From HEAVERN
Member
- Jun 8, 2014
- 25
- 3
Jamani naomben mnisaidie mimi sijaelewa suala la mahakama ya kadhi limepitishwa au vipi?
hahahaha nilimsikiliza sana kwa makini Chenge lakini sikuambulia lolote na PHD yangu. Amemungunyamungunya maneno na kuliacha likielea. Hakusema imewekwa au haijawekwa. Inaonekana hili limewawia gumu.
PHD ni aina ya king'amuzi kama TING HD au ni kama zile degree za Kainerugaba?hahahaha nilimsikiliza sana kwa makini Chenge lakini sikuambulia lolote na PHD yangu. Amemungunyamungunya maneno na kuliacha likielea. Hakusema imewekwa au haijawekwa. Inaonekana hili limewawia gumu.
Litakuwa halijawekwa.Kawaacha watu njia panda anajua wengi hawatasoma Rasmu wengi watasema ndiyooooo hata bila kusoma
Hakuna kitu kama hicho soma ibara ya 40Hehehehe, embu someni, mahakama ya kadhi imepitishwa kwenye katiba. tusubiri kuipigia kura ya ndio au hapana lakini imo kwenye katiba
Hakuna kitu kama hicho soma ibara ya 40
Uhuru wa imani ya
dini
40.-(1) Kila mtu ana uhuru wa mawazo, dhamiri, imani na uchaguzi
katika mambo ya imani ya dini na anao uhuru pia wa kubadilisha dini, imani
yake au kutokuwa na imani na dini.
(2) Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni
huru na jambo la hiari kwa mtu binafsi ilimradi hakiuki sheria za nchi.
(3) Shughuli ya uendeshaji wa jumuiya za dini itakuwa nje ya shughuli
za mamlaka ya Serikali.
Kadh ateuliwe huko msikitini!
Huo mfumo wa banking si kwamba wenye mabank wanawapenda sana waisilamu, kikubwa hapo ni kwamba wanazipenda hela zao zaidi. Hapo wapo kibiashara zaidi, na wanajua namna ya kujipatia faida kupitia account za namna hiyo... Kama wanavyoanzisha Islamic banking bila kulazimishwa na hukum za Kiislam zingine zitashamiri kutokana na wao hao wapinga Uislam bila kulazimishwa.
Kuwepo au kutokuwepo kadhi si jambo la kuurudisha nyuma au kuupeleka mbele Uislam.
Waislam tutasonga mbele bila fujo na ukifika wakati, licha ya katiba, hukum zote zitakuwa za Kiislam, tena wataanza wao wenyewe, kwani Uislam ndio njia pekee ya kuishi hapa duniani na akhera.
Kama wanavyoanzisha Islamic banking bila kulazimishwa na hukum za Kiislam zingine zitashamiri kutokana na wao hao wapinga Uislam bila kulazimishwa.