NakuliliaTanzania
JF-Expert Member
- Sep 24, 2007
- 555
- 7
Wakuu, wakati tunaendeela na mijadala ya mafisadi, kuna hili la mahakama ya kadhi
Nakumbuka siku zilizopita hapa tulikuwa na mjadala mzito kuhusu hili, na reent development zinaonyesha kuwa kesi hii aliyokuwa amefungua Mtikila, imefutwa na mahakama kuu,
Kilichonifanya nilete hii hoja hapa ni kutaka ufafanuzi wa maana na implication ya hii hukumu,
Je, ndo kusema mjadalaumefungwa,?
Kwa vile kesi imefutwa, bila kusikiliza hoja za mtikila za kwa nini mahakama hiyo isiwepo, na hasa uwepo wake ukiwa na mkono wa serikali isiyo na dini,na
Kwa vile Mtikila katika utetezi wake inaonekana alikosa milioni 4 za kumilipa wakili, na
kwa vile wanaharakati hawakujitokeza kumtetea/kumsaidia katika hili,
Ndio kusema kuwa:
Serikali sasa inaweza kuendela na mchakato wa kuanzaisha mahakama hiyo? au wakuu am missing apoint? naombeni msaada wenu maana honestly mi sio mwanasheria.
Nakumbuka siku zilizopita hapa tulikuwa na mjadala mzito kuhusu hili, na reent development zinaonyesha kuwa kesi hii aliyokuwa amefungua Mtikila, imefutwa na mahakama kuu,
Kilichonifanya nilete hii hoja hapa ni kutaka ufafanuzi wa maana na implication ya hii hukumu,
Je, ndo kusema mjadalaumefungwa,?
Kwa vile kesi imefutwa, bila kusikiliza hoja za mtikila za kwa nini mahakama hiyo isiwepo, na hasa uwepo wake ukiwa na mkono wa serikali isiyo na dini,na
Kwa vile Mtikila katika utetezi wake inaonekana alikosa milioni 4 za kumilipa wakili, na
kwa vile wanaharakati hawakujitokeza kumtetea/kumsaidia katika hili,
Ndio kusema kuwa:
Serikali sasa inaweza kuendela na mchakato wa kuanzaisha mahakama hiyo? au wakuu am missing apoint? naombeni msaada wenu maana honestly mi sio mwanasheria.
Mahakama Kuu yafuta Kesi ya Mahakama ya Kadhi Tanzania Na Tausi Ally
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam imeifuta kesi ya kikatiba ya kupinga kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi iliyofunguliwa na Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila.
Uamuzi wa kufuta kesi hiyo, ulifanywa na jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo wakiongozwa na Jaji Kiongozi, Salum Masati aliyesaidiwa na Jaji Robert Makaramba na Jaji Aisha Nyerere baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwasilisha pingamizi la kutaka kesi hiyo ifutwe.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, aliwasilisha ombi la kufutwa kwa kesi hiyo, Novemba 15, mwaka jana akitaka kesi hiyo ifutwe na pia kumtaka Mchungaji Mtikila kujibu hoja hiyo.
Naye Mchungaji Mtikila aliwasilisha ombi katika mahakama hiyo, kuongezewa muda ili aweze kujibu hoja ya kufutwa kwa kesi hiyo na majaji walimruhusu na kupanga kusikilizwa maombi yake ya kutaka kuongezwa muda Februari 26, mwaka huu.
Baada ya ombi la Mchungaji Mtikila la kuongezewa muda, alifika katika mahakama hiyo na kuomba aongezewe muda mwingine kwa madai kuwa alikuwa hana wakili.
Wakili wa Serikali, Nickson Ntimbwa aliiomba mahakama itupilie mbali maombi ya Mtikila kwa madai kuwa ombi lake la kutaka aongezewe muda lilipangwa vibaya.
Mbali na ombi hilo, Ntimbwa aliiomba mahakama imwajibishe kwa kutofuata taratibu za kimahakama na kwamba ikiwezekana atiwe hatiani kwa kuidharau mahakama na kulipa faini.
Mchungaji Mtikila alijitetea akisema kuwa alijitahidi kufuata taratibu za mahakama, lakini alikuwa hana Sh4 milioni kwa ajili ya kumlipa wakili wa kumsaidia katika kesi hiyo.
Mtikila alidai kuwa mbali na ukosefu wa fedha mawakili na taasisi za haki za binaadamu walikuwa hawajisikii kumwakilisha katika kesi hiyo kwa ajili ya kumtetea.
Mchungaji Mtikila alifungua kesi hiyo, Oktoba 23, 2007 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, akipinga kuanzishwa kwa mahakama hiyo.
Mtikila alifungua kesi hiyo kufuatia suala la kuanzishwa Makahama ya Kadhi kuwemo kwenye ilani ya uchaguzi (ya CCM) ya mwaka huu, ambayo inatumiwa na Serikali ya Awamu ya Nne kufikia malengo yake ya kuwapa maisha bora Watanzania.
Suala hilo pia liliwahi pingwa na maaskofu wote nchini kwa maelezo kuwa lina mwelekeo wa upendeleo kwa dini moja na kwamba linaweza kusababisha mgawanyiko wa kidini nchini
http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=4856