Magufuli na Mt.Petro: "majabali" Wawili katika enzi tofaiti.

SANCTUS ANACLETUS

JF-Expert Member
Mar 5, 2016
3,337
4,664
Tunaposema na kuvaa ujivuni juu ya kuzawadiwa imani Katoliki tunafanya hivyo baada ya tafakari ya kina sana.Baadhi yetu tunatembea kifua mbele na ujivuni wenye upole na unyenyekevu kwa kutambua kuwa ukweli,amani,utulivu,mshikamano,maendeleo na mapinduzi yoyote ya kitekenolojia ambayo dunia inayapitia sehemu kubwa chimbuko lake ni Kanisa Katoliki.

Leo nimebahatika kupata Kitabu ambacho kinachimbua historia ya Mtakatifu Petro,Mkuu wa Kwanza wa Kanisa lake Kristu,Kanisa Katoliki.Kitabu kimeandikwa na Mwanafasihi Padri Stefano Kaombe,wa Jimbo Kuu la Dar es salaamu.Sitaki kujadili kwa undani jinsi alivyomchambua Mt.Petro( Baba Mtakatifu wa Kwanza) kadri anavyoelezwa na Wainjili wanne kutoka Maandiko Matakatifu, bali nataka kumshukuru Mungu kwa jinsi anavyoweza kutung'amurisha mambo mbalimbali maishani mwetu kwa namna ya ajabu sana.

Ni hivi: dibaji ya Kitabu hicho " Mfahamu Mtakatifu Petro anavyosimuliwa na Wainjili" imeandikwa na John Pombe Joseph Magufuli.Ni muumini wa Kanisa Katoliki.Ni huyu huyu Raisi wa Tanzania.

Baada ya kusoma kitabu hicho juu ya tabia za Mtakatifu Petro na kuoanisha na tabia za Magufuli,ndipo nikang'amua jinsi Roho Mtakatifu anavyotimiza ahadi yake ya kulisaidia na kulitegemeza Kanisa kila wakati kwa namna ya ajabu sana.Sijui Mwandishi (Pd.Kaombe) akiulizwa ni kitu gani kilimfanya amchague Magufuli ndiye awe mwandishi wa Dibaji ya Kitabu chake atasemaje. Lakini mimi nimeng'amua kuwa pamoja na sababu zozote zinazoweza kutolewa na Mwandishi,ni Roho Mtakatifu kupitia Mwandishi amependa kumuimarisha na kumkamilisha Magufuli katika kazi ya uongozi wa nchi yetu kwa yeye kumsoma Mt.Petro na kisha kuandika kwa usuli juu ya kiongozi kama yeye,Petro,Kefa.

Ukisoma dibaji ya Magufuli katika Kitabu hicho utagundua ni Mtu mwerevu sana.Ni mtu ambaye anacho kipaji cha kuweza kuchambua mambo na akayapa tafsiri chanya kabisa! Uwezo na karama hii wamepewa wachache lakini kwa faida ya wengi.

Mtakatifu Petro,kwa muhutasari alikuwa na sifa zote chanya na hasi.Aliishi kama mtu jasiri.Alikuwa mwepesi wa kukubali majukumu yoyote aliyopewa na aliyoona ni stahili yake kuyahudumu.Mtakatifu Petro,aliifanya vizuri sana kazi ya utume na ya uongozi wa Kanisa.Ni yeye aliweka misingi ya Kanisa tunalojivunia Leo.Petro alichukua uongozi wa Kanisa katika kipindi kigumu sana wakati huo.Petro aliachiwa uongozi wa Kanisa kipindi ambacho "mafisadi" wa imani ya Ukiristo mayahudi na dola ya Kirumi(kisiasa) walikuwa hawana mchezo na yeyote anayejaribu kuhatarisha maslahi yao.Lakini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu kazi ya Petro matunda yake ndio tunajivuni nayo Leo.

