Ushauri wa sala, kwa wachagga (Wa-anjo, Waorombo, Wamachame, wakibong’oto, wakiwoso etc), na kwa majirani zao (upande wa Arusha na upande wa upareni), na kwa watanzania wote wanaoenda kijijini kwa sherehe za mwisho wa mwaka.
Kwahiyo, siku mmoja uwapo kijijini kwenye eneo lako la ukoo ukipenda unaweza ukafanya haya:
1) Chagua Jumamosi moja (siku ya saba ya wiki/Sabato takatifu).
2) Kwenye Jumamosi hiyo chagua mida ya saa tisa mchana.
3) Ingia chumbani, funga mlango, piga magoti sali. Kama ukitaka unaweza ukaelekeza sura yako kuelekea Jerusalemu, lakini ukiwa huifikirii Jerusalemu ya sasa, bali unaifikiria Jerusalemu mpya itakayoshuka kutoka mbinguni.
4) Kwenye sala yako tumia Jina la YAHWEH (Muumba wa Mbingu na nchi) na la mwanae Bwana Yahshua Masiha. Ukipenda, unaweza pia kusema Kanuni ya Imani ya Mkristo. Ukimaliza sala yako usisahau kusema: Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, YAHWEH wa Majeshi, Mbingu na Dunia zimejaa utukufu wako, hossana juu mbinguni, Amen.
5) Muombe Bwana asamehe madhambi yako na ya vizazi vya sasa na vilivyopita vya familia yako, ukoo wako, kabila lako, nchi yako, rangi yako, na wanadamu kwa ujumla. Muombe Bwana awape afya njema, furaha na mafanikio mazuri ya kiroho na kimwili katika maisha. Vile vile waombee wasidhuriwe na wasidanganywe na Shetani.
Of course note that Bwana Yahshua alizaliwa during the Feast of Tabernacles (ambayo this year iliangukia kwenye last week of September). Na mwaka wa kibiblia huwa una anza mwezi wa kwanza wa kibiblia ambao unaitwa Abib, ambao unaangukia March-April kwenye calendar hii tunayoitumia.
Unaweza kukuta familia yako au na ukoo wako umekua ukididimia kadri miaka inavyoenda. Sala hii inaweza ikapunguza kudidimia huko.
Sala hii, pia, inaweza kupunguza mapito mbali mbali ya kimaisha tunayo yapitia.
Nawatakia safari njema ya kwenda na kurudi kijijini kwenu.