Magufuli: Subirini ushindi wa Tsunami

Magufuli: Subirini ushindi wa Tsunami

Wana CCM tusijitie unyonge kwa kelele za UKAWA ushindi ni wetu kwa namna wagombea wetu wanavyouzika huko majimboni. Tujiandae na sare zetu kusubiria kuapishwa kuanzia Rais, wabunge na madiwani.
Safari hii uwanja wa Taifa hautatosha kumwapisha Magufuli.Magufuli kura atakazopata zitavunja rekodi ya maraisi wote kasoro Nyerere.Atapata kura ailimia 80 kwenda juu.
 
is
 
raisi wa twaweza,ama kweli wanawake wakiwezeshwa wanaweza
 
Hawa wahuni wa Ukiwa hawakuamini kule Dodoma wakati mtu alipokatwa mbichi mbichi, sasa wasubiri waone kama kiziwi uisikia filimbi ama la
 
Mgombea wa Urais kupitia CCM amesema katika ziara zake mikoani katika mikutano ya kampeni maelfu ya wanainchi wamekuwa wakijitokeza na kumpatia pongezi tele za ushindi wake. Amezidi kusisitiza ushindi wa mwaka huu ni zaidi ya Sunami.
 
Twaweza wametukana wasomi na kuwadhalilisha.Watu waweke vitu kwa uhalisia ndicho tunachotaka na sio kuhongwa kulikozoeleka CCM hii haibebeki kamwe kila mwenye macho anaona kuwa watanzania wameamua na hawarudi nyuma.ujinga mtupu ulioandikwa na Twaweza,najua waandishi wa huo utafiti wanajinasibu kuwa wasomi,sasa kwa halihii isiyozingatia uhalisia inaonyesha wazijanga lililopo ktk ELIMU yetu na kunakila sababu ya watu hawa kunyang'anywa udokta,uprofesa,na degree zao ili wabaki FORM SIX WA KAWAIDA,maana kilichofanyika ni udhalilishaji wa ELIMU.Propaganda za kijinga na kipumbavu hazina nafasi kwa sasa.Rais ni Lowasa hilo halipingiki wa kujifunza ujasiriamali aanze sasa maana uwaziri tulio ahidiwa ndani ya CCM haupo.
 
Kama heading iliovyotangulia naona ushindi mkubwa sana katika uchaguzi huo,DHIDI YA VYAMA PINZANI TZ na sababu kubwa ni kwamba;
1. CCM inahazina kubwa ya washabiki lukuki wasomi,wataalamu wa siasa 'wazee,vijana wa kati wenye ajira za kudumu na wachache wasio na ajira rasmi ,wanao- ishi mijini na vijijini.
vyama pinzani vimeonyesha kukita mizizi mijini na hasa miji mikubwa.

2. CCM INA MATAWI NA WANACHAMA inchi nzima kuanzia kijijini hadi makao makuu wakati baadhii ya vyama hawana hata ofisi vijijini wala mijini na wapo dar tu na sehemu walikozaliwa tu.

3. CCM ina mikakati na mbinu za ushindi zinazochangiwa na hazina kubwa ya raslimali watu na mikwanja ya kutosha inayotoka na vitegauchumi vingi vya chama,huku vyama pinzani vikiwa havina hata magari ya kufanyyia kampeni na kuwafikia watu wengi vijijini na huku campain zao zikijikita zaidi kuing'oa CCM bila kujua wataing'aje

Na ww ukipenda ongeza yako;
by
Mawazo huru
 
ccm imesahau majukum yake ya kuisimamia serikali ili iwahudumie wananchi zaidi ya kutumia nguvu kubwa kujilinda ili kiendelee kubakia madarakani kwa gharama yoyote huku wananchi wakiwemo wengi wa wanachama wake wakibakia hoi bin taabani kwa ufukara na umaskini uliopiga kambi kukiwa na matumaini hafifu sana ya huo umaskin kuondoka
 
CCM imerudishwa kwa wazalendo na wanyonge walioijenga.
CCM imeondolewa kwenye makucha ya matajiri na mafisadi na sasa ccm ni wamoja kama mchwa.
 
CCM imerudishwa kwa wazalendo na wanyonge walioijenga.
CCM imeondolewa kwenye makucha ya matajiri na mafisadi na sasa ccm ni wamoja kama mchwa.
kwa akina magufuri wauzaji nyumba za serikal , joka lenye makengeza, millions of money aka hela ya mboga, mwakyembe mabebewa fake?. kama ni hivyo twafaaaa!.
 
CCM imerudishwa kwa wazalendo na wanyonge walioijenga.
CCM imeondolewa kwenye makucha ya matajiri na mafisadi na sasa ccm ni wamoja kama mchwa.

Hilo sina hakika, ila kwakupenda au kutopenda imejikuta inatupatia mzalendo, komesha ya mafisadi naye akatuvuta wazalendo wote kama sumaku
 
CCM imerudishwa kwa wazalendo na wanyonge walioijenga.
CCM imeondolewa kwenye makucha ya matajiri na mafisadi na sasa ccm ni wamoja kama mchwa.

Jingalao Toroka Uje.Juma lijalo utabadili gia mpaka akina Lizaboni.na Mr Chin hawataamini kama nawe umesaliti CCM
 
walichoweza ni kufanya kile kinachowasaidia kutufanya watz tuwe na akili finyu ya kufikiri kwa kupuuza elimu watoto wetu humaliza darasa la saba wengi wao hawawezi kufanya mitihani ya darasa la pili. wizara ya elimu inatengewa 1% tu ya pato la nchi wakati South Africa inatenga 30% matokeo yake tuna taifa ambalo haliwezi kushndana na wenzetu na kwa huo mwelekeo tutapitwa sana tunaenda kwa tractor wakati wenzetu wametangulia na cruser eti tunaota tutawapita! inauma sana CCM NI AINA YA JANGA LA HATARI SANA LINAANGAMIZA TAIFA.
 
kama hiyo haitoshi wazee wangu kijijini walikopwa mazao yao na serikali wakati yenyewe haijawahi kuwakopesha pembejeo wala pesa ya kuwasaidia kufanya kazi za shamba wakati huo mwaka uliotangulia iliwapiga marufuku wasiuze mazao yao nje ya nchi hivyo wakauza kwa bei za kutupa. CCM ISHAWAGEUZA WANANCHI KUA SHAMBADARASA
 
SIKU moja baada ya matokeo ya utafiti wa taasisi huru ya Twaweza kuonesha kuwa anapaa katika urais, mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli ametamba kupata ushindi wa ‘tsunami’.

“Aliamua kutembea kwa gari, kutembea katika barabara mbovu, kwani uwezo wa kutembea na helikopta anao, angeweza kwenda kwa helikopta, lakini aliamua kutembea ili kujionea hali halisi, ili akifika Ikulu akumbuke shida za Watanzania na akafanye kazi ya kuwatumikia,” alisema Dk Magufuli.
 
SIKU moja baada ya matokeo ya utafiti wa taasisi huru ya Twaweza kuonesha kuwa anapaa katika urais, mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli ametamba kupata ushindi wa ‘tsunami’.

“Aliamua kutembea kwa gari, kutembea katika barabara mbovu, kwani uwezo wa kutembea na helikopta anao, angeweza kwenda kwa helikopta, lakini aliamua kutembea ili kujionea hali halisi, ili akifika Ikulu akumbuke shida za Watanzania na akafanye kazi ya kuwatumikia,” alisema Dk Magufuli.

Kutamba sio kushinda
 
Back
Top Bottom