Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,875
Maharamia wa Somalia wameiteka meli ya yenye bendera ya Panama-iliyokua ikisafiri kutoka Muungano wa Kiarabu ikielekea kwenye bandari mjini Mogadishu.
Meli hiyo ilishambuliwa usiku wakati wahudumu wake walipokua wamelala. Shirika la habari la Anadolu limewanukuu maafisa wa jimbo lililojitenga na Somalia la Puntland.
Maharamia sita walihusika katika shambulio hilo kwa mujibu wa gavana wa eneo la Gardafu katika jimbo la Puntland, Musse Salah, ambaye alinukuliwa na Shirika la habari la Reuters.
Maafisa wa eneo la Bari ambako tukio hilo lilitokea wanasema kuwa meli hiyo ilipatwa na matatizo ya kiufundi.