MAGUFULI anajua vyanzo vya mapato ya CCM

MAGUFULI anajua vyanzo vya mapato ya CCM

kipara kipya

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2016
Posts
20,142
Reaction score
24,446
Kitendo cha kuwakana wafanyabiashara mbele ya hadhira kuwa hawakuchangia na hawakudai hata senti na anaekudai asimame lilikuwa kosa kubwa ili hali kila mtu anajua kuwa hao watu wanamchango kufanikisha kampeni mpaka kuchaguliwa urais,kama mwenyewe ulivyojinasibisha kuwa huna kitu,hivi unafikiri mwenyekiti na genge lake wana furaha nawe haiwezekani sababu sura yako haikuonekana kwenye kukopa wala kuomba michango umekiachia chama mzigo wa madeni,sasa hawa malipo yao ilikuwa kuwachiwa wafanye watakavyo.

Angalia sasa wanaficha sukari ccm wanakukomoa sababu hao ndio wenye hivyo viwanda na hisa,mwenyekiti anajua lakini ana hasira amekuchunia yupo upande wa rafiki zake,kwani mtoto wa mkulima aliposema mafisadi wakifungwa nchi itayumba alimaanisha hao ndio wenye flow meter,sukari na bandari kavu. Na ndio vyanzo vya mapato ya chama sio viwanja wala kulaza magari wala shule,jua umeingilia mapato ya chama.

Angalizo huwa wanamchezo wa kubadilisha ubao wa matangazo mwenzio aliambiwa madawa ya kulevya akapambana nayo kweli kumbe maliasili na bandari na taasisi za umma wanamaliza,wewe wamekuwekea wa sukari sasa.Jivike mabomu ulipuke nao hakuna jinsi.
 
Umenena vema. Hujataja RVA feki. Eti kesi kashinda na sasa anaidai serikali Bilioni 60!!!! Hivyo mmiliki wa kiwanda hiki nani vile????!!!!!???
 
Umenena vema. Hujataja RVA feki. Eti kesi kashinda na sasa anaidai serikali Bilioni 60!!!! Hivyo mmiliki wa kiwanda hiki nani vile????!!!!!???
Si ni yule kipindi cha mchakato akatakiwa kuwaomba msamaha waislam.
 
Tusinfefika popote kama nchi kwa mwendo ule. Kaza buti Dr magufuli
 
Tusinfefika popote kama nchi kwa mwendo ule. Kaza buti Dr magufuli
Buti akaze kweli sababu familia imeshaanza kuficha vitu ndani ya nyumba,kesho watakufungia mlango usiingie
 
N
Kitendo cha kuwakana wafanyabiashara mbele ya hadhira kuwa hawakuchangia na hawakudai hata senti na anaekudai asimame lilikuwa kosa kubwa ili hali kila mtu anajua kuwa hao watu wanamchango kufanikisha kampeni mpaka kuchaguliwa urais,kama mwenyewe ulivyojinasibisha kuwa huna kitu,hivi unafikiri mwenyekiti na genge lake wana furaha nawe haiwezekani sababu sura yako haikuonekana kwenye kukopa wala kuomba michango umekiachia chama mzigo wa madeni,sasa hawa malipo yao ilikuwa kuwachiwa wafanye watakavyo.Angalia sasa wanaficha sukari ccm wanakukomoa sababu hao ndio wenye hivyo viwanda na hisa,mwenyekiti anajua lakini ana hasira amekuchunia yupo upande wa rafiki zake,kwani mtoto wa mkulima aliposema mafisadi wakifungwa nchi itayumba alimaanisha hao ndio wenye flow meter,sukari na bandari kavu.na ndio vyanzo vya mapato ya chama sio viwanja wala kulaza magari wala shule,jua umeingilia mapato ya chama.
Angalizo huwa wanamchezo wa kubadilisha ubao wa matangazo mwenzio aliambiwa madawa ya kulevya akapambana nayo kweli kumbe maliasili na bandari na taasisi za umma wanamaliza,wewe wamekuwekea wa sukari sasa.jivike mabomu ulipuke nao hakuna jinsi.
Nakumbuka kipindi Si kirefu akiwa waziri, matajiri wa malori waligoma wakapaki barabarani, mh. akasema kupaki ruksa ila majikoni kwenu....mwisho wa picha matajiri wakaibuka kidedea, tusubiri toleo lijalo....!.
 
Kazi kwelikweli!

20160508_080435.jpg
 
Kusema ukweli maghufuli anakazi kubwa Sana, maana yake mamafia wote wapo ccm
 
KaaaZi kweli kweli. Kuendesha nchi ni kazi nzito sana
 
Mama Salma amesema uchaguzi umekwisha, tuaache kusukumana sukumana...!!
 
Back
Top Bottom