Queen V
JF-Expert Member
- Jan 19, 2012
- 776
- 1,330
Hii imejulikana katika utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori(TAWIRI) wa kuchunguza mwenendo wa uzazi na ukuaji wa duma katika Mbuga ya Serengeti nchini Tanzania
Utafiti umerekodi ongezeko la vifo vya wanyama hao jamii ya paka katika miaka ya karibuni kutokana na kugongwa na magari ya watalii yaendayo kasi
Utafiti umebaini duma nane waliuawa kwa kugongwa na magari yaendayo kasi kati ya 2016 na 2018
Licha ya faini ya dola za kimarekani 5000 na kuzuiwa kuingia tena mbugani, bado tatizo la mwendokasi limezidi kuongezeka ndani ya mbuga hiyo
Duma ni wanyama wenye kasi ndogo ya kuzaliana na watoto wao hushambuliwa na wanyama wawindaji wengine kama fisi, simba na chui. Kati ya duma 100 wanaozaliwa, ni watatu tu huishi hadi ukubwani
My take:
Ikumbukwe duma anakimbia kilomita 100 hadi 120 kwa saa. Sasa hao wanyama wengine si ndo watamalizika kabisa?!!
Utafiti umerekodi ongezeko la vifo vya wanyama hao jamii ya paka katika miaka ya karibuni kutokana na kugongwa na magari ya watalii yaendayo kasi
Utafiti umebaini duma nane waliuawa kwa kugongwa na magari yaendayo kasi kati ya 2016 na 2018
Licha ya faini ya dola za kimarekani 5000 na kuzuiwa kuingia tena mbugani, bado tatizo la mwendokasi limezidi kuongezeka ndani ya mbuga hiyo
Duma ni wanyama wenye kasi ndogo ya kuzaliana na watoto wao hushambuliwa na wanyama wawindaji wengine kama fisi, simba na chui. Kati ya duma 100 wanaozaliwa, ni watatu tu huishi hadi ukubwani
My take:
Ikumbukwe duma anakimbia kilomita 100 hadi 120 kwa saa. Sasa hao wanyama wengine si ndo watamalizika kabisa?!!