Msitake kujifanya Kila mtu ni msafi jamii forum, wapo watu humu Wana ma background yao nyuma yakutisha ili wamefyata mkia, wapo watu wamelelewa na masingle mother Ila wanajsahaurisha,wapo watu humu wameacha mama zao vijijini wakiwa wametelekezwa na waume zao na msururu wa wadogo zao Ila wanajsahaurisha, wapo watu wamelelewa na baba ambao sio wa kuwazaa humu, ushukuru unalijua Hilo, alafu Leo useme single mother sio afai mlitaka uyo mtoto akamtupe chooni? Mje kusema wanawake Wana roho Mbaya? Mlitaka akatoe mimba mpate lingine la kuongea? Lipi jema kwenu? Shida yao ni kwenda leba na kuleta kiumbe dunian? Au shida ni kulea mtoto bila baba? Kama wewe hutoweza kuoa single mother yupo ambae ataweza kumuoa na kumpa ya thamani yake Kama wanawake wengine. Kama binti zenu wakizalishwa nyumbani muwe na msimamo huo huo wa single mother kutoolewa muendelee kuvuna mloyapanda Kama mnaona ni sawa, Mwisho wa siku maisha ni haya haya hakuna maisha mengine, #ishi unavyoweza
Sent using
Jamii Forums mobile app