Bado hajajibu swali,
Kwanini basi huyo wakala wa majengo asiwe yeye ndio mmiliki wa hizo nyumba za serikali? Yaani kwanini serikali isingeanzisha agency ya kuzisimamia hizi nyumba badala ya kuziuza?
Na ukiuza nyumba aliyokua akikaa labda mkuu wa wilaya, akija mpya atakaa wapi?
Inaingia vipi akilini uuze Nyumba kwa Million 20 (mapato) miaka 15 iliyopita, kisha uanze kuwalipia rent waliokosa Nyumba baada ya hizo kuuzwa labda jumla million 45 (matumizi) kwa kipindi chote hicho??
Unakiri kua idadi ya wafanyakazi wa serikali inaongezeka kila kukicha, kama waliokuwepo serikalini kipindi kile waliuziwa hizo nyumba, vipi walioko serikalini sasa watauziwa zipi? Huoni kama ni ubaguzi?
Nani alipanga bei za kuuzia hizo nyumba? Utauzaje nyumba iliyoko Prime location kama Bongoyo Street, Oyesterbay, Kiwanja Low Density (Sqm 4,000) kwa million 30?? Tena hela ambayo huikusanyi mara moja bali unakata kidogokidogo kwenye mishahara??
Category ya kuwachagua wafanyakazi wa kuzinunua ilikua ni nini? Wapo watu ambao waliuziwa kwanza Nyumba kabla ya kupata ajira serikalini. Magazeti ya Habari Corporation yakiwa chini ya Jenerali Twaha Ulimwengu yaliandika sana hii story, tena file la transfer of ownership alikua akilibeba Magufuli mwenyewe kulipitisha Department mbalimbali na ole wako ucheleweshe, huu ni ufisadi huu, hauwezi kufutika kwa sifa ya mtu tu kukariri idadi ya madaraja na kilomita za barabara, bado anabaki fisadi tu.
Hapa bana watu waliamua kujiuzia hizo nyumba kifisadi, na hata kama ni uamuzi wa baraza la mawaziri basi walihakikisha kila mmoja anapata nyumba kwake au kwa ndugu yake
Kwa hili naungana na
Zitto, yeyote alieshiriki huu ufisadi akiwemo Fredrick Tuluway Sumaye hatufai, na sio ws kuombea apitishwe hiyo tarehe 12-July