Smiling killer
JF-Expert Member
- May 1, 2018
- 1,290
- 1,126
Niliisha jiachia kusoma magazeti
Na ule mradi bubu Dege kigamboniUDOM ilijengwa na fedha za NSSF sasa jiulize marejesho ni shilingi ngapi ? Badala yake magazeti ya hovyo yanakuja na habari za kutimuliwa Mkurugenzi Mkuu.Pengine Magazeti yanataka kuaminisha wasomaji wake tatizo ni Irene na si serekali inayokopa bila utaratibu wa kurejesha.Daraja la Nyerere fedha za NSSF jiulize kiasi gani kimerejeshwa ?.
Mkuu Ngongo, kwanza naunga mkono hoja,
Tanzania tuna a very serious problem kwenye media zetu, hatuna waandishi na wahariri competent wenye uwezo wa kufanya news analysis.
Mfano jana kama mlimsikia waziri Mhagama na Mkurugenzi wa SSRA kuhusu reasons za kikokotoo kipya ni hali mbaya ya mifuko ya PSPF na LAPF, baada ya kufanywa kwa actorial valuation ya afya ya mifuko hiyo, na ikabainika ilikuwa ife kufuatia formula yake ya 1/500.
Kwa vile mifuko hiyo miwili tayari ilikuwa on death bed, na sasa imekuwa merged into PSSSF, ili kuizuia PSSSF isife, baada ya jana rais kukirudisha kikokotoo cha zamani kilichokuwa kiuwe mifuko hii, ilitegemewa serious media ije na analysis of what does that mean.
Media zetu nyingi uwezo wake ni news reporting tuu na sio news analysis na hili niliwahi kulizungumza humu.
Vyombo Vya Habari Vya Tanzania, Havina Uwezo wa Uchambuzi wa Habari, News Analysis-Jicho Letu - JamiiForums
P
Ahsante sana Ndugu Pascal nilifikiri pengine ni Mimi nimeuona huu upumzike wa vijarida vyetu kumbe tuko wengi.
Fungueni vyuo vya uandishi au katuleteeni hao wazuri toka Rwanda na IndiaHakuna Cha kumuogopa Rais wala nini
Tanzania Hakuna Waandishi competent kuanzia Habar Za uchunguzi, Uchambuzi wala Za burudani
Tuna reporters wa Matukio tu
Mimi nimekoma siku nyingi pia ,nikipita nasoma vichwa habar kuchukua hint whats is on the news then natafuta hizo habari katika vyanzo vingine kama JFand twitter!
Watu wanafiki wanajitoa ufahamu,watu wapo na wana uwezo sasa je mnawapa uwanja mpana kuyaonesha wayajuayo.Nani anataka kufa.Yule Azori Gwandu si alitaka kuandika habari za kiuchunguzi comprehensively? Jambo lililompata sote tunalijua
Kwa ukongwe wako kwenye tasnia ya uandishi utakua unamkumbuka marehemu Stan Katabalo and what was his fate. Tanzania ni zaidi ya uijuavyo. Uhuru wa kuchunguza unamipaka tena mipaka mingine ni ya siri na ya hatari sana
Upo sahihi kabisa mkuuWatu wanafiki wanajitoa ufahamu,watu wapo na wana uwezo sasa je mnawapa uwanja mpana kuyaonesha wayajuayo.Nani anataka kufa.
Wanaenda shule kusomea ujinga.Kwa maneno rahisi vyuo vyetu vinazalisha wahitimu wa hovyo 😭
Ha ha ha haaaa... Nimecheka sana, uko very royal Mkuu, kwakweli Pasco huyu wa sasa hawezi kuthubutu tu hata kufikiria akilini mwake kufanya kipindi kama kile.A journalist ndiye huyo huyo reporter, being a reporter ndio the first stage ya journalist kwenye print media, baadae unapanda grades unakuwa staff reporter, unakuwa senior reporter, unakuwa specialized reporter, unakuwa sub editor, unakuwa chief sub, unakuwa editor, unakuwa Chief editor, hadi Editor in Chief.
Kwenye broadcast media unaanzia announce kutangaza kifuatacho, baadae unakuwa presenter, unakuwa program host, unakuwa producer, director, executive producer, manager, hadi mkurugenzi.
Kadri unavyopanda ndipo majukumu yanaongezeka
Kwa Tanzania kadri unavyopanda na kubobea ndivyo uoga unavyo ongezeka, kwa wale waliokuwepo wakati wa Kiti Moto, unadhani Pasco huyu wa sasa anaweza kuendesha kipindi kama kile?.
P
kukikoni ndio nini mkuu?Mleta mada pia unatujaza ujinga. Vichwa vya habari uvione wewe, sisi hatujaviona wala hujavigusia unatuambia vinasononesha na kusikitisha.
Kukikoni?
Umemaanisha nini kwa neno "royal" hapo mstari wa kwanza?Ha ha ha haaaa... Nimecheka sana, uko very royal Mkuu, kwakweli Pasco huyu wa sasa hawezi kuthubutu tu hata kufikiria akilini mwake kufanya kipindi kama kile.
So kwa kifupi tuseme HAKUNA UHURU WA MWANDISHI nchini.
😀😀😀Umemaanisha nini kwa neno "royal" hapo mstari wa kwanza?
Sijuwi nani mwenye afadhali Tanzania hii.
Kulikoni.kukikoni ndio nini mkuu?