Kabla ya Kuzungumza dhumuni Kubwa La Post Hii Napenda Niweke wazi Kuwa, Kwa Miaka Mingi, Kuwashinda hata wengi wa wanaCCM, Nilitambua Uwezo Mkubwa wa Magufuli wa Kufanya Kazi. Nilikuwa na Shukurani Kubwa sana Kwa Magufuli kwa Upendo wake kwa Tanzania na Watanzania. Nilimpenda zaidi Kwa Tabia yake ya Kutokumwogopa yeyote.
Bahaati Mbaya sana Magufuli anatabia Moja mbaya, Ni Mnafiki, sio Mkweli Kama anavyosema "Msemakweli ni Mpenzi wa Mungu" Inapofikia Katika Maswala ya Siasa Magufuli sio mkweli wala mwenye haki, inayofanana na Magufuli wa Ujenzi wa Taifa na Huduma za Jamii.
Unafiki wa wazi ni Pale aliposisitiza Kuwa ati Majaji walimwambia Kuwa Hawana haja ya Kuonekana Live, akiwa anaweka dhana Kuwa Majaji wanamuunga Mkono kwa Kuingilia Utendaji wa Bunge. Swala la Kukatisha matangazo ya TBC ilikuwa ni kwa Lengo la Kuubana Upinzani Bungeni na Kuruhusu Uonevu. Kusema Vinginevyo Ni Unafiki,
Swala Lingine Lilikuwa Ni swala la Zanzibar, Magufuli anajua wazi, Kikwete na Mkapa, walishinikiza Jecha Kufuta matokeo kwa Maslahi ya CCM, Magufuli anajua kuwa NEC, na ZEC sio Tume Huru. Magufuli anajua Uhuni Uliotendeka Zanzibar, Kwa yeye Kujifanya Jecha alifanya maamuzi yake Kikatiba Ni Unafiki.
Watu wanasahau Kuwa Sio Madictator wote Ni wa Aina ya Mobutu, Wengine walikuwa Madictator wa Kuchaguliwa na Watu waoliwaabudu, Madictator hao walikuwa Tayari kutoa damu yao Kuwapa watu wao Wainywe kama wana Kiu. Lakini kwenye Ukubwa wangemtoa yeyote Roho. Mfano halisi alikuwa ni Adolf Hitler. I hope Magufuli Ataacha Unafiki When it comes to Politic.
Mnamjua Mpanju yule Jamaa wa Bunge la Katiba, sasa Hivi kapewa Ukubwa Kwenye Wizara ya Sheria na Katiba.
Mnamkumbuka Makonda na siasa zake za maji taka, Naye Pia alikuwa Kwenye Bunge la Katiba, Magufuli sasa anampa Chapuo
Naaamini hata Bi Asha Bakari asingefariki, angepewa Madaraka Makubwa Kwa Kumtukana Jusa Bungeni! Huyo Ndiye Magufuli Mwanasiasa!
Sikiliza Maneno Yake Katika Sherehe za CCM, Msikilize Mpka Mwisho, Kuna Mahali aliropoka Ukweli, Kuonyesha Zanzibar ilikuwa Ni "Kukataa Kutawaliwa"