Sandinistas
JF-Expert Member
- Jul 5, 2013
- 2,616
- 1,778
Kitu ambacho sisi kama taifa (Tanzania) tunakosea ni kwamba Lissu mpaka kwenda kuongea na vyombo vya habari vya kimataifa ni PLANNED ISSUES ya jumuiya ya kimataifa Kwa maana kwamba walimhoji kuhusu kadhia iliyompata baada ya hapo wakawa wanatafuta njia ya kupata information kutoka upande wa pili unaotuhumiwa na LISSU wakaona njia pekee ya kupata majibu/information hizo ni LISSU kwenda kwenye vyombo vya habari kuyasema Kwa kufunguka hasa kama ambavyo LISSU alivyofanya. Kazi yao ilikuwa ni kusikiliza majibu ya upande unao tuhumiwa unasema nini, kibaya zaidi upande unaotuhumiwa umetoa majibu yasiyokizi hadi kufikia hatua kuanza kumtisha mhusika na vijembe vya kila aina tena kwa watu wasio na weredi jadidi wa kujibu hoja nzito kama ambazo LISSU amezitoa.
USHAURI WANGU Kwa serikali na nchi yang.
1. Tuwe na vitengo maalumu vya watu wenye uwezo mkubwa wa kupambana na hoja nzito zinazoilenga nchi na serikali
2. Tuwadhibiti watu wengine wasio husika kujibu vitu ambavyo hawana weredi navyo kama akina Bashiru, Makonda na polepole
3. Tutofautishe lipi linatakiwa kujibiwa kisiasa na weredi wa kisiasa na lipi linatakiwa kujibiwa ki-weredi na wenye ujuzi wa kujibu ki-weredi zaidi
4. Tuache ushabiki wa kivyama unaotupelekea kuwa na chuki miongoni mwetu maana sisi sote ni Watanzania na Tanzania ni yetu sote
5. Sheria na utu wa mtu uheshimiwe asiwepo mtu hata mmoja ambaye atapanga/kunuia kumzuru mwenzie kisa tu ametofautia naye kimawazo/kimtazamo.
6. Tunapotofautia kimtazamo tuwe na utamaduni wa kukaa Meza moja kwa nashauriano ya kufikia mwafaka.
7. Kuongoza nchi ni haki ya kila Mtanzania hivyo basi tusijenge taswira kwamba kikundi/Chama fulani ndicho chenye haki ya kuiongoza nchi wakati kikundi/Chama fulani hakina haki hiyo tutasababisha vurugu na machafuko nchini. Katika hili tunatakiwa kuweka vyombo huru vitakavyosimamia haki kwa vyama vyote vya Siasa.
Tutende Kwa haki bila buguza zozote maana haki ikiendelea kuvunjwa itawafanya watu kujengeana chuki na visasi ambapo mwisho wake ni machafuko nchini.
Mungu akubariki sana. Kama mzalendo wa kweli wa nchi hii nimeipenda zaidi hili la kuwa na wasemaji maalum wa kiserikali kwenye mambo makubwa kama hili la shambulio la Lissu. Just imagine waziri anaibuka from nowhere anasema eneo la shambulio halijapata kuwa na cctv kamera. Hata kama ni kweli hazikuwepo, kwa sasa haikuwa busara kusema hivyo! Katibu Mkuu wa ccm pamoja na Ph.D yake ni janga tupu. Kama taifa tunaibika kutokana na watu wasiokuwa na weledi. Some of us are really ashamed of our own country because of these lilliputians at the helm of our politics.