Magazeti yana nini na Mh. Dr. Emanuel Nchimbi?

Magazeti yana nini na Mh. Dr. Emanuel Nchimbi?

Mpitagwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2012
Posts
2,338
Reaction score
1,126
WanaJF, kwa waliokuwepo ukumbi wa Nkrumah na kwa waliofuatilia mjadala wa jana kupitia ITV, watakubaliana nami kuwa kama kuna siku Nchimbi alionesha ukomavu wa kisiasa basi ni jana. Kwanza walimuwashia moto kama yeye, waliiwashia moto serikali kwa hali ya juu. Lakini alivyoinuka na kuanza kuongea, hakujibu matusi sana sana aliongea kama utani tu kwamba Dr. Slaa ni padri wake na yeye anamheshimu hivyo. Alijitahidi sana kujibu hoja zilizo kwenye uwezo wake na kuacha zile zilizo juu yake kama ya kumpandisha cheo Kamhanda. Hilo ni la JK mwenyewe. Na baadaye akakili ukweli kuwa kuna mazingira watu wanabambikiwa kesi na kutoa mfano. Cha ajabu magazeti ya leo yote hakuna hata moja lilimcover. Kunani kati ya Nchimbi na vyombo vya habari?

Mimi nilitegemea walau gazeti moja liandike waziri akiri serikali kusingizia watu kesi ili uibuke mjadala utakaopelekea kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya masikini wengi waliojaa magerezani kisa wamebambikiziwa kesi au hawana nguvu ya kisheria lakini wapi bwana. Waandishi hawako huko.

Ikumbukwe pia kuwa baada ya kumaliza kuongea alipigiwa makofi na watu wengi tu.

Binafsi ninampongeza Nchimbi kwanza kwa kuthubutu kwenda mlimani ambako boss wake anakuogopa kama nyoka, na pili kwa kutoa hotuba fupi ya kiutu uzima na kuonesha kuwa yeye ni mtawala.
Natamani ule mjadala wa jana wauone Nape na Nchemba ambao wanadhani kutukana ndiyo siasa. CCM tumeni watu kama Nchimbi kwenye mijadala sio watukanaji.


Ramadhan Kalim
 
Iam not a big fan of him lakini kweli alijitahidi
 
alinikela tu pale alivyosema lazima gesi ya mtwara hije dar kwa dharau kweliii...
 
Hata magazeti ya Uhuru na Mzalendo hayakuona pointi kutoka kwake? Unasema hata magazeti ya serikali waliona kabwabwaja tu? Namshauri amtake mkuu wake wajitathmini kukubalika kwao na wachukuwe hatua. Kukiri tu kuwa kweli polisi wanawambikia watu kesi hakutoshi bali anatakiwa afike mbali zaidi na kueleza ni hatua gani amewachulia wahalifu hao watesi wa wananchi wasio na hatia. Vingi walishakiri lakini hawana uduruki wa kuchukua hatua labda iwe kuwarushia mabomu chadema na kuwabaka wamakonde wanaotaka kujua manufaa ya gesi kwao.
 
Alijitahidi lakn hakuna haja sana ya kumwandika huyu jamaa mzee wa marathon na udaktari kabla ya thesis
 
Yaaaani kama umetumwa,unajua kwenye kiapo alisema maneno gani???

Yaaani unalalamika kuwa hajaandikwa kwenye magazeti!!!!!!! Kweli bora muumba akunyime mali kuliko maarifa,kipindi hiki kigumu cha maisha watu wanakufa kwa kukosa matibabu kwa wakati na yaliyo sahihi,watoto wanafeli mashuleni na vijana hawana ajira anajitokeza mtu na kulalamika waziri hajaandikwa gazetini!!!!!!!

Mental impontence!!!!!
 
Mkuu Mpitagwa,
Huyo anaitwa Emmanuel Nchimbi siyo Dr. Emmanuel Nchimbi. Rejea orodha ya mafisadi wa elimu kwenye kitabu cha Kenerugaba Msemakweli.
 
Last edited by a moderator:
Ulipomtaja Dr Slaa kama PADRI ukaharibu na mada nzima uliowasilisha hapa jamvini,Ramadhan Kalim.Wewe ni mdini.
 
