Mahakama ya rufaa yaiamuru TANESCO iwalipe DOWANS

3squere

JF-Expert Member
Aug 2, 2011
925
181
Na Flora Mwakasala

MAHAKAMA ya Rufaa imetupilia mbali ombi la Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) la kusimamisha utekelezaji wa hukumu ya Mahakama Kuu, iliyoamuru wailipe Sh bilioni 94 kampuni ya Dowans.

Katika ombi hilo Tanesco walidai kuwa fedha hizo walizoamriwa kulipa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) kutokana b kukatisha mkataba kinyume cha sheria ni nyingi na hawana uwezo wa kulipa.

Aidha wanadaia kuwa, kama watatekeleza hukumu hiyo, itaathiri uwezo wake wa kuzalisha na kusambaza umeme nchini na hivyo kusababisha tatizo kubwa la ukosefu wa umeme, ambao utaathiri uchumi wa nchi kwa jumla.

Katika hoja zao, walidai kuwa tayari walishawasilisha nia ya kukata rufaa kupinga hukumu hiyo na ya Mahakama Kuu na wanaamini watashinda rufaa hiyo.

Akisoma uamuzi huo jana, Naibu Msajili wa mahakama hiyo Elizabeth Mkwizu, alitupa ombi hilo na kuiamuru kwa kuwa waliwasilisha ombi hilo nje ya muda unaotakiwa kisheria.

Mahakama hiyo ilikubaliana na hoja za Wakili wa Dowans Kennedy Fungamtama aliyedai ombi hilo lilipaswa liwasilishwe katika muda wa siku 60 tangu kutolewa kwa hukumu, lakini badala yake Tanesco iliwasilisha maombi hayo baada ya siku 351.

Septemba 28, mwaka juzi, Mahakama Kuu iliiamuru Tanesco kuilipa Dowans fidia ya Sh biloni 94 na riba ya asilimia 7.5 baada ya kukubali kuisajili tuzo ya Dowanc.

Katika hukumu ya Mahakama ya ICC, iliyotolewa Novemba 15 mwaka juzi, Tanesco iliamriwa kuilipa Dowans Holding SA na Dowans Tanzania Ltd (Dowans) dola za Marekani milioni 65, pamoja na riba na gharama za kuendesha kesi, baada ya kuvunja mkataba na kampuni hiyo kinyume cha sheria.

Hata hivyo, Tanesco ilipinga hukumu hiyo lakini Septemba 28 mwaka jana, Jaji Emilian Mushi wa Mahakama Kuu, alikubali kusajili tuzo ya malipo ya Dowans na kuiamuru Tanesco kulipa fedha hizo pamoja na gharama za uendeshaji kesi.

Baada ya hukumu hiyo Tanesco iliwasilisha ombi la kibali cha kukata rufaa kupinga hukumu hiyo na ombi la kusimamisha utekelezwaji wa hukumu hiyo.

Hata hivyo Februari 20, mwaka jana , Mahakama ilitupilia mbali ombi la kibali cha kukata rufaa na Septemba 6, 2012, pia mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi la kusimamisha utekelezwaji wa hukumu hiyo.

Kutokana na uamuzi huo, ndipo Tanesco wakafungua ombi la kusitisha utekelezaji wa hukumu hiyo katika Mahakama ya Rufaa, huku wakitoa hoja walizozitoa katika ombi la Mahakama Kuu.

Kwa mujibu wa Wakili wa Dowans, Kenedy Fungamtama, hadi kufikia Novemba mwaka jana, deni la Dowans lilifikia zaidi ya Sh bilioni 122 kutokana na kuongezeka kwa riba ya asilimia 7.5 ya deni la awali la kila siku.

Mwisho.
 
Mahakama ya rufaa imetoa hukumu na kuiamuru TANESCO iilipe kampuni ya DOWANS kiai cha Dola za kimareni milioni 122 kama fifidia ya kukatisha mkataba.

Kiasi hicho ni ongezeko la jumla ya Dola milioni 58 ambapapo awali TANESCO ilitakiwa kulipa kampuni hiyo Dola 65 milioni baada ya mahakama kuu kutoa amri hiyo mwaka 2011.

Ongezeko hilo ni kutokana na riba iliongezeka kufuatia TANESCO kukata rufaa.

CHANZO: MWANANCHI
 
Hizi movie za Magogoni kujilipa kupitia mahakama licha ya kuapa kwamba hawaifahamu Dowans inayosadikiwa kuwa ni kampuni hewa, hakika kuna gharama inakisubiri CCM huko mbeleni kwenye debe.
 
Wanabodi,
Sisi wengine tulisema tangu mwanzi kuwa hili la Dowans, halikwepeki!, tulinyooshewa vidole hadi kutukanwa kuwa hatuna uzalendo!. Wajameni, dawa ya deni ni kulipa tuu!.