Magufuli,alikubali kuandika dibaji ya kitabu kinachomwongelea kiongozi mwenzake (lakini Kiroho) pengine bila kujua kuwa anaweka summary juu ya mtu anayefanana naye kitabia.Na pengine hajalitambua hilo hadi wakati huu kitabu kinapokuwa sokoni.Pd.Kaombe pengine aliliona hilo kwa msaada wa Roho Mtakatifu na ndio kisa akamtwisha kazi hiyo.

Magufuli ni Kimbelembele sana kama alivyokuwa Petro.Magufuli ni mkurupukaji na mropokaji kama alivyokuwa Petro.Magufuli ni jasiri sana na yuko tayari kuchukua maamuzi yoyote madhali anaona mbele ya maamuzi hayo iko nuru.Petro alitawaliwa na tabia kama hii.Petro alikubali hata kutolewa uhai wake kwa ajili ya imani Katoliki isitawi.Magufuli alikubali kuachana na kujitenga na "falsafa" ya chama chake ya kuwajali matajiri na wenye fedha na kuwageukia maskini na wasio na tumaini.Yeye Magufuli anachukua toka mikono ya matajiri na kuweka katika mikono ya maskini.Anavua "samaki" kwa ajili ya wasio na kitoweo.Petro naye alikubali kuboresha kazi yake ya uvuvi toka ya kuvua samaki kwenda kuwa ya kuvua watu.Kazi ya kuhudumia watu kiroho na kimwili.Kazi ya kuchambua,kufafanua,kufundisha maadili na tunu za kimwili,kiakili na kiroho.Magufuli anaweka misingi ya utajirisho wa Tanzania.Anabadili Mikataba yenye masharti hasi.Anawaweka pembeni viongozi wenye mwelekeo hasi kihuduma za kijamii,kiuchumi na kisiasa.

Magufuli amefanana na Mt.Petro kwa majukumu yao.Wote walichukua majukumu ya kuongoza jamii zao katika vipindi vigumu sana.Kwa Magufuli,nchi yetu ilikuwa ni nchi iliyokosa mwelekeo baada ya kuondoka Mwalimu Nyerere.Nchi ilifikia kuwa mithili ya Lori linaloendeshwa na walevi.

Baada ya kusoma,kitabu hiki cha Pd.Kaombe nimepata mang'amuzi makubwa sana juu ya Magufuli na jinsi ambavyo Pd.Kaombe amekusudia kumuimarisha Magufili katika uongozi kwa kumukumbusha historia ya Kiongozi wa jamii kama yeye,Mt.Petro.

Nitaandika siku zijazo Kitabu juu ya Magufuli kuchambua ufanisi wake na kushindwa kwake kama ishara ya kumuunga mkono Pd.Kaombe.Historia za viongozi waliowahi kuishi huko nyuma zina mchango mkubwa sana katika kutuimarisha na kutuongoza nasi katika kazi zetu na wajibu wetu wa Leo.Na hiki ndicho alichokifanya Fr.Kaombe.

Basi nawaalikeni kwa mjadala.
 
Basi sawa. Tujivune taifa letu limebarikiwa sana mpaka tumepewa Petro wa pili hapa kwetu. Hakika tutatukuka dunia nzima nayo mataifa mengi kama si yote yatajengwa juu yetu.
 
Nisaidie kunijuza ,ni nini ambacho amefanya chenye manufaa kwa masikini . N.a. hao matajiri ni nini walichokosea hadi awanyang'anye ? N.a. mwisho uthibitisho upi kwa hayo(juu)?

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
M
Nisaidie kunijuza ,ni nini ambacho amefanya chenye manufaa kwa masikini . N.a. hao matajiri ni nini walichokosea hadi awanyang'anye ? N.a. mwisho uthibitisho upi kwa hayo(juu)?

