Magufuli amekosea wapi, mbona 'anachuja' haraka?

Mimi tangu siku ile alopowaambia wafanyabiashara eti yeyote aliyenisaidia kwenye uchaguzi anyooshe mkono nikajua tu kuwa jamaa kweli kama mdau mmoja alivyosema hapo juu "NGUVU TEMBO, AKILI SUNGURA"
 

Magufuli hakosolewi kwa nia na adhma ya kupambana na ufisadi na ubadhirifu, bali kwa mikakati na mienendo iliyo na mwelekeo wa ubaguzi na kufifisha badala ya kuimarisha nguvu za mfumo wa dola. Ukiona mtu anapinga wezi kuchukuliwa hatua basi huyo ana tatizo kubwa.

Lakini mapambano haya hayatafika mbali endapo yataendelea kutegemea maamuzi ya mtu mmoja tu. Alianza vyema kwa kutikisa mfumo. Sasa aongeze na utashi wa kuimarisha mfumo imara usiojali mtu au chama. Kwa mfano, alichofanya kwenye uchaguzi wa meya DSM unaweza kukiita "real statesmanship". Ingawa inasikitisha kwamba CCM haijali kukiuka sheria na taratibu hadi "rais aseme". Hicho ndicho hatukitaki.
 
mkuu,nimekurushia pesa kwa m-pesa,uninunulie na mie,chenji itakayo baki ninulie mafuta ya kupikia,maana nayo yako mbioni kupanda bei...
Mkuu umesahau pia bei ya simu za mkononi inatarajiwa kupanda ifikapo 31 mwezi juni maana zile wanazoita feki zitazimwa. Bei ilishuka sana mpaka 15000 unapata simu sasa wakizima inamaana kariakoo watabakia na zile original hata kama nazo ni feki fresh ila watapandisha bei, sijui kama nalo hilo wanaliangalia au bado tupo kwenye kukamata sukari?????
 
Hata mke wake nasikia anataka kurudia kazi yake ya ualimu kwasababu ya visa vya jamaa. Akirudi home eti anataka akute pilau kuku wakati hela ya matumizi haachi.
 
Hapo unapotoka. Hicho ulichoandika ni nje ya UTAWALA WA SHERIA.Kwa hilo mimi nampongeza Mh kwa kuvumilia na kuchukua muda kujiridhisha. Tuache kulaumu kila mahali!
Vipi alivyomfukuza Kabwe hadharani?
 
Point! Unamwaga point baada ya point!
 
Kweli, ile approach sikuipenda. Rais anasimama hadharani kusema nimemuonya waziri........mkewe....! Haya mambo ya barabarani ni yakawaida na wakati mwingine hawa traffic wanakera sana unakuta kosa la kawaida anakuharasi sana hadi mimi saa nyingine huwa najiuliza au hawa polisi wanaonea wivu wenye magari? Rais ni amiri jeshi wa majeshi ya ulinzi na usalama anakaa na waandishi wa habari kuzungumza habari za koplo? Dah!
 
mamawe!dah,kibano kila angle!
 
Nadhani aliambiwa kuwa haikua sawa, ndiyo maana issue ya Airport hakufanya kama alivyofanya pale Darajani. Haikua sahihi kabisa!
Sasa si atanywea. Kwasababu jamaa alizoea kuzoa sifa kwa kufukuzafukuza hadharani.
 
Hata Lowasa mliambiwa muachane nae hana nguvu yoyote ya kuipasua ccm , mkakomaa ataipasua ccm.

Nilifikili mmejifunza kuwa siasa za kwenye mitandao hazina nafasi , kumbe bado. Nyumbu bwana ,subilini kuumia tena 2020.
 
Ni mazuri hayo ila gharama sasa.
Ila mlizoea sana kuishi kama malaika sasa mtaishi kama mashetani
Mimi naona kauli hii ya JPM imekaa kinyume. Nadhani majizi, mafisadi, wahujumu uchumi ndo Mashetani. Malaika ni wapole na hawaibi na si mafisadi. Sasa taifa la mashetani ni zuri kweli? Naona taifa la malaika ndo linafaa kuishi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…