Niwakumbushe kidogo mlolongo mzima na mwisho wa siku, deni litalipwa!.

  1. Game lilianza rasmi 1995 baada JK na EL kutoswa kwenye urais, wakaunganisha nguvu, "stand together, fight together", as one, hivyo kuunda rasmi mtandao!. The Master Mind was "The King Maker!"
  2. Tangu mwanzo the plan was JK rais, EL, PM!, ndani ya mtandao kuna watu "safi" wakadai EL ni "too dirty", hivyo wakampendekeza 6 ndie awe PM!.
  3. Baada ya ushindi wa kishindo wa JK, he had no option bali kusikiliza zile sauti za "who paid the piper, had to call the tune!", na kwa kusingatia walipoamzisha Boys II Men tangu 1995, JK akakumbuka fadhila, akamuimbua EL as PM!. 6 na wengine waliojiita "wasafi" waka mind!.
  4. The King Maker, akamng'oa Msekwa kwenye us Spika na kumzawadia 6 as consolation ya kuukosa u PM, wakijua yamekwisha!. Kumbe wapi!.
  5. Kulipotokea dili la umeme wa dharura, "Jamaa" mwenyewe alitia timu, ndipo Richmond ikazaliwa!, na baada ya koboronga, ndipo "The King Maker" akaokoa jahazi kwa kuileta "Dowans" ili ku save face ya "jamaa!", na kiukweli, Dowans walifua umeme kweli!.
  6. Kwa vile 6 bado alikuwa na usongo wa kuukosa u PM, na kumepatikana kiji opportunity cha kumfix EL, ili atoswe na yeye eteuliwe!. 6 kwa kumtumia Mwaki, wakatimiza lengo, tena kwa kuhakikisha EL hahojiwi wala kuulizwa chochote, bali kusukumiwa zigo zima zima just to save the face ya "Jamaa!", na El angekohoa, nyumba nzima ingeporomoka na wangekosa wote!.
  7. Ilimbidi EL kukubali matokeo na kuwapa walichotaka na yeye kujikalia kimya, pembeni!, na kuvumilia dhihaka, matukano, kubeswa na matusi ya kila aina!, na alivumilia yote, kama yule aliyewambwa msalabani!. Si wengi wanaoelewa ni kwa kuteswa kwake, CCM ilipona!.
  8. Ni kufuatia ripoti ile, mkataba halali wa Dowans ulisitishwa kwa sababu za kijinga kabisa!. ZZK kupitia kamati yake ya POC alishauri, kama tumevunja mkataba, bora basi tuinunue mitambo ile tuendelee kuzalisha umeme!, na kama hija za kuuvunja mkataba, ni kosa la Dowans, then, bora tuitaifishe mitambo ya Dowans, iwe mali ya umma!. Kwa mnao kumbuka, mtakumbuka waliopinga kwa nguvu zao zote!.
  9. Dowans wakafungua kesi ICC, wakashinda!, mkataba ukaletwa humu jf, watu tulipouona tuu tukasema wazi, hakuna pa kutokea!. Dawa ni kulipa the sooner the better!. Hatukulipa tukaendelea kudanganywa sasa deni limeongezeka mara dufu na lazima tulipe!.
  10. Tanzania ni nchi ya ajabu sana!, tunaviongozi wa akili za panzi kweli kweli!, Tumevunja mkataba wa Dowans, tumeingia mkataba ule ule na Simbion, kwa masharti yale yale ya Dowans!. Nunueni mashine basi muendelee kuzalisha umeme! eti "hatununui mashine kuu kuu!" na sasa tumepitisha sheria ya kununua mashine kuu kuu!. Wakati wote mitambo ya Dowans imezimwa, tuliwasha mitambo ya IPTL kwa gharama ya mara kumi ya mitambo ya Dowans!, na uchafuzi mkubwa wa mazingira on top of that!. Sasa hizi ni akili au matope?!.
  11. Sasa maandamu Tanesco wameamriwa rasmi kulipa!, na aliyeiponza Tanesco ni serikali, hivyo kiukweli, na hali halisi ilivyo sasa, Tanesco haina "capacity to pay!", hivyo deni litalipwa na serikali!, hii ikimaanisha fedha za kulipa deni hilo zitatokana na kodi zetu!, jiandaeni kufunga mikanda kwa kuongezwa gharama katika maeneo mbalimbali hadi fedha za kulipa Tozo ya Dowans zipatikane!.
  12. Pia namshauri EL, now its about time atoke to the open, aweke wazi his role kwenye Richmond, ili Watanzania wamjie who is the real beneficiary of "tozo ya Dowans!", kwa kuendelea kukaa kimya, "he has everything to loose and nothing to gain!" lakini kwa kumtaja sasa, "he'll have everthing to gain and nothing to loose!", kwa sababu, 2015, yeye sio mgombea!. He'll save his face, his party and his nation!.