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app

Mkuu ulizo lako sio jipya.Yesu mara baada ya kufufuka alijitokeza kwa wanafunzi na wafuasi wake kwa namna ya binadamu wa kawaida kabisa wakati fulani.Tukio mojawapo linaloakisi ukweli huo ni lile alipojiunga njiani na wafuasi wa Emau.Hawa wafuasi walikuwa wakitokea Yelusalemi kurudi makwao Emau.Wakati watu hao wakibadilishana mawazo juu ya jinsi Yesu alivyoweza kufufuka kadri alivyokuwa amejitabiria,Mara Yesu akajiunga nao na kuanza kuwauliza (huku aki-pretend hajui nini kilikuwa kimetokea Yelusalemi) juu ya uhakika wa walichokuwa wakikikiongelea.Wafuasi wale walimshangaa sana mtu Huyo (Yesu kabla hajajifunua kwao).Kwamba pamoja habari kuenea kote Yelusalemi na miji mingine bado yeye alikuwa hayuko aware na tukio kubwa kama lile.Yesu alifanya (ku-pretend) vile ili kutufundisha juu ya aina ya binadamu wanaoweza kutoona ama kutambua uwepo na ukweli wa mambo fulani licha ya matukio fulani fulani kutokea au kuwepo.Ni Fundisho juu ya baadhi yetu kushindwa kuona,kusoma na kutafakari matukio kadhaa yana ujumbe gani katika maisha yetu.Sijui nawe uko katika jamii ya namna hiyo.

Basi kwa ufupi sana Magufuli ameshafanya mengi kwa kipindi kifupi sana! Mambo haya yanajulikana hata kwa walio nje ya Tanzania(Yelusalemi). Amejenga mfumo wa uwajibikaji katika nafasi mbalimbali Serikalini. Ameleta nidhamu katika kazi na matumizi ya rasilimali fedha na maliasili za nchi.Anaboresha huduma za kijamii:elimu (ruzuku mashuleni,mimba kutoruhusiwa mashuleni) ,afya(gharama za dawa na matibabu zinashuka) ,na michezo(akina Kabulu na Malinzi wanasomeshwa kuwa soka la eneo la kujitajirishia.Je,wewe umefika Leo Tanzania?
 
Basi sawa. Tujivune taifa letu limebarikiwa sana mpaka tumepewa Petro wa pili hapa kwetu. Hakika tutatukuka dunia nzima nayo mataifa mengi kama si yote yatajengwa juu yetu.

Ama kwa hakika dunia itaweza chota majiundo anayoyafanya Magufuli.Tanzania na Afrika tunapata "utume" mpya kijamii,kiuchumi na Kisiasa.Basi,tuzidi kumwomba Bwana wa Mavuno amuzidishie nguvu za utendaji kwa ajili ya Watanzania.
 
Mtoa mada umemaliza kila kitu.
Rais Magufuli
akimaliza muda wake bila kubadilika(sidhanii) basi atakuwa ameyaishi maandiko yako.
Viongozi wengi wa Afrika zaidi huangalia maslahi ya matumbo yao tu ambayo ni ya muda mfupi sana.
Wanapoanza kutawala kwa kuchaguliwa kutokana na sera walizouza kwa raia, huanza kukiuka makusudi ahadi zao, wakienenda tofauti kabisa na sera walizochaguliwa kuzifuata.
Mtu yeyote mwenye akili timamu hapa Tz, asiyeegemea upande wowote,asiye mkabila wala mchama, hawezi kumsema vibaya Rais Magufuli.
Labda mtu huyo awe kazaliwa miaka ya karibuni, ambaye hawezi kupambanua tawala zilizopita.
Nimekuwa nikifikiri sana ambacho Magufuli anatakiwa kukifanya sasa cha muhimu zaidi kabla hajaondoka madarakani, ni katiba mpya, tena kuihuisha hiihii rasimu ya Warioba.
Wote waliokodishwa kwenda kutuvurugia kwenye bunge la katiba nyuso zao hatutaki kuziona tena.
Akifanya hivyo atakuwa ametupatia nyavu za kuvulia badala ya samaki anaotupatia hivi sasa. Nikimaanisha bila ya kuwa na sheria madhubuti, atakapomaliza muda wake, mibaka uchumi yatarudi "kamakawa".

