Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 25,946
- 38,656
Hatua ya Kwanza
Mgombea Mwenza anatoka hadharani tarehe 11/ 08/ 2025 na kudai kuwa chakavu wanahitaji 100B waweze kufanikisha kampeni ya kubakiza Costra Nosta sebuleni kwao. Roadmap ni harambee scheme
Hatua ya pili
Tarehe 12/ 08/ 2025 inafanyika harambee kabambe ambapo jumla ya Bilion 86+ zinakusanywa. Wafanyabiadhara wanaonekana walikuwa wameshajiandaa kitambo kuchangia.
MATUKIO FIKIRISHI
My Take:
CCM akina Tlaatlaah, Lucas Mwashambwa, chiembe, Pascal Mayalla, Ritz na wengineo, nawaalika tujadili haya maigizo ya chama chenu...
Mgombea Mwenza anatoka hadharani tarehe 11/ 08/ 2025 na kudai kuwa chakavu wanahitaji 100B waweze kufanikisha kampeni ya kubakiza Costra Nosta sebuleni kwao. Roadmap ni harambee scheme
Hatua ya pili
Tarehe 12/ 08/ 2025 inafanyika harambee kabambe ambapo jumla ya Bilion 86+ zinakusanywa. Wafanyabiadhara wanaonekana walikuwa wameshajiandaa kitambo kuchangia.
MATUKIO FIKIRISHI
- Tangazo la harambee linatoka leo, kesho yake tukio linajiri kwa ufanisi mkubwa
- Kamati ya maandalizi hakuna wala waratibu lakini mialiko imeshatumwa, ukumbi umeshachaguliwa na kulipiwa less than 24hrs pamoja na itifaki zote kupangiliwa na kupangika
- Washiriki ni wawekezaji wakubwa ambao ndani ya muda mfupi wameonesha kujiandaa kikamilifu kushiriki huku wengine wakijinasibu kuwa walifanya vikao na wenzao waliowawakilisha
My Take:
- CCM kuishiwa mikakati na mbinu za kipropaganda ni ajali, makusudi au kukosa kujiamini?
- Tukio hili la harambee linazidi kuiweka CCM shimoni kwa sababu sehemu kubwa ya washiriki wanatuhumiwa kwa.ufisadi na matukio yanayohusisha kukosa maadili kijamii.
- CHADEMA imeendesha kampeni zake kwa kuchangiwa na Watanzania wengi kwa mtindo wa tone tone, lakini CCM inachangiwa mabilioni kutoka kwa matajiri wachache. Hii inatuma ujumbe kuwa wenye nguvu wameungana na kujenga umoja nyuma ya CCM kuwakabili wanyonge wa tone-tone
- Mtanzania unaenda kutiki hapo Oktoba kwa utaratibu ama demokrasia ipi?
- Suala la utakatishaji fedha lipo kwenye heading tu. Sijaliandikia humu ndani zaidi ya passage hii
CCM akina Tlaatlaah, Lucas Mwashambwa, chiembe, Pascal Mayalla, Ritz na wengineo, nawaalika tujadili haya maigizo ya chama chenu...