Magufuli kuwabana vigogo wa CCM

Magufuli kuwabana vigogo wa CCM

Kuondoa Tawala za Koo ndani ya CCM ni sawa na kujipiga risasi kifuani kuokoa pumbu zako. Ni ngumu sana.
e.g Makongoro Nyerere,Vita Kawawa, Riz Kikwete,Malima,Mwinyi,Msuya, Makamba na hivi karibuni Warioba Jr.
sijui itawezekanaje Dr.Pombe Magufuli uweze kuondoa hili la kubeba familia za viongozi ktk nafasi za utawala.
Kwa kuanzia anza na kuteua Mawaziri wasio na Majina ya Kifamilia za Kisiasa.

Tehe 😄 😄 😄 😄 🚶🏽
 
Kwan kipnd chote akiwa wazir hakuliona hilo aache danganya Toto anakumbuka shuka wakati kumepambazuka ? Elly ngoyai ndyo habar ya mjn
 
Huku nikufanganyana tuuuuuuuu nisawa na mwanao kampiga mwenzie ukaletewa mashta nakumwambia mwanao nitakuchapa ungetakiwa hapohapo kutoa adhabu uliluwa kiongozi ulifanya lipi kama mfano ??? Pipooooooz ndio mpango
 
Huyu baba nimuongo sijapata kuona anachotaka kufanya ni sawanamtu anayetaka kuwauwa panya waliopo ndani ya nyumba yake kwakuchoma nyumba moto wakati nayeye yuko ndani ya nyumba hiyo hivi unategemea ninikitatokeo?
 
Magufuli mbele kwa mbele hiki ni chama chetu mabadiliko tunayataka na uyafanye kivitendo sekta zote na ndani ya chama hadi 2020 wasiwe na agenda ya kuongea kwanza hapo walipo wameisha sambaratika
 
1.Source?
2. Ana jeuri hiyo? Akithubutu ajiadae kuwa rais maye si mwenyekiti wa CCM Taifa. Ana jua kilicho mpata 'Thambo Mbeki na ANC?'
3. CCM kwa maneno, hawajambo, mfn Kikwete 2005!!?? Huyu naye kaja kwa staili yake hupenda kumalizia neno kwa kusema hiiii........
 
Porojo za kampeni tu hizo...

Jaribu kutazama marais wote waliopita wana wao wamenufaika kutokana na vyeo vya baba zao...

Kuna daraja ukishalifikia huwezi kukwepa baadhi ya mambo, watoto wa Rais wa nchi hawawezi kuwa watoto tu wa kawaida kama wengineo na hata mke pia...

Dah, I can't wait to opt for magufuri, nimefurahi sana kuwaambia hata make wake aachwe aendelee na chaki make kusema kweli urais siyo wa familia, hatutaki rais wa kusongwa songwa tu na mamluki na watu kibao kana kwamba ni ufalme wa pepo ..Magufuri amenifanya nijisikie raha sana moyoni ..Hapo kazi tu mbwembwe mpe Lowassa
 
wanaosema hawezi wakapimwe akili Magufuli amesema ataweza wewe unasema hataweza shame of you
 
Hayo yana wezekana kupitia UKAWA.... Updates za kujivua magamba zikoje, zimeishia wapi? Chezea CCM?!

Magufuli hatudanganyiki.... mumesha tudanganya sana, huwezi kuua kunguni kwa kuchoma nyumba uliyomo. Wewe utabaki salama? Hoja za Kikwete wa 2005 zimeishia wapi? Usicheze na CCM, ila endelea kusema hivyo unaweza kuwa unaongeza kura kwa mpinzani wako.
 
kumbe na dr.magufuli unajua mfumo wa chama chako haufai hadi uubomoe
any way isikupe shida tutaubomoa wenyewe oct.
 
Hayo yana wezekana kupitia UKAWA.... Updates za kujivua magambazikoje, zimeishia wapi? Chezea CCM?!



Magufuli hatudanganyiki....mumesha tudanganya sana, huwezi kuua kunguni kwa kuchoma nyumba uliyomo. Weweutabaki salama? Hoja za Kikwete wa 2005 zimeishia wapi? Usicheze na CCM, ilaendelea kusema hivyo unaweza kuwa unaongeza kura kwa mpinzani wako.


Baba yake amekupigania, amekubeba ufike hapo ulipo leo, mwanayeusi mpe uwaziri, umerogwa? Mekengeza mpiga deal aliye wezesha upatikanaji wamabilioni upate mabango ya kutosha kila kona kukutangaza, upate mawe ya kutoshakuwalipa wenye malori, namabasi yao kukusombea hadhara, walio saidia chamakipate senti za kuwalipa wanao jaza hadhara ktk mikutano ya kampeni zenu Rais,makamu katili (bunge la katiba), wabunge na madiwani!!??

Hao wote wanao kauka koo kuokoa jahazi lako utawatosa wakishakamilisha safari na kukalisha kwenyekiti cha enzi? Kweli yanatoka moyoni nandiyo unayo ya amini? Kweli, kweli Kweli?


Apa hapa kwa IMANI ya dhehebu lako ili tupate kuku kumbusha Jan2016 endapo uatafakiwa kuukwaa Urais!?
 
