Magari ya Rizwan

Magari ya Rizwan

Alisema siku moja'' HAPA MAISHA NI KIISHI KIMJINI MJINI TU.Tutasikia mengi ila hukumu yake ni pale raisi dhaifu atakapo toka ikulu.
 
mimi naona kama ni zake safi sana maana miela hakuikimbiza nje, za balali ziko wapi na zinafanya nini? bora huyu angalau anaweza kueleza ameshinda kesi ishirini kila moja milion mia tano au ana mkopo wa ADB, kwani kutakuwa na shida gani? hivi ukiwa mtoto wa Rais uwezi kukopa, tuache wivu tufanye kazi, tuangalie kaajiri watanzania wangapi?
 
Umekosea kk, huyo Nzi 1 ni gelesha tu ila hzo ni za Mkwewe aka Mzee wa Kudondoka dondoka. Nchi hii Chukua Chako Mapema (CCM). Hakuna cha ushahidi hapo ila ki ujumla hali ndo hio.
 
mawazo yote yapo sahihi wanaunga mkono kuwa malori ni ya riz sawa wanaopinga sawa. la muhimu je mawazo yenu ni ya kizalendo yanayoitakia mema Tanzania. kila mtu apime.kama kkuhoji ni kosa hata Zito basi hakuwa sahihi
 
EL kasema, tuache kulalamika na kupakana matope kwani ni dhambi R kuwa tajiri , nafasi aliyonayo kila mwekezaji anapenda aingie naye ubia jamani kuna mambo mengine tuache wivu, dogo kama ni magari yako hongera saaana usilale chapa kazi ,toa ajira huna sababu ya kurundika fedha nje, saidia watanzania wenzako .angalizo wajanja wengine wasiwe wanawatisha maofisa wetu pale mpakani kuwa magari ya R ili wapate unafuu fulani chunguzeni kwa makini hapo .
 
Itafika siku vitu vyote vitarudishwa kwa watanzania, kumbuka Azimio la Arusha au enzi za Mwalimu. Hivi hawa watu wanataka utajiri uwafikishe wapi?
 
Yaani kwa kusikia tu, ndo unataka kutuaminisha kuwa ni gari zake?!
Wengine hatuwezi kuishi maisha ya hisia tu, hata kama mtu hatumpendi... Hebu tutafutie ushahidi kwa hao watu waliokwambia ni gari zake!
 
naiba kupitia mwanangu...mliomba rais mkapata jizi,mkome kuringa,wabongo mnapenda sana wauza sura
 
Wanajf.
Hapa niko mpakani Namanga naona magari mapya ya kubebea mafuta zaidi ya 78 harakaharaka nilizoweza kuhesabu. Naambiwa ni za Rwizan zimetoka Nairobi kujengewa tank za mafuta. Sawali utajiri huu ameutoa wapi?
Na wewe kwa kuambiwa tu kuwa ni ya Rizwan umeamini kuwa ni yake kweli?
 
umu jamiiforum,mna matatizo makubwa ya kufikiria,mti kaona kauliza na kaambiwa ni gari za mtu flani, naye kakurupuka kuja jf na kuleta uzi,ushaidi tukikuuliza unao?
 
Kijana katumia vizuri nafasi ya mshua,Golden chance never come twice!!
Nasikia ana hisa lake oil ,anajenga kiwanda cha cement kigamboni duh
uuuuuuiiiiiiiiii Tanzania

Kuna mtu aliwahi kusema kwamba wabongo ni watu wanaopenda umbeya sana wape mada ya kujadili tu wataacha shughuli zao zote watakuwa wanajadili jambo hilo. Sasa hata huyu mtoa taarifa amesikia tu then anataka watu tujadili jambo ambalo halina ushahidi je huku si kutupotezea muda tuache kujadili mambo yenye fact tujadili kitu ambacho ni uzushi? Tuache mambo ya kinafiki kama unafact lete hoja tujadili ndio maana hata mawaziri wetu wamesha tufanya wajinga leo likizuka jambo hata kama linaukweli wanasema mwenye ushahidi alete then watachukua hatua na mambo yanaishia juju?
 
Nimemkopesha vijisent kidogo kutoka akaunti yangu ya uswizi ili angalau ipungue. Halafu shida yenu nyie Watanzania kila jambo kulalamika tu. Tukiweka hela uswizi, kelele, eti zitafutwe zirudishwe. Tukinunua magari tuwaajiri mpate mkate mkale na watoto wenu bado shida, kelele kibao. Tuwasaidie nini ili mridhike sasa. Kwa hiyo mnataka wooote tuwe na hela sawa hapa TZ? Haiwezekani. Lazima wawepo wa kufa maskini, na sie wa kuishi peponi hapa duniani. Mnyamaze mfikirie namna mtakavyoishi au kupambana kwenye hayo maisha yenu ya kila siku. Mnatuchosha na makelele yenu yasiyokuwa na mpango
 
Yapige picha na utuwekee picha humu ndani. Pia ni vizuri ungepata namba hata za magari matano.
 
Kautoa Tanzania.

Utajiri kautoa kwenye kodi yako ya kibiriti na chunvi unavyo tumia kilasiku pamoja na kodi nyingine zote unazozijua wewe za hapa Tanzania. a corrupt ruling part of CCM will never leave power in the country unless through people revolution(peoples power as it was in Egypt or by military revolution, politically will take many years if not impossible!
 
Back
Top Bottom