Mahari inaendaga wapi?

Mahari inaendaga wapi?

Sabah al-kheyri wanaJF, Mara nyingi utamaduni wa kutoa na kupokea mahari huwa baada ya makubaliano kati ya wazazi wa bi Harusi(binti) na Bw.harusi au wahusika wake, Mwenye kupokea mahari huwaga wazazi wa bi.harusi hapo sasa Bi harusi anaambiwa figures tu lakini listi ya programu za shughuli ndizo zinakula mahari yote.[ ..... Sasa hapa kuna faida gani kwa wazazi kama mahari yote itapotelea kwenye hizo programu za shughuli?
Na'am, Bi Munkari tamaduni zapishana, Kutokana na hali halisi yakuwa wazazi huona BINTI yao kafaikiwa Mume nao kupata mkwe (ufahari ndani ya ukoo) hiyo kwanza ni hadhii ! kwakuwa bidhaa hii imejaa mjini ambayo inaushindani mkubwa Pili Money(mahari) sii lolote mbele ya mwali wao kufurahia harusi yake THE DAY (hiyo kiuswahili ni hadhii na heshima) Tatu, huwaga hawuzi binti kujitajirisha ndo maana wapo kama walivyo... "Natamani maBinti wetu wote wapate Waume wema" na "Vijana wetu wote wapate Wake wema" AMIN

 
Mahari inaenda wapi?

Inategemea. . .kama familia imekaa kibiashara zaidi (kukomoana kwa kudai dau kubwa mpaka ujuuuuute kumfahamu mtarajiwa inahusika) basi huo ni mtaji. Japo ile ni kama zawadi kwa wazazi au binti(kwa waislamu) wapo wanaofanya kama mtaji/kipato cha kuendeleza mambo ya kifamilia ama kutatua shida zao mf. waMassai na ng'ombe wa mahari.
 
mi nilichoonaga uswazi,inatumuka kutatua changamoto za household,
kulipia viporo vya skuli fees,kumnunulia mzee bodaboda etc..
its a windfall unexpected income..just spend it to solve any immediate problem..
anaebisha anitafute nkamuoneshe ushahidi wa wathi kabitha..
 
Hahahahahaahaaa!!!! umenichekesha, anyway, mkaja ni kama zawadi wanayopewa wazazi kama asante yao ya kunizaa , kunilea vizuri mpk nikapata mume, so yule mume anawapa wazazi kuwashukuru.

Lisa nimeipenda hiyo yako ya kudai mahari ununuliwe vitu vya ndani.ulifanya vema! Lakiinii, huoni kuwa kama ulimtesa huyo bwana yani atoe mahari afu atoe na zawadi kwa wazazi(mkaja) for what? Ama ndo utaratibu wa kabila lenuu ama ndivyo ulivyoamua wewe,ama ndivyo ulivyokuwa umepanga na mumeo mtarajiwa! Haahaa! Maswali mengi kidogo!
 
Last edited by a moderator:
kama mimi kwa upande wangu nilidai mahari vitu vyote vya ndani(kabati la nguo,kabati la vyombo, kitanda,makochi,dresing table, set ya Tv) wakambiwa wanunue waviweke kwenye nyumba nitakayo kwenda kuishi...
'Mchaga' wewe una mahesabu makali lol...yaani timing yako ni kama ya kuvizia shingo ya kobe upate kumtenganisha na kiwiliwili chake.
 
Kwa mujibu wa taratibu na mafundisho ya kiislam, Mahari huwa ni stahiki ya binti.

Mengineyo ni tamaduni na mapenzi binafsi juu ya mgao.

ok,hii nzuri maana hapo binti ataamua mwenyewe afanye mgao au lah! Siyo wengine utakuta hadi shangazi mzaa mjomba anatolea macho hilo fungu utadhani cku nikilala na njaa na mumewangu atakuwepo vilee loh!
 
Kwa mujibu wa taratibu na mafundisho ya kiislam, Mahari huwa ni stahiki ya binti.

Mengineyo ni tamaduni na mapenzi binafsi juu ya mgao.
Hivi mahari ni lazima iwe pesa?hakiwezi kuwa kitu chochote ambacho huyo bi harusi mtarajiwa anakitaka mfano kama akimwambia bwanaharusi ukinisomea mashafu nzima imetosha?
 
Heshima yenu wakuu! mwenzenu hilo swali hapo juu linasumbua akili yangu hivyo nataka kufahamu. Binti anapochumbiwa na kutolewa MAHARI(pesa) huwa inaenda WAPI? Je,anapewa yeye mwenyewe yote kwa mambo yake binafsi, au wazazi/walezi baba na mama wanagawana peke yao, au familia nzima huwa inagawana wakiwemo mashangazi cjui wajomba madada na makaka, au binti mwenyewe na wazazi wake pekee, au huwa inawekwa kwa ajili ya maandalizi ya vitu kama kitchenparty na sendoff?,ama inakuwaje? Au matumizi na mgawanyo huo hutofautiana kabila na kabila? Nijuzeni mwenzenu mana sikuhizi mahari imekuwa kama mtaji mtu anaoa hadi kwa millioni 2 utadhani ananunua kiwanja magwepande daah! That y vijana bado wapowapo wakifikiria hapa, siwalaumuu! Haya karibuni kwa discussion..... Nitarudi bdaye! Cc Heaven on earth christine ibrahim Lady doctor @Lara1 Nivea Smile miss strong DEMBA Kongosho Mamndenyi Mtambuzi watu8 Himidini HorsePower Mr Rocky Kaizer and OTHERS...

