Mahari inaendaga wapi?

Mahari inaendaga wapi?

Munkari

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2013
Posts
8,084
Reaction score
4,365
Heshima yenu wakuu! mwenzenu hilo swali hapo juu linasumbua akili yangu hivyo nataka kufahamu. Binti anapochumbiwa na kutolewa MAHARI(pesa) huwa inaenda WAPI? Je,anapewa yeye mwenyewe yote kwa mambo yake binafsi, au wazazi/walezi baba na mama wanagawana peke yao, au familia nzima huwa inagawana wakiwemo mashangazi cjui wajomba madada na makaka, au binti mwenyewe na wazazi wake pekee, au huwa inawekwa kwa ajili ya maandalizi ya vitu kama kitchenparty na sendoff?,ama inakuwaje? Au matumizi na mgawanyo huo hutofautiana kabila na kabila? Nijuzeni mwenzenu mana sikuhizi mahari imekuwa kama mtaji mtu anaoa hadi kwa millioni 2 utadhani ananunua kiwanja magwepande daah! That y vijana bado wapowapo wakifikiria hapa, siwalaumuu! Haya karibuni kwa discussion..... Nitarudi bdaye! Cc Heaven on earth christine ibrahim Lady doctor @Lara1 Nivea Smile miss strong DEMBA Kongosho Mamndenyi Mtambuzi watu8 Himidini HorsePower Mr Rocky Kaizer and OTHERS...
 
Last edited by a moderator:
Sabah al-kheyri wanaJF, Mara nyingi utamaduni wa kutoa na kupokea mahari huwa baada ya makubaliano kati ya wazazi wa bi Harusi(binti) na Bw.harusi au wahusika wake, Mwenye kupokea mahari huwaga wazazi wa bi.harusi hapo sasa Bi harusi anaambiwa figures tu lakini listi ya programu za shughuli ndizo zinakula mahari yote. Kwa kuwa binti anataka kutoka hapo nyumbani kwao basi huamua kujiozesha (kumpata mume) na hatimaye kutoambulia katika ile mahari....huku uswahilini hakunaga kitchen-party. Tunafanyaga KARAMU na Maulidi !! Sucha nice cermony.!
 
Munkari suala la mahari inaenda wapi ni suala pana sana kujadili, maana inategemea imani ya dini mtu aliyonayo au na pengine na tamaduni za kabila husika. Kwenye tamaduni nyingi, mahari huchukuliwa kama "token of appreciation" inayotolewa toka kwa kuoaji kwenda kwa mzazi wa binti kumshukuru kwa kumzalia na kumtunzia huyo binti. Mahari hiyo pia hugawiwa kwa ndugu wa karibu kama babu, bibi, wajomba, mashangazi nk kulingana na mila na tamaduni za eneo husika.

Tukirudi kwenye imani, kama alivyosema Rock City, kwa waislam mahari huenda kwa binti anayeolewa. Ukisome Quran [4:4] kuna andiko linasema "You shall give the women their due dowries, equitably. If they willingly forfeit anything, then you may accept it; it is rightfully yours."

Lakini kwa upande wa Wawakristo, Maandiko yanasema mahari huenda kwa wazazi wa binti na ilitafsiriwa kama "payment made by a man as a gift to the family of a woman he desired to be his wife". Ukisoma Genesis 29, andiko linasema "Jacob loved Rachel and offered to work seven years for her father, Laban, in exchange for her hand in marriage". Na huu ulikuwa ni mfano wa mahari zilizotolewa zamani ktk imani na tamaduni tofauti.

Hitimisho kwa mtazamo wangu
Hivyo, ndugu suala la mahari inakwenda wapi inategemea imani ya dini yako na kama si mtu wa imani sana basi tamaduni za kabila lako husika. Ni ngumu kuelezea moja kwa moja wapi mahari iende kwa sababu ya tofauti za kiimani na kitamaduni.
 
Inategemea na Familia, kama mimi kwa upande wangu nilidai mahari vitu vyote vya ndani(kabati la nguo,kabati la vyombo, kitanda,makochi,dresing table, set ya Tv) wakambiwa wanunue waviweke kwenye nyumba nitakayo kwenda kuishi, walipo maliza ndugu upande wangu wakaenda kukagua ndipo nikafunga ndoa, na tunavitumia mimi na mume wangu mpk leo.
Ila mashangazi, Baba na mama walipewa mkaja wao.Hii inapelekea mpk mume wangu alifurahi na kusema alikuwa anahisi nataka kumfilisi kumbe tunakuja kuvitumia wote mimi na yeye na watoto wetu kwa ujumla.
 
mie nanyojua huwa wanagwana wanafamilia,kina shangazi wajomba,bibi na wengineo

nakumbuka wakati my sister anaolewa ndio ilikuwaga hivi
 
Inategemea na Familia, kama mimi kwa upande wangu nilidai mahari vitu vyote vya ndani(kabati la nguo,kabati la vyombo, kitanda,makochi,dresing table, set ya Tv) wakambiwa wanunue waviweke kwenye nyumba nitakayo kwenda kuishi, walipo maliza ndugu upande wangu wakaenda kukagua ndipo nikafunga ndoa, na tunavitumia mimi na mume wangu mpk leo.
Ila mashangazi, Baba na mama walipewa mkaja wao.Hii inapelekea mpk mume wangu alifurahi na kusema alikuwa anahisi nataka kumfilisi kumbe tunakuja kuvitumia wote mimi na yeye na watoto wetu kwa ujumla.

mwe mkaja ndio nini na mie wazazi wangu waje kupewa
 
Munkari......mahari ni zawad inayostahil kutolewa kwa wazaz au walez pindi bint yao anapofikia muda wakuolewa.