Ya nini kuandikia mate na wino upo kwani mbali jawabu utalipata hiki ni chama cha mapinduzi
 
HUYU NDIYE RAIS NIMTAKAYE MIMI


~Asema atafumu mfumo wa utendaji ndani ya Chama


~Akerwa na vigogo kiwabeba watoto wao katika nafasi za uongozi


Zikiwa ni takribani siku 20 zimepita toka pazia la kampeni za uchaguzi mkuu zianze mgombea urais wa CCM Dkt. John Magufuli akutana na katibu mkuu wa chama hicho ambaye pia ndiye mwenyekiti wa kampeni za chama hicho na kumpa mambo anayotaraji kufanyika.


~Dkt. Magufuli ni mmoja ya mawaziri wachapakazi na wanaoogopwa sana kwa misimamo hata na Rais mwenyewe kwa jambo analoliamini analifanya kwa mujibu wa sheria,kanuni na taratibu. Amemuekeza Kanali Kinana kuwa moja hatapenda kuiona familia yake ikishiriki katika kampeni za urais kwani hataki familia yake kujihusisha au kujinasibisha na urais wa nchi. "Nataka nikapambane kufuta hili lililojengeka kwa watoto wa vigogo kubebwa kwenye nafasi za uongozi hata ajira na kuwaacha watoto wa watanzania maskini wakiwa mitaani eti kwa sababu hawana wa kuwashika mikono haki ya Mungu hili nitapambana nalo ili chama hiki kiwe cha wote na nchi hii iwe ya wote" Alisema kwa sauti ya ukali MAGUFULI


~Hivyo mke wangu naomba aachwe akafundishe, wanangu waendelee na mambo yao na hata ndugu zangu. Jukumu lao kubwa ni kuniombea kwa Mungu ili nikawatumikie watanzania kwa moyo wa dhati bila kiburi na majivuno.


~Asema kabla hajaapishwa anataka Chama chake kiandae utaratibu wa kuwabana wabunge wake hususani kupata ripoti za kila mwezi za kila mbunge juu ya utendaji wake kwa wananchi na mchango wake anapokuwa bungeni. Hii itasaidia kuwa na wabunge wanaochapakazi na kuwatumikia wananchi kuliki ilivyo sasa.


~Amesema akiingia Oktoba utaratibu wa kuwapa misamaha ya kodi wabunge imewafanya wasahau majukumu yao na kujiingiza kwenye biashara wakati wanalipwa vizuri na wanapata posho kubwa sasa amesema atafuta misamaha hiyo ili wajikite kuwatumikia wananchi.


~Asema atafumua utendaji wa chama kwa kukijengea chama uwezo zaidi kiuchumi ili watendaji wake na jumuiya zake walipwe vizuri na kuondoa michango ya gharama za kura za maoni na hata kuchangia gharama za uchaguzi kwenye majimbo ili kutoa fursa kwa vijana wanaotoka familia maskini kushiriki nafasi ya kuitumikia nchi yao kuanzia nafasi za mtaa, udiwani na ubunge hata urais. Pamoja na kufuta utendaji kazi wa mazoea.


~Asema siku 100 za mwanzo zitakuwa za kufanya mageuzi makubwa ndani ya serikali yake na Chama. Asema kama kuna kiongozi aliyeshiriki ufisadi wowote ajiandae maana atakula nao sahani moja ili sheria ichukue mkondo wake.

Chanzo chetu cha habari kinasema hata hivyo Kanali Kinana na Philip Mangula wamemuleza kumuunga mkono kwani ni mtazamo mzuri na watampa ushirikiano japo hautawapendeza wengi.

HUYU NDIYE RAIS WANGU
 
Angalia usije jutia kura yako. Fanya maamuzi ya busara. Jiepushe na lawama
 
Dah, I can't wait to opt for magufuri, nimefurahi sana kuwaambia hata make wake aachwe aendelee na chaki make kusema kweli urais siyo wa familia, hatutaki rais wa kusongwa songwa tu na mamluki na watu kibao kana kwamba ni ufalme wa pepo ..Magufuri amenifanya nijisikie raha sana moyoni ..Hapo kazi tu mbwembwe mpe Lowassa

Maneno haya matamu, ambayo yanaweza kabisa kumtoa nyoka pangoni, ingetakiwa, na si kwa Magufuli tuu bali kwa wasaka urais wote, yawekwe kama commitment na mhusika ajaze fomu jinsi atakavyotekeleza yooote aliyotamka, wapi atapata fedha, nani mtekelezaji, na muda wa utekelezaji. Fomu ionyeshe hatua atakazochukuliwa na bunge kama, baada ya muda kwisha, atakuwa hajatimiza alichoahidi. Kiufupi rais asaini mkataba wa kazi na wananchi na kila mwisho wa mwaka azunguke mikoa na wilaya zote wananchi wamfanyie tathmini ya kazi alizofanya sawa na ahadi alizotoa. Baada ya kumaliza wilaya zote bunge lihitimishe kwa kupitia mkataba wa rais na kutoa matokeo.
 
Back
Top Bottom