Sent from my itel it1501 using JamiiForums mobile app
 
M


Mkuu ulizo lako sio jipya.Yesu mara baada ya kufufuka alijitokeza kwa wanafunzi na wafuasi wake kwa namna ya binadamu wa kawaida kabisa wakati fulani.Tukio mojawapo linaloakisi ukweli huo ni lile alipojiunga njiani na wafuasi wa Emau.Hawa wafuasi walikuwa wakitokea Yelusalemi kurudi makwao Emau.Wakati watu hao wakibadilishana mawazo juu ya jinsi Yesu alivyoweza kufufuka kadri alivyokuwa amejitabiria,Mara Yesu akajiunga nao na kuanza kuwauliza (huku aki-pretend hajui nini kilikuwa kimetokea Yelusalemi) juu ya uhakika wa walichokuwa wakikikiongelea.Wafuasi wale walimshangaa sana mtu Huyo (Yesu kabla hajajifunua kwao).Kwamba pamoja habari kuenea kote Yelusalemi na miji mingine bado yeye alikuwa hayuko aware na tukio kubwa kama lile.Yesu alifanya (ku-pretend) vile ili kutufundisha juu ya aina ya binadamu wanaoweza kutoona ama kutambua uwepo na ukweli wa mambo fulani licha ya matukio fulani fulani kutokea au kuwepo.Ni Fundisho juu ya baadhi yetu kushindwa kuona,kusoma na kutafakari matukio kadhaa yana ujumbe gani katika maisha yetu.Sijui nawe uko katika jamii ya namna hiyo.

Basi kwa ufupi sana Magufuli ameshafanya mengi kwa kipindi kifupi sana! Mambo haya yanajulikana hata kwa walio nje ya Tanzania(Yelusalemi). Amejenga mfumo wa uwajibikaji katika nafasi mbalimbali Serikalini. Ameleta nidhamu katika kazi na matumizi ya rasilimali fedha na maliasili za nchi.Anaboresha huduma za kijamii:elimu (ruzuku mashuleni,mimba kutoruhusiwa mashuleni) ,afya(gharama za dawa na matibabu zinashuka) ,na michezo(akina Kabulu na Malinzi wanasomeshwa kuwa soka la eneo la kujitajirishia.Je,wewe umefika Leo Tanzania?
Hayo yamedhihirika kwa matokeo au takwimu?

Ruzuku mashuleni kutolewa umejiridhisha tija iliyopatikana?

Kukamatwa viongozi wa vilabu/ Tff kumepandisha soka ?

Mimba hazijawahi kuhalalishwa mashuleni. HOJA ni " je,wahanga wanastahili nini-adhabu au mkono wa kuwapa ahueni?

Dhamira nzuri hupimwa kwa matokeo n.a. si kwa hatua pekee!

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Daaaa. unanikumbusha mambo yafuatayo kuhusu mtakatifu petro
  1. alishawahi kufokewa hadharani na mt palulo kwa kuwa na mambo ya kinafki
  2. alishawahi kumpa adhabu mtoto wake wa kumzaa awe mlemavu wa milele (ni wakristo wachache tu wanaojua hii story. na kuhusu huyu mtoto wa petro aliyekuwa mlemavu lakini baba ake akakataa kumponya)
  3. alishawahi kuporomoshewa matusi ya nguaoni na ndugu na majirani zake kwa kutelekeza familia yake
  4. ni muoga, aliwahi kukimbia nchi na kwenda uhamishoni badala ya kuhubiri neno. aliwakimbia wayahudi. hii tabia alikuwa nayo tokea mwanzo, ndio maaana alimkana yesu hadharani
  5. kama kiongozi wa kwanza kabisa wa kanisa alishindwa kuliunganisha kanisa, walithi wake katika uongozi ndio waliolijenga kanisa
  6. Hakuacha maandiko makubwa katika injili/au agano jipya kwa ujumla zaidi ya vibarua vyake viwili ambavyo haijulikani hata alimwandikia nani -labda mchepuko wake
  7. alizaliwa Bethsadia, mji mdogo huko galilaya karibu na ziwa genesereti. Akapindukia katika uvuvi wa samaki
  8. Alikuwa na ndugu (kaka) yake anaitwa andrea. Huyua andrea alikuwa mwanfunzi wa Yohana Mbatizaji
  9. Petro (simoni) kwa jina jingine ni KEFA au mwamba
  10. alikufa kwa kunyongwa, kichwa chini miguu juu. Inasemekana aliikana imani yake akitaraji kuachiwa huru na wanyongaji, jambo ambalo halikumsaidia.
 
