Proved
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 27,540
- 34,864
Usiogope Mama Magreth Sitta wana Urambo watakuchagua kwa kishindo.Haya Ni maigizo ya wamama wa Urambo wa Baraza la wanawake CHADEMA, hiki ndicho walichoamua kukifanya kwa kujitengenya wenyewe na kucheka wenyewe kwa kujiongopea wenyewe huku wakitaka kuwadanganya watanzania .
Nimejaribu kuwaza hivi Kama kweli Urambo kuna tatizo la maji ujasiri wa hawa akinamama wa kutandika nguo zao chini kwenye vumbi wanapata wapi wakati hakuna maji ya kufulia hizo nguo jibu Ni kwamba haya Ni maigizo tu .
Kama tatizo la maji lipo Urambo vijana wa Urambo wamepata wapi maji ya kumwagia barabara na kudeki ili mgombea wachadema apite jibu Ni kwamba haya Ni maigizo ya CHADEMA.
Kama kweli Urambo hakuna maji hizi nguo walizovaa na kupendeza kabisa wanafulia maji ya wapi au wanafulia damu nguo zao jibu linakuja Ni kwamba hivi Ni vionja tu vya Uchaguzi kwa CHADEMA.
Kama Urambo hakuna maji hawa akinamama na wababa wanaoonekana wanaafya nzuri kabisa wanapikia nini na wanakunywa maji au matope jibu Ni kwamba wanakunywa maji safi na Salama sema wameamua kufanya the isidingo
Kama Urambo hakuna maji hii jeuri ya akinamama kusimama juani wanaitoa wapi wakijua miili yao itatoka jasho na kuchafuka na inaweza kunuka wanaitoa wapi mwisho wa siku Ni maigizo ya tu yanafanyika .
Nimalizie kwa kusema uongo una mwisho wake Mama Magreth Sitta Mbunge wa URAMBO atatolea ufafanuzi zaidi dhidi ya haya maigizo ya watu kununuliwa.