Wana jf, katika professional za watu na mahusiano nimekutana na kikao cha watu wakijadili hiyo mada. Wanasema kuwa wanawake wanaofanya kazi ya uuguzi(manesi) ni rahisi sana kutoka nje ya ndoa zao kulingana na nature ya kazi yao. Kuna mama mmoja naye ni nesi kwenye hospitali mojawapo ya mkoa hapa Tanzania alikuwa anawaambia wanakikao hao kuwa katika ile hospitali manesi wote wa kike walioko pale wanafanya kile kitendo kwenye vile vyumba vilivyomo wodini kwa ajili ya kupumzikia. Eti mara nyingi hufanya hvyo usiku. Kwa kweli nilivyosikia hvyo ikabidi niwaletee wadau humu tuijadili kama haya mambo yanatokea kweli au huyu mama alikuwa anawasingizia.