Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,234
Mahakama Kuu ya Zanzibar, Masjala ya Tunguu, mbele ya Mheshimiwa Jaji Salma Hassan, leo imetoa Amri ya Muda ya Kusitisha Kitendo (Status Quo) katika Maombi Madogo ya Madai Na. 18 ya Mwaka 2026.
Amri hiyo imesimamisha rasmi mpango wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) wa kuharibu vifaa na nyaraka za uchaguzi.
Waombaji, ambao ni wadai katika Mashauri ya Uchaguzi Na. 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12, 13, 14, 15, 16, 17 na 18 ya Mwaka 2025, waliwasilisha maombi hayo chini ya Hati ya Dharura.
Hatua hiyo imekuja kufuatia tangazo la ZEC kwa umma likielezea nia ya kuteketeza nyaraka zote za uchaguzi wa mwaka 2025.
Akizingatia uzito wa suala hilo na uwezekano wa kutokea kwa madhara yasiyoweza kurekebishika katika mchakato wa utoaji haki, Mheshimiwa Jaji ameamuru kudumishwa hali ya sasa (Status Quo).
Mahakama imeelekeza kuwa nyaraka zote za uchaguzi zibaki kama zilivyo hadi pale maombi hayo yatakaposikilizwa kwa pande zote mbili (inter partes).
Kusoma zaidi
Amri hiyo imesimamisha rasmi mpango wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) wa kuharibu vifaa na nyaraka za uchaguzi.
Chimbuko la Shauri
Waombaji, ambao ni wadai katika Mashauri ya Uchaguzi Na. 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12, 13, 14, 15, 16, 17 na 18 ya Mwaka 2025, waliwasilisha maombi hayo chini ya Hati ya Dharura.
Hatua hiyo imekuja kufuatia tangazo la ZEC kwa umma likielezea nia ya kuteketeza nyaraka zote za uchaguzi wa mwaka 2025.
Uamuzi wa Mahakama
Akizingatia uzito wa suala hilo na uwezekano wa kutokea kwa madhara yasiyoweza kurekebishika katika mchakato wa utoaji haki, Mheshimiwa Jaji ameamuru kudumishwa hali ya sasa (Status Quo).
Mahakama imeelekeza kuwa nyaraka zote za uchaguzi zibaki kama zilivyo hadi pale maombi hayo yatakaposikilizwa kwa pande zote mbili (inter partes).
Kusoma zaidi