Inategemea na makabila .....ila kabila letu,inaliwa na kila inayomuhusu kama alivyosema BADILI TABIA
 
Last edited by a moderator:
Unakolipa ndiko inakokwenda au unatakaje
 
Sie kwetu mahari hadi walioko vijijini hata kama ni watoto lazima wapewe chao haijalishi ni 200,300 lazima wapewe.
 
Munkari suala la mahari inaenda wapi ni suala pana sana kujadili, maana inategemea imani ya dini mtu aliyonayo au na pengine na tamaduni za kabila husika. Kwenye tamaduni nyingi, mahari huchukuliwa kama "token of appreciation" inayotolewa toka kwa kuoaji kwenda kwa mzazi wa binti kumshukuru kwa kumzalia na kumtunzia huyo binti. Mahari hiyo pia hugawiwa kwa ndugu wa karibu kama babu, bibi, wajomba, mashangazi nk kulingana na mila na tamaduni za eneo husika.

Tukirudi kwenye imani, kama alivyosema Rock City, kwa waislam mahari huenda kwa binti anayeolewa. Ukisome Quran [4:4] kuna andiko linasema "You shall give the women their due dowries, equitably. If they willingly forfeit anything, then you may accept it; it is rightfully yours."

Lakini kwa upande wa Wawakristo, Maandiko yanasema mahari huenda kwa wazazi wa binti na ilitafsiriwa kama "payment made by a man as a gift to the family of a woman he desired to be his wife". Ukisoma Genesis 29, andiko linasema "Jacob loved Rachel and offered to work seven years for her father, Laban, in exchange for her hand in marriage". Na huu ulikuwa ni mfano wa mahari zilizotolewa zamani ktk imani na tamaduni tofauti.

Hitimisho kwa mtazamo wangu
Hivyo, ndugu suala la mahari inakwenda wapi inategemea imani ya dini yako na kama si mtu wa imani sana basi tamaduni za kabila lako husika. Ni ngumu kuelezea moja kwa moja wapi mahari iende kwa sababu ya tofauti za kiimani na kitamaduni.

mie nanyojua huwa wanagwana wanafamilia,kina shangazi wajomba,bibi na wengineo

nakumbuka wakati my sister anaolewa ndio ilikuwaga hivi

kwa mujibu wa uislamu kama alivyojibu braza hapo juu, mahari ni mali ya binti na yeye ndie anapaswa kutamka kiasi au kitu cha kumaanisha mahari agewe ikiwa zawadi kutoka kwa mumewe mtarajiwa, na wala sio ya kuliwa na ndugu na jamaa.
 
mwe mkaja ndio nini na mie wazazi wangu waje kupewa

Hahahahahaahaaa!!!! umenichekesha, anyway, mkaja ni kama zawadi wanayopewa wazazi kama asante yao ya kunizaa , kunilea vizuri mpk nikapata mume, so yule mume anawapa wazazi kuwashukuru.
 
Kwa mujibu wa taratibu na mafundisho ya kiislam, Mahari huwa ni stahiki ya binti.

Mengineyo ni tamaduni na mapenzi binafsi juu ya mgao.

Sawa kabisa!
Matumizi ya mahari hutofautiana dini kwa dini! Tamaduni kwa tamaduni na wakati mwingine hali zetu za kimaisha (umasiki, normal na utajiri) hudertamine ze usage of Dowry!
Moreover utaona kuna wazee wengine hawaathiriwi na tamaduni wala dini, hawa ni Mafyonso wanaweza kupokea na kutumia watakavyo bila ya kuwashirikisha mke, muolewa na wanafamilia kwa ujumla!
Ktk uislamu ni kama alivyoelezea jamaa hapo juu! Ingawa inashauriwa kwa muolewa kutodai pesa hiyo kwa wazazi iwe kama ni bahashishi kwa wazazi wake walivyomlea vizuri hadi akavutia watu na kuolewa!!!
 
Sabah al-kheyri wanaJF, Mara nyingi utamaduni wa kutoa na kupokea mahari huwa baada ya makubaliano kati ya wazazi wa bi Harusi(binti) na Bw.harusi au wahusika wake, Mwenye kupokea mahari huwaga wazazi wa bi.harusi hapo sasa Bi harusi anaambiwa figures tu lakini listi ya programu za shughuli ndizo zinakula mahari yote.[ ..... Sasa hapa kuna faida gani kwa wazazi kama mahari yote itapotelea kwenye hizo programu za shughuli?
 
Sie kwetu mahari hadi walioko vijijini hata kama ni watoto lazima wapewe chao haijalishi ni 200,300 lazima wapewe.

daaah! Tehteh! Umenichekesha aisee ! Hiyo kali!
 
Back
Top Bottom