Mtoa mada umemaliza kila kitu.
Rais Magufuli
akimaliza muda wake bila kubadilika(sidhanii) basi atakuwa ameyaishi maandiko yako.
Viongozi wengi wa Afrika zaidi huangalia maslahi ya matumbo yao tu ambayo ni ya muda mfupi sana.
Wanapoanza kutawala kwa kuchaguliwa kutokana na sera walizouza kwa raia, huanza kukiuka makusudi ahadi zao, wakienenda tofauti kabisa na sera walizochaguliwa kuzifuata.
Mtu yeyote mwenye akili timamu hapa Tz, asiyeegemea upande wowote,asiye mkabila wala mchama, hawezi kumsema vibaya Rais Magufuli.
Labda mtu huyo awe kazaliwa miaka ya karibuni, ambaye hawezi kupambanua tawala zilizopita.
Nimekuwa nikifikiri sana ambacho Magufuli anatakiwa kukifanya sasa cha muhimu zaidi kabla hajaondoka madarakani, ni katiba mpya, tena kuihuisha hiihii rasimu ya Warioba.
Wote waliokodishwa kwenda kutuvurugia kwenye bunge la katiba nyuso zao hatutaki kuziona tena.
Akifanya hivyo atakuwa ametupatia nyavu za kuvulia badala ya samaki anaotupatia hivi sasa. Nikimaanisha bila ya kuwa na sheria madhubuti, atakapomaliza muda wake, mibaka uchumi yatarudi "kamakawa".

Sent from my itel it1501 using JamiiForums mobile app


Ni kweli ndugu yangu.Umenena yaliyo ya kweli.Nami nina imani Katiba ya Warioba itakuja tu kabla ya Magufuli kuhitimisha muda wake.Zoezi la Warioba liliharibika sababu ya baadhi ya watu wanafiki.Watu walioenda huko Dodoma sababu ya posho na kujitafutia sifa binafsi.Hawa ndio Magufuli anajaribu kuwaweka kando.Nina imani ikifika zamu ya kuhuisha Katiba hiyo wanafiki kama hao hawatakuwa na nafasi kabisa.Basi na tumuombee.
 
Ama kwa hakika dunia itaweza chota majiundo anayoyafanya Magufuli.Tanzania na Afrika tunapata "utume" mpya kijamii,kiuchumi na Kisiasa.Basi,tuzidi kumwomba Bwana wa Mavuno amuzidishie nguvu za utendaji kwa ajili ya Watanzania.
....Tuwekee huo usuli nasi tuusome na tuyapime.

Sent from my CHC-U01 using JamiiForums mobile app
 
Hayo yamedhihirika kwa matokeo au takwimu?

Ruzuku mashuleni kutolewa umejiridhisha tija iliyopatikana?

Kukamatwa viongozi wa vilabu/ Tff kumepandisha soka ?

Mimba hazijawahi kuhalalishwa mashuleni. HOJA ni " je,wahanga wanastahili nini-adhabu au mkono wa kuwapa ahueni?

Dhamira nzuri hupimwa kwa matokeo n.a. si kwa hatua pekee!

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
Muelewe mtoa mada.
Sema ukilinganisha utawala wowote kuanzia Nyerere kuwa alifanya a,b,c bora sana na kwa tija kubwa kuliko anayoyafanya Magufuli, ukiweka takwimu zako, ndipo tutakapoona unamshipa na ubavu wa kukosoa.
Mtu anapotayarisha "site" kwa ajili ya kuiendeleza, lazima avuruge sana eneo hilo kusawazisha.
Katika matayarisho hayo, atachimba vifusi atang'oa miti isiyohitajika, nk nk.
Je utamuitia wanamazingira kumshitaki kuwa kaharibu mazingira kwa kukata miti na kung'oa visiki?
Mfano huo ndivyo inavyofanywa Tz iliyokuwa "ICU"kwa sasa, ambapo baadaye itajiset tu na kinachofanywa kwa kuwa kina malengo mema, lazima kitaleta tija.
 
