu mbona dar kukunusu kienyeji inafika 10k na tena wanakufa nichotara si kienyeji of.
 
Back
Top Bottom