Click_and_go
JF-Expert Member
- Nov 21, 2010
- 451
- 5
WAZIRI wa Ujenzi, John Magufuli amekitaka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kiache kutoa watusi katika mikutano yake huku akikiombea dua akitaka "Kishindwe na kilegee katika jina la Yesu."
Alitoa kauli hiyo jana jioni, katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa shule ya Msingi, Chato ambao ulihudhuriwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye yuko katika siku yake ya nne ya ziara ya kikazi mkoani Kagera.
"Tulipata ugeni katika Wilaya yetu ya Chato lakini wakubwa wao hawakuja, hakuna cha msingi walichosema bali ni matusi tu. Mimi nasema washindwe, washindwe na walegee katika jina la Yesu" alisema huku akishangiliwa. Alisema Watanzania wanachotaka ni kuona wanatatuliwa matatizo yanayowakabili na hasa changamoto za barabara, walimu au maji na sio kusikia matusi katika majukwaa.
MWANANCHI MACHI 8 2011
naona anafanya siasa za ushabiki sometimes!!!