Muelewe mtoa mada.
Sema ukilinganisha utawala wowote kuanzia Nyerere kuwa alifanya a,b,c bora sana na kwa tija kubwa kuliko anayoyafanya Magufuli, ukiweka takwimu zako, ndipo tutakapoona unamshipa na ubavu wa kukosoa.
Mtu anapotayarisha "site" kwa ajili ya kuiendeleza, lazima avuruge sana eneo hilo kusawazisha.
Katika matayarisho hayo, atachimba vifusi atang'oa miti isiyohitajika, nk nk.
Je utamuitia wanamazingira kumshitaki kuwa kaharibu mazingira kwa kukata miti na kung'oa visiki?
Mfano huo ndivyo inavyofanywa Tz iliyokuwa "ICU"kwa sasa, ambapo baadaye itajiset tu na kinachofanywa kwa kuwa kina malengo mema, lazima kitaleta tija.
....Ni chama gani kiliipeleka TZ ICU? Je kwa sasa tuna chama kipya chenye madaktari wapya kabisa from heaven?

Sent from my CHC-U01 using JamiiForums mobile app
 
Daaaa. unanikumbusha mambo yafuatayo kuhusu mtakatifu petro
  1. alishawahi kufokewa hadharani na mt palulo kwa kuwa na mambo ya kinafki
  2. alishawahi kumpa adhabu mtoto wake wa kumzaa awe mlemavu wa milele (ni wakristo wachache tu wanaojua hii story. na kuhusu huyu mtoto wa petro aliyekuwa mlemavu lakini baba ake akakataa kumponya)
  3. alishawahi kuporomoshewa matusi ya nguaoni na ndugu na majirani zake kwa kutelekeza familia yake
  4. ni muoga, aliwahi kukimbia nchi na kwenda uhamishoni badala ya kuhubiri neno. aliwakimbia wayahudi. hii tabia alikuwa nayo tokea mwanzo, ndio maaana alimkana yesu hadharani
  5. kama kiongozi wa kwanza kabisa wa kanisa alishindwa kuliunganisha kanisa, walithi wake katika uongozi ndio waliolijenga kanisa
  6. Hakuacha maandiko makubwa katika injili/au agano jipya kwa ujumla zaidi ya vibarua vyake viwili ambavyo haijulikani hata alimwandikia nani -labda mchepuko wake
  7. alizaliwa Bethsadia, mji mdogo huko galilaya karibu na ziwa genesereti. Akapindukia katika uvuvi wa samaki
  8. Alikuwa na ndugu (kaka) yake anaitwa andrea. Huyua andrea alikuwa mwanfunzi wa Yohana Mbatizaji
  9. Petro (simoni) kwa jina jingine ni KEFA au mwamba
  10. alikufa kwa kunyongwa, kichwa chini miguu juu. Inasemekana aliikana imani yake akitaraji kuachiwa huru na wanyongaji, jambo ambalo halikumsaidia.


Asante mkuu kwa kuongeza sifa hasi za Mtume Petro.Sasa ni Mtakatifu.Anatuombea Mimi na wewe tukitaka.Ndiye mwenye funguo za Mbinguni.Yeye ndo anafungua mlango wa Mbinguni na kisha Yesu anatukaribisha tuingie.Tabia zetu hasi ni fursa.Ni daraja tukizitambua na kukiri kuwa tuko hivyo ili tuweze kujikamilisha.Upungufu wetu katika maumbile ya nafsi zetu ndio kioo cha kutukamilisha.Binadamu tuko kama mbegu inayochipua.Mbegu inayochipua haina kila kitu.Haina majani.Haina Matawi na wala maua.Na ndege hawawezi kutua hapo na wala kujenga kiota juu yake.Lakini kadri ya muda,vyote vilivyokuwa vinapungua hujikamilisha na hivi hata kutoa faraja ya kivuli.

Petro sasa Mtakatifu alipungukiwa vingi sana kama ulivyoanisha lakini Yesu Kristu alimuchukulia kama Mbegu.Sote tuko hivyo kwa namna tofauti tofauti katika maisha yetu.Basi tuchukue udhaifu wetu kama fursa ya kujiunda na kujaribu kujikamilisha.
 