Kila kabila na utaratibu wake. Wengine binti mwenyewe ndio hupewa, wengine baba nk
 
Hivi mahari ni lazima iwe pesa?hakiwezi kuwa kitu chochote ambacho huyo bi harusi mtarajiwa anakitaka mfano kama akimwambia bwanaharusi ukinisomea mashafu nzima imetosha?
Sio lazima pesa.
Unaweza hata ukamwambia nataka kitenge tu biashara ikaisha, ila mwanaume nae anaangalia kama anaweza/taka kukupa zaidi ya kile ulichosema wewe basi anaongeza dau.
 
Lisa nimeipenda hiyo yako ya kudai mahari ununuliwe vitu vya ndani.ulifanya vema! Lakiinii, huoni kuwa kama ulimtesa huyo bwana yani atoe mahari afu atoe na zawadi kwa wazazi(mkaja) for what? Ama ndo utaratibu wa kabila lenuu ama ndivyo ulivyoamua wewe,ama ndivyo ulivyokuwa umepanga na mumeo mtarajiwa! Haahaa! Maswali mengi kidogo!

Hapana hata yeye mwenyewe alistuka kidogo, hadi akaniomba nimpunguzie nikamwambia wewe fanya hivyo, baadaye alikuja kujua kuwa ni vyetu mimi na yeye na si vya wazazi, ni kama nilikuwa namwambia anunue vitu vipya vya kuja kutumia mimi na yeye pamoja na watoto wake. nakumbuka siku aliyokuja kusema vimekamilika akadhani wataenda kuvifuata akashangaa kuona wameenda watu 2, kukagua kama vimekamilika na kuviacha hapo hapo, kisha wakauliza mbona hambebi wakajibiwa ni vya maharusi na si vya wazazi. wakabaki wanashangaa.
 
'Mchaga' wewe una mahesabu makali lol...yaani timing yako ni kama ya kuvizia shingo ya kobe upate kumtenganisha na kiwiliwili chake.

Hahahahaahaaa!!!! Hapana si mahesabu ila ni kuona mbali, na sasa hivi ananikubali sana maana tunavitumia wote kwa raha mustarehe, kiasi nikimshauri kitu anakubali bila kipingamizi kwa sababu anajua lazima kitakuwa na faida kwake na familia yake.
 
Heshima yenu wakuu! mwenzenu hilo swali hapo juu linasumbua akili yangu hivyo nataka kufahamu. Binti anapochumbiwa na kutolewa MAHARI(pesa) huwa inaenda WAPI? Je,anapewa yeye mwenyewe yote kwa mambo yake binafsi, au wazazi/walezi baba na mama wanagawana peke yao, au familia nzima huwa inagawana wakiwemo mashangazi cjui wajomba madada na makaka, au binti mwenyewe na wazazi wake pekee, au huwa inawekwa kwa ajili ya maandalizi ya vitu kama kitchenparty na sendoff?,ama inakuwaje? Au matumizi na mgawanyo huo hutofautiana kabila na kabila? Nijuzeni mwenzenu mana sikuhizi mahari imekuwa kama mtaji mtu anaoa hadi kwa millioni 2 utadhani ananunua kiwanja magwepande daah! That y vijana bado wapowapo wakifikiria hapa, siwalaumuu! Haya karibuni kwa discussion..... Nitarudi bdaye! Cc Heaven on earth christine ibrahim Lady doctor @Lara1 Nivea Smile miss strong DEMBA Kongosho Mamndenyi Mtambuzi watu8 Himidini HorsePower Mr Rocky Kaizer and OTHERS...
mara nyingi mahari inachukuliwa na wazazi. hata waislamu wengi ambao nimewaona mimi wazazi wao ndo wamekula mahari ingawa dini inasema achukue binti. nadhani wengi tunafuata mila na desturi na si dini katika suala hili.
 
Kwa sukumaland mahari ni mali ya familia, kwa hiyo mkuu wa familia ndo mmiliki wa hiyo mali, kama baba yupo yeye ndo huwa mmiliki, kama baba alishatangulia humilikiwa na kaka (namanisha ndugu zake wa kiume baba mmoja mama mmoja bila kujali kama ni wadogo au wakubwa kwake) zake kwa mwongozo wa mama yao, kama hana kaka wala baba basi ni mali ya mama yake na kama mama hayupo basi itakuwa mali ya wadogo zake wa kike iwasaidie kusoma chini ya mwongozo wa babu na bibi hasa wazaa baba, baba mdogo/mkubwa, mama mdogo/mkubwa, shangazi au mjomba au dada yake; yule aliyehusika kumkuza na anayelea hao wadogo zake ndo anayetajwa hapa; kama wote hao hawapo basi aliyemlea ndo halali yake; na kama kwa bahati mbaya pengine baba yake hakutambulika au alimkataa basi mahari huwa mali ya mama yake au babu yake mzaa mama au mjomba hapa inategemea na aliyemlea.
 
^^
Kwa baadhi ya mila na desturi mahari ni alama ya shukrani kwa malezi mema ya binti..hivyo ndugu waligawana mahari kwa furaha amani na upendo.
Pia mahari ni alama ya muungano halali wa ndoa.
Kwa sasa nadhani bado mahari kitamaduni inaenda kwa upande wa mwanamke na wanaigawana.
Munkari nachojua mimi ni hicho,,na mahari imekuwa pesa ambayo ni rahisi kugawana.
^^
 
Last edited by a moderator:
dah, wengine tulipokea mahari zetu wenyewe tena kwa mpesa.
 
Back
Top Bottom