Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Mahabusu wajisaidia porini kwa kukosa vyoo
na Stephano Mango, Nyasa
MAHABUSU wa Kituo cha Polisi Lituhi, wilayani Nyasa, mkoani Ruvuma wanajisaidia porini kutokana na ukosefu wa vyoo na maji, hali inayoweza kusababisha mlipuko wa magonjwa mbalimbali.
Wakizungumza na Tanzania Daima jana kwenye eneo la kituo hicho cha polisi, mahabusu hao ambao hawakutaka majina yao yatajwe walieleza kuwa pindi wanapotaka kujisaidia huwajulisha askari waliopo zamu kituoni hapo ili wawapeleke vichakani kujisaidia.
Waliongeza kuwa wakati mwingine hulazimika kuwaomba ndugu zao kuwaletea maji ya kunywa na kuoga kwa madai kuwa kituo hicho hakina maji tangu kilipojengwa wala huduma nyingine muhimu kwa afya za binadamu.
Baadhi ya askari wa kituo hicho ambao hawakutaka kutajwa majina yao gazetini walikiri kuwepo kwa tatizo hilo pamoja na nyumba za kuishi, hivyo wamehifadhiwa kwenye nyumba za raia waliopo jirani na kituo hicho.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamhanda, alikiri kuwepo kwa matatizo hayo na kusema kuwa yapo kwenye utekelezaji.
na Stephano Mango, Nyasa
MAHABUSU wa Kituo cha Polisi Lituhi, wilayani Nyasa, mkoani Ruvuma wanajisaidia porini kutokana na ukosefu wa vyoo na maji, hali inayoweza kusababisha mlipuko wa magonjwa mbalimbali.
Wakizungumza na Tanzania Daima jana kwenye eneo la kituo hicho cha polisi, mahabusu hao ambao hawakutaka majina yao yatajwe walieleza kuwa pindi wanapotaka kujisaidia huwajulisha askari waliopo zamu kituoni hapo ili wawapeleke vichakani kujisaidia.
Waliongeza kuwa wakati mwingine hulazimika kuwaomba ndugu zao kuwaletea maji ya kunywa na kuoga kwa madai kuwa kituo hicho hakina maji tangu kilipojengwa wala huduma nyingine muhimu kwa afya za binadamu.
Baadhi ya askari wa kituo hicho ambao hawakutaka kutajwa majina yao gazetini walikiri kuwepo kwa tatizo hilo pamoja na nyumba za kuishi, hivyo wamehifadhiwa kwenye nyumba za raia waliopo jirani na kituo hicho.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Michael Kamhanda, alikiri kuwepo kwa matatizo hayo na kusema kuwa yapo kwenye utekelezaji.