Mungu Ibariki Tanzania.

Jumapili Njema!.

Pasco.
 
Pasco mimi ni moja ya watu tuliopinga sana hoja ya Zitto humu lakini kwa hili lazima nikubali Zitto aliona mbali na si kwa jicho la kisheria kama wewe Pasco bali danadana za kisiasa na falsafa za upepo kupita!

Tunaelekea kushindwa kila jambo na kelele zetu zimebaki historia!

Yuko wapi Sitta na Mwakyembe waliohaidi kujiuzulu wakilipa?

Nini msimamo wa tegemeo lililobaki Chadema?
 
Last edited by a moderator:
Nauli wameanza kupandisha. Kumbuka kupanda kwa nauli means kila kitu kitapanda ili pesa zipatikane kuilipa Dowans. Ndiyo Tanzania hiyo-INAJENGWA NA WENYE NGUVU INALIWA NA WENYE MENO.
 
Hiyo ndio serikali sikivu ya ccm na bunge lao lenye kujali kulindana kichama kuliko maslahi ya taifa
 
Spika wakati huo alikuwa mwanasheria,ambaye alibadilika badala ya kuonyesha impartiality akawa mshabiki na kusahau ethics za kisheria. Mwenyekiti wa probe committee alikuwa mwanasheria tena aliyebobea kufundisha chuo kikuu cha Dar es salaam.Najua baadhi ya wabunge waliokuwa wanashabikia tendo hilo hawakujua hatari ambayo ingetokea kwa kuvunja mkataba kwa sababu wengi wao si wanasheria.

Nadhani kwa hawa wawili waliongozwa sana na personal whims na kutufikisha hapa tulipo.Nasema hivyo kwa sababu kwa mwanasheria kabla hujafikia kuvunja mkataba lazima ujue matokeo yake ya baadaye na utachukua uamuzi huo tuu pale ambapo unajua uwezekano wa kushinda shauri hilo likienda mahakamani ni asilimia kubwa sana.Najua hata mtu aliyesoma basic ya law of contract mwaka wa kwanza chuo kikuu chochote nchini atakuwa anajua effects of breach of contract.

Haya sasa tanescco ikilipa hilo deni pindi ampapo DOWANS watakapoomba enforcement sijui umeme tutaupata tena? Wakati huo waliotufikisha hapa tulipo wanasema Walikuwa na spidi na viwango? na wengine wakasema wanafahamu vizuri natural justice na wamefundisha chuo kikuu miaka mingi na kuzitaja kwa kilatini NEMO JUDEX----,AUDI ALTERAM----NA NULLUM ALBITRIUM----- wakati kwenye hiyo probe comitee hayakuwepo? Kazi ipo hii ndio TZ ya kisiasa
 
Tatizo kuu hapa ni kwamba chakula hiki kilipikwa bila kuiva vizuri!
1. Mwakyembe aliacha baadhi ya masuala ili kufunika aibu ya Serikali. Laiti angefungua "Pandora Box" hapa tungekuwa tunaongelea mambo mengine kabisa!
2. Mwakyembe huyo huyo alimkwepa kumhoji Lowassa, sijui kwa maslahi yake binafsi au ya nani? Laiti angemhoji angefungua "Pandora Box" nyingine, tungefunguliwa macho!
3. Lowassa naye alifungua kinywa nusu kwa kudai eti "ni Uwaziri Mkuu!" Hakutuambia kuwa nani hasa aliyekuwa anautaka huo Uwaziri Mkuu. Laiti angeenda extra mile tungepata mengi zaidi!
4. Msabaha naye alifunguka kiduchu akidai eti "huu ni mradi wa wakubwa!" Laiti angefunguka zaidi ngoma hii ingekuwa inachezwa tofauti kwa sasa!
5. JK naye akaibuka akidai kuwa "siijui kabisa Dowans!" Hii ndio ilikuwa funga mwaka. Laiti angefunguka zaidi tungetolewa tongotongo maana kitu imeundiwa hata Kamati teule ya Bunge, mwenye nyumba akadai kuwa "ni michezo ya watoto tu mimi siijui!"
6. Lowassa aliibuka tena walipotaka "kumvua gamba" akidai kuwa YOTE aliyokuwa anayafanya kuhusu Richmond yalikuwa na "Baraka" za Magogoni! Hapo tena inatukumbusha juu ya hadithi za "Mradi wa Wakubwa" za Msabaha!!

Clips ni nyingi na bahati mbaya zitatoa hilights tu! Hiki chakula kimepikwa nusu nusu makusudi ili mkitaka kukila tu mnaogopa kuvimbiwa mnakiacha!
Katika background hii sishangai hata kidogo kwa Mahakama zetu kuwa pia compromised kama ilivyokuwa kwa kesi ya Mgombea Binafsi ili ile dhana ya "mradi wa wakubwa" iweze kusimama!
 
