Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Magdalena Rwebangira, ametoa wito kwa Watendaji wa Uchaguzi kuhakikisha wanafuata kwa umakini Katiba, sheria, kanuni na miongozo yote inayosimamia mchakato wa uchaguzi nchini
Akizungumza akiwa Tabora wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Watendaji wa Uchaguzi ngazi ya mikoa na majimbo kwa mikoa ya Tabora na Kigoma, Mhe. Rwebangira amesisitiza umuhimu wa uelewa sahihi wa nyaraka za uchaguzi ili kuepusha mkanganyiko na changamoto zisizokuwa za lazima
"Someni kwa umakini katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na Maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume na ulizieni ili mpate kufafanuliwa kwenye maeneo ambayo kwa namna moja au nyingine kutakuwa na changamoto" alisema Rwebangira
Pia amewakumbusha washiriki wa mafunzo hayo kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuibua malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa au wadau wengine wa uchaguzi, akisisitiza kuwa uteuzi wa watendaji wa vituo uwe makini, ukizingatia maadili, uzalendo na weledi badala ya kuendekeza upendeleo wa kifamilia au kiundugu.
Mafunzo haya ya siku tatu yanalenga kuwajengea uwezo watendaji kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao, na yanatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 17, 2025
Chanzo: ITV
Akizungumza akiwa Tabora wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Watendaji wa Uchaguzi ngazi ya mikoa na majimbo kwa mikoa ya Tabora na Kigoma, Mhe. Rwebangira amesisitiza umuhimu wa uelewa sahihi wa nyaraka za uchaguzi ili kuepusha mkanganyiko na changamoto zisizokuwa za lazima
"Someni kwa umakini katiba, Sheria, Kanuni, miongozo na Maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume na ulizieni ili mpate kufafanuliwa kwenye maeneo ambayo kwa namna moja au nyingine kutakuwa na changamoto" alisema Rwebangira
Pia amewakumbusha washiriki wa mafunzo hayo kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuibua malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa au wadau wengine wa uchaguzi, akisisitiza kuwa uteuzi wa watendaji wa vituo uwe makini, ukizingatia maadili, uzalendo na weledi badala ya kuendekeza upendeleo wa kifamilia au kiundugu.
Mafunzo haya ya siku tatu yanalenga kuwajengea uwezo watendaji kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao, na yanatarajiwa kukamilika ifikapo Julai 17, 2025
Chanzo: ITV