Muelewe mtoa mada.
Sema ukilinganisha utawala wowote kuanzia Nyerere kuwa alifanya a,b,c bora sana na kwa tija kubwa kuliko anayoyafanya Magufuli, ukiweka takwimu zako, ndipo tutakapoona unamshipa na ubavu wa kukosoa.
Mtu anapotayarisha "site" kwa ajili ya kuiendeleza, lazima avuruge sana eneo hilo kusawazisha.
Katika matayarisho hayo, atachimba vifusi atang'oa miti isiyohitajika, nk nk.
Je utamuitia wanamazingira kumshitaki kuwa kaharibu mazingira kwa kukata miti na kung'oa visiki?
Mfano huo ndivyo inavyofanywa Tz iliyokuwa "ICU"kwa sasa, ambapo baadaye itajiset tu na kinachofanywa kwa kuwa kina malengo mema, lazima kitaleta tija.


Hongera sana kwa kujazia palipopungua kwa weledi wa hali ya juu sana.Hivi ndivyo alivyofanya Yesu.Alipingana na Falsafa na itikadi za Kiyahudi na madhulumu ya Watawala wa Kirumi.Alivunjilia mbali makapu ya mayai hekaluni( ndio kutifua ardhi na kung'oa visiki).Aliasisi miongozo ya kimaadili na Kiroho.
 
Nadhani baadae sana wakatoliki hamtakawia kumpa magu utakatifu.

Ikistahili,ikipasa na kulazimu atapewa tu huo utakatifu maana ndio zawadi tunayoitiwa na Mungu.Utakatifu ni kilele cha kuumbwa kwetu.Yeye alituumba ili mwishowe tufurahi na kuishi naye milele pamoja na Viumbe vingine.Kwa hiyo sio jambo la kuonea aibu.Ikitokea amekidhi vigezo atatangazwa tu tena kwa nderemo,bashasha na shangwe kubwa na dunia itajua kuwa wakati huo ni Mtakatifu.Mambo yatawekwa hadharani.
 
Hana utakatifu wowote huyu fisadi, muongo, mwizi aliye na chuki za kutisha, mtu wa visasi na mwenye kupenda kutoa vitisho kila mara.

Mkuu yawezekana yuko hivyo kweli lakini kwa kiwango gani? Hakuna anayesema Nagufuli ni mkamilifu.Sisi tunasifu mazuri yake mengi.Tunafunua pia madhaifu yake ili ajikamilishe.Na ndio maana Mwandishi niliyemuongelea katika Kitabu ambacho yeye Magufuli alichokiandikia dibaji "amemchomekea" ili asome mapungufu ya Mwenzie (Petrol) na akiwezekana kama yrye Magufuli anataka kufaulu kama Mt.Petro ajiunde upya.Petro alifanikiwa kwa kutambua mapungufu yake na kujirudi.
 
Kiwango cha aliyofanya kinatosha kabisa kumuona yuko hivyo. Ukwapuzi wa nyumba za Serikali, kulidanganya Bunge kuhusu upotevu wa zaidi ya bilioni 200, ununuzi wa kivuko na ndege, ukwapuzi wa zaidi ya bilioni 16 za wahanga wa tetemeko na kuchota bilioni 100 kupeleka chato bila idhini ya Bunge.

Mkuu yawezekana yuko hivyo kweli lakini kwa kiwango gani? Hakuna anayesema Nagufuli ni mkamilifu.Sisi tunasifu mazuri yake mengi.Tunafunua pia madhaifu yake ili ajikamilishe.Na ndio maana Mwandishi niliyemuongelea katika Kitabu ambacho yeye Magufuli alichokiandikia dibaji "amemchomekea" ili asome mapungufu ya Mwenzie (Petrol) na akiwezekana kama yrye Magufuli anataka kufaulu kama Mt.Petro ajiunde upya.Petro alifanikiwa kwa kutambua mapungufu yake na kujirudi.
 
Back
Top Bottom