Eti magazeti yangetoa heading zote kumsifia Nchimbi, who is Nchimbi by the way nasikitika magazeti yalikuwa yameapa kutokuandika habari za jeshi la polisi sasa yanaandika
 
Mkuu Mpitagwa,
Huyo anaitwa Emmanuel Nchimbi siyo Dr. Emmanuel Nchimbi. Rejea orodha ya mafisadi wa elimu kwenye kitabu cha Kenerugaba Msemakweli.
Hii sio hoja tena alishathibitisha kuwa ana Phd na ilisaishiwa external supervisor Udsm....wewe umetoka usingizini
 
Last edited by a moderator:
WanaJF, kwa waliokuwepo ukumbi wa Nkrumah na kwa waliofuatilia mjadala wa jana kupitia ITV, watakubaliana nami kuwa kama kuna siku Nchimbi alionesha ukomavu wa kisiasa basi ni jana. Kwanza walimuwashia moto kama yeye, waliiwashia moto serikali kwa hali ya juu. Lakini alivyoinuka na kuanza kuongea, hakujibu matusi sana sana aliongea kama utani tu kwamba Dr. Slaa ni padri wake na yeye anamheshimu hivyo. Alijitahidi sana kujibu hoja zilizo kwenye uwezo wake na kuacha zile zilizo juu yake kama ya kumpandisha cheo Kamhanda. Hilo ni la JK mwenyewe. Na baadaye akakili ukweli kuwa kuna mazingira watu wanabambikiwa kesi na kutoa mfano. Cha ajabu magazeti ya leo yote hakuna hata moja lilimcover. Kunani kati ya Nchimbi na vyombo vya habari?

Mimi nilitegemea walau gazeti moja liandike waziri akiri serikali kusingizia watu kesi ili uibuke mjadala utakaopelekea kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya masikini wengi waliojaa magerezani kisa wamebambikiziwa kesi au hawana nguvu ya kisheria lakini wapi bwana. Waandishi hawako huko.

Ikumbukwe pia kuwa baada ya kumaliza kuongea alipigiwa makofi na watu wengi tu.

Binafsi ninampongeza Nchimbi kwanza kwa kuthubutu kwenda mlimani ambako boss wake anakuogopa kama nyoka, na pili kwa kutoa hotuba fupi ya kiutu uzima na kuonesha kuwa yeye ni mtawala.
Natamani ule mjadala wa jana wauone Nape na Nchemba ambao wanadhani kutukana ndiyo siasa. CCM tumeni watu kama Nchimbi kwenye mijadala sio watukanaji.


Ramadhan Kalim
Inatakiwa ujiulize Mwangosi aliuliwa na nani na je yeye kama Waziri mwenye dhamana alichukua hatua gani? kwa hiyo vyombo vya habari bado vina kumbukumbu ya tukio hilo.
 
Hata mimi naona jana alijitahidi, nilikuwa na jamaa yangu pembeni nikamuuliza hivi huyu nchimbi kweli?
 
Du hata mm alinishangaza kwa kuwa na Confidence ya namna ile kwani majibu aliyapanga kiuhakika
Si mara ya kwanza hata wakati ule wa Jangwani issue ya ulimboka alienda na Waandishi hawahawa chini ya kina Nevile meena walimnanga, leo wasingeweza kumtoa kwenye Magazeti yao
 
niliguswa sana na kisa cha mtego wa panya! hadi slaa alinywea! chezea nchimbi ww!
 
mbona bungeni anaongea kama anaharisha?au kwa vile nje ya bunge hakuna hansard?siliamini gamba lolote
 
WanaJF, kwa waliokuwepo ukumbi wa Nkrumah na kwa waliofuatilia mjadala wa jana kupitia ITV, watakubaliana nami kuwa kama kuna siku Nchimbi alionesha ukomavu wa kisiasa basi ni jana. Kwanza walimuwashia moto kama yeye, waliiwashia moto serikali kwa hali ya juu. Lakini alivyoinuka na kuanza kuongea, hakujibu matusi sana sana aliongea kama utani tu kwamba Dr. Slaa ni padri wake na yeye anamheshimu hivyo. Alijitahidi sana kujibu hoja zilizo kwenye uwezo wake na kuacha zile zilizo juu yake kama ya kumpandisha cheo Kamhanda. Hilo ni la JK mwenyewe. Na baadaye akakili ukweli kuwa kuna mazingira watu wanabambikiwa kesi na kutoa mfano. Cha ajabu magazeti ya leo yote hakuna hata moja lilimcover. Kunani kati ya Nchimbi na vyombo vya habari?

Mimi nilitegemea walau gazeti moja liandike waziri akiri serikali kusingizia watu kesi ili uibuke mjadala utakaopelekea kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya masikini wengi waliojaa magerezani kisa wamebambikiziwa kesi au hawana nguvu ya kisheria lakini wapi bwana. Waandishi hawako huko.

Ikumbukwe pia kuwa baada ya kumaliza kuongea alipigiwa makofi na watu wengi tu.

Binafsi ninampongeza Nchimbi kwanza kwa kuthubutu kwenda mlimani ambako boss wake anakuogopa kama nyoka, na pili kwa kutoa hotuba fupi ya kiutu uzima na kuonesha kuwa yeye ni mtawala.
Natamani ule mjadala wa jana wauone Nape na Nchemba ambao wanadhani kutukana ndiyo siasa. CCM tumeni watu kama Nchimbi kwenye mijadala sio watukanaji.


Ramadhan Kalim

Wataandika kesho.
 
kwangu ccm ni kituko...ila jamaa jana alijitaidi
 
Back
Top Bottom