Khe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee JK hongera sana ipo siku, malipo hapa hapa duniani.
 
Hizi movie za Magogoni
kujilipa kupitia mahakama licha ya kuapa kwamba hawaifahamu Dowans
inayosadikiwa kuwa ni kampuni hewa, hakika kuna gharama inakisubiri CCM
huko mbeleni kwenye debe.

hapo mi ndio nachanganyikiwa rais alishasema hawajui dowans na wala hiyo kampuni haipo sasa inakuwaje tunajipa kampuni hewa jamani au mimi ndio sielewi.
 
hapo mi ndio nachanganyikiwa rais alishasema hawajui dowans na wala hiyo kampuni haipo sasa inakuwaje tunajipa kampuni hewa jamani au mimi ndio sielewi.

Khe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee JK hongera sana ipo siku, malipo hapa hapa duniani.

Kuna siku itafika hakika hawa maskini wanaoLALIWA na wachache bila ridhaa yao watachoka!

Nauli wameanza kupandisha. Kumbuka kupanda kwa nauli means kila kitu kitapanda ili pesa zipatikane kuilipa Dowans. Ndiyo Tanzania hiyo-INAJENGWA NA WENYE NGUVU INALIWA NA WENYE MENO.


Mambo yamefika huku kote kwa sababu ya watu kama nyinyi ambao hamjui mipaka kati ya siasa na sheria. Dowans ilishatoku kuwa jambo la kisiasa, sasa hivi ni jambo la kisheria...
 
Mambo yamefika huku kote kwa sababu ya watu kama nyinyi ambao hamjui mipaka kati ya siasa na sheria. Dowans ilishatoku kuwa jambo la kisiasa, sasa hivi ni jambo la kisheria...
Chanzo cha haya mambo ni nini na waasisi wake ni viongozi wa chama gani? Naomba unijibu swali langu tafadhali
 
Mnakumbuka ushauri wa Zitto?

Hatukumbuki. Endelea kutetea magamba kama kawaida yako.

Kwa hili ccm na magamba ni adui zangu, ni adui wa watanzania waelewa wa sakata hili.

Hivi kwa nini jk asijiuzuru? maana alisema wamiliki wake hawajui mbele ya umma wa magamba nec dodoma. Serikali kupitia taneso inamplipa nani? tiss/mahakama/jeshi mmewaachia magama wawaumize watanzania? Haki hiko wapi?
 
Hatukumbuki. Endelea kutetea magamba kama kawaida yako.

Kwa hili ccm na magamba ni adui zangu, ni adui wa watanzania waelewa wa sakata hili.

Hivi kwa nini jk asijiuzuru? maana alisema wamiliki wake hawajui mbele ya umma wa magamba nec dodoma.

Fikra kama hizi zako ndio zilizosababisha tozo kuongezeka kutoka USD mil 58 mpaka USD mil 122. Mijadala ingefanyika sanely, dowans wangekuwa wameshalipwa na sasa tungebaki tunajadili nani wa kumuadhibu.

Jifunzeni busara inayosema "the fox must be chased away before the chicken is warned not to go into the bush"
 
Chanzo cha haya mambo ni nini na waasisi wake ni viongozi wa chama gani? Naomba unijibu swali langu tafadhali

Chanzo cha haya mambo ni UBISHI na tabia ya kupinga kila jambo linalosemwa na watu fulani.

USHABIKI umeshamiri kwenye mambo ya kitaalam ya sheria, gharama zake ndio hizi...
 
Fikra kama hizi zako ndio zilizosababisha tozo kuongezeka kutoka USD mil 58 mpaka USD mil 122. Mijadala ingefanyika sanely, dowans wangekuwa wameshalipwa na sasa tungebaki tunajadili nani wa kumuadhibu.

Jifunzeni busara inayosema "the fox must be chased away before the chicken is warned not to go into the bush"

Kwako usd mil 58 zilikuwa kidogo na uliona inafaa serikali yako kupitia tanesco walipe kampuni hewa?
 
Kwako usd mil 58 zilikuwa kidogo na uliona inafaa serikali yako kupitia tanesco walipe kampuni hewa?

Umekataa kununua mitambo ukapigwa fine ya mil. 58. Umekataa kulipa kwa sababu za kisiasa sasa hivi imefika mil 122. Bado unaendeleza ubishi.

Sijui unataka Mungu akutumie malaika wa kuiamsha saneness yako ili ujue kuwa kadri unavyozidi kupoliticise swala hili la kisheria ndivyo unavyozidi kuingia gharama zaidi!!!
 
